Ndugu. Mwenyekiti salama?
Natumaini upo salama muda huu hapo Dubai, huku Dar es Salaam hali shwari kwa maskini na wanyonge ila si salama kwa wasaka madaraka!
Sina lengo la kukushtua ukatishe ziara nina lengo la kukupasha habari kazi yetu sisi ni kukuhabarisha.
Umbea wa mjini kidogo pamoja na hali ya Uliyoiacha nyuma huku najua nikituma kwa njia ya kawaida kiutendaji taarifa hizi hazitafika hata kidogo kwako ngumu kidogo machoni pawengi, lakini nitaeleweka bila mawaa wala chembe ya makunyazi.
Siasa tuiache kando siku ya leo profesionalism (Uweledi) ichukue nafasi yake, ni muda mrefu sasa mfumo wa utendaji kazi wa idara nyeti ni kama unahujumiwa na kikundi kidogo cha watu wenye nafasi ya kupokea taarifa kutoka vyombo vyote vya usalama katika kulitumikia taifa la Tanzania.
Ndugu Mwenyekiti idara hii sote tunafahamu ipo chini ya ofisi yako. hii inamaana kuwa mkuu wa idara hii anaripoti kwako moja kwa moja, pia mkuu wa idara hii huteuliwa na Ofisi yako kwa kuzingatia vetting maalumu.
Muundo wetu kiutendaji umegawanyika katika sehemu sita kiutendaji ambapo kuna idara ndogondogo ndani ya idara kubwa nazo ni idara ya mambo ya ndani, dawati la siasa, dawati la mambo ya nje, dawati la uchumi, dawati la ukusanyaji taarifa, dawati la uchakataji taarifa na Dawati la amani utatuzi wa migogoro (vita nk).
Mhe. Mwenyekiti barua hii haina nia ya lengo la kumwaga ugali bali inalengo la kurekebisha mifumo iliyopo ndani ya Taasisi.
Hapa nataka kuzungumzia idara ya siasa ambayo ndio kila leo inayoiweka serikali kwenye upande wa kujibu hoja zote za Wananchi na kukuambia yale tunayokumbana nayo mtaani kila kukicha. Ila kwasasa dawati hili ni defensive side.
Ulinzi wa chama na serikali unategemea sana idara ya siasa ni muhimu kiutendaji kwako na ufanisi wa serikali yako.
Mhe Rais umefanya ziara tatu kubwa nje ya mipaka ya Tanzania ndani ya kipindi cha miezi miwili.
1. Mkutano na Rais wa Msumbiji Felipe Nyusi mji wa Pemba mkutano ulizungumzia hali ya siasa na matishio ya ugaidi.
2. Umeitembelea Ufaransa na Ubegiji na kufanya mazungumzo na viongozi wakubwa zaidi Duniani wakuu wa Taasisi kubwa na washauri mashuhuri mbalimbali.
3. Ukiwa Belgium umekutana na Mhe. Lissu hali iliyoleta matumaini kwa wengi juu ya muuafaka wa kisiasa na kuliunganisha Taifa.
Pamoja na yote haya mazuri uliyoyafanya bado kuna idara isiyotimiza wajibu wake kwa utendaji wako. Kuna idara inayopokea taarifa nje na maelekezo zaidiyako Mhe. Mwenyekiti kuna sauti inayowaambia msifanye hayo. Si kwasababu wana nguvu kukuzidi ila sababu ni upofu wa madaraka.
Pamoja na serikali yako kujitahidi kuendeleza miradi iliyoachwa na mtangulizi wako kwa kasi na ukubwa na viwango na mingine ipo mbioni kumalizika. Jitihadi kabambe zinafanyika kufifisha jitihadi zako nzuri.
Mambo yamekuwa yakifanyika gizani umenyimwa Fursa ya kutamba kwa Wema wako Taifa hili. kwa Leo sitawataja majina ila napenda niweke wazi. Baadhi ya ofisi zinazoshindwa kwenda na kasi yako.
Ofisi ya msemaji Mkuu wa serikali./ kurugenzi Idara habari Maelezo.
Sijui nani ndiye muhusika wa kusema na Kutoa Taarifa juu ya utendaji wa serikali lakini kwa hapa nikujulishe wazi hakuna msemaji bali unamtimiza majukumu tu. Why?
Incident ya kwanza Rais alisafiri kutoka Zanzibar hadi Paris na ndege ya abiria wa kawaida, jambo hili lilikuwa wazi halikusemwa likafichwa kutengeneza mazingira Rais anatumia Pesa za walipa kodi vibaya. Kibinadamu tulijua kapitiwa ila kutenda kosa si kurudia kosa. Pwani tunasema kosa moja haliichishi mke.
Accident tunamaanisha kama hakutarajia nasi jambo la pili lilikuwa ni ajali. Rais alirejea na ndege ya abiria kutoka Brussels hadi Tanzania hakuna Taarifa iliyotolewa badala yake ikajenga picha Rais amerudia kufuja Pesa.
Jambo la tatu huu ni mpango wa wazi (Planning ambushing) kuingia kwa kichwa cha Treni ya majaribio nchi inafahamika wazi kabla ya mkandarasi kukabidhi mradi lazima afanye majaribio ya njia katika mradi wa reli ya Mwendokasi (Reli ya Umeme).
Taarifa ya ujio wa kichwa cha majaribio ilikuwa wazi kwa maelekezo ya upotoshaji Taarifa haikuwekwa bayana. Aliyekuwa msemaji aliwahi kuhudumu Kama Mkuu wa kitengo cha mawasiliano ya Rais Ikulu anafahamu aina ya kichwa kitakachokuja kama usafiri na mkataba upo na kampuni ya Korea.
Hatakiwi kuwa defensive alitakiwa kuhabarisha umma kuwa tunayatarajia haya siku na muda huu kitakachofika si mali yetu ni kwa ajili ya majaribio.
Mhe Rais Dawati lina jukumu la kufuatilia na kutambua mienendo ya wanasiasa viongozi na watu wote katika taifa, inahusisha mawasiliano yao, email zao, mizunguko yao ya kila siku, vipato vyao nk.
Idara bila shaka inazo Taarifa muhimu kwa kutelekezewa Wizara ya Nishati kwa Mhe Waziri peke yake. Umeme ni wa Waziri na kukatika umeme ni kwa Waziri. Utakapokatika umeme ni Waziri, hakuna utendaji wa collective efficacy kimuundo wa serikali.
Upo mchezo wa baadhi ya Ofisi inazopokea Taarifa nyeti Na kuzitumia kujinufaisha nazo wenyewe kwa maslahi yao binafsi.
Ni uhujumu na usaliti endapo ofisi ya msemaji Mkuu wa serikali itafanya kazi kwa maslahi ya kikundi cha watu wachache. Idara ya usemaji wa serikali si mdomo wa ofisi ya watu wachache ni jukumu la kusemea na kutolea ufafanuzi kila jambo muda wote na wakati wote wa uhai wa serikali.
Kwa Taarifa katika maonyesho ya kibiashara umefanya mengi yameonekana kwenye picha najua tutapewa machache mengine yatafichwa kwa ajili ya propaganda chafu dhidi yako.
Asante Mwenyekiti.
Natumaini upo salama muda huu hapo Dubai, huku Dar es Salaam hali shwari kwa maskini na wanyonge ila si salama kwa wasaka madaraka!
Sina lengo la kukushtua ukatishe ziara nina lengo la kukupasha habari kazi yetu sisi ni kukuhabarisha.
Umbea wa mjini kidogo pamoja na hali ya Uliyoiacha nyuma huku najua nikituma kwa njia ya kawaida kiutendaji taarifa hizi hazitafika hata kidogo kwako ngumu kidogo machoni pawengi, lakini nitaeleweka bila mawaa wala chembe ya makunyazi.
Siasa tuiache kando siku ya leo profesionalism (Uweledi) ichukue nafasi yake, ni muda mrefu sasa mfumo wa utendaji kazi wa idara nyeti ni kama unahujumiwa na kikundi kidogo cha watu wenye nafasi ya kupokea taarifa kutoka vyombo vyote vya usalama katika kulitumikia taifa la Tanzania.
Ndugu Mwenyekiti idara hii sote tunafahamu ipo chini ya ofisi yako. hii inamaana kuwa mkuu wa idara hii anaripoti kwako moja kwa moja, pia mkuu wa idara hii huteuliwa na Ofisi yako kwa kuzingatia vetting maalumu.
Muundo wetu kiutendaji umegawanyika katika sehemu sita kiutendaji ambapo kuna idara ndogondogo ndani ya idara kubwa nazo ni idara ya mambo ya ndani, dawati la siasa, dawati la mambo ya nje, dawati la uchumi, dawati la ukusanyaji taarifa, dawati la uchakataji taarifa na Dawati la amani utatuzi wa migogoro (vita nk).
Mhe. Mwenyekiti barua hii haina nia ya lengo la kumwaga ugali bali inalengo la kurekebisha mifumo iliyopo ndani ya Taasisi.
Hapa nataka kuzungumzia idara ya siasa ambayo ndio kila leo inayoiweka serikali kwenye upande wa kujibu hoja zote za Wananchi na kukuambia yale tunayokumbana nayo mtaani kila kukicha. Ila kwasasa dawati hili ni defensive side.
Ulinzi wa chama na serikali unategemea sana idara ya siasa ni muhimu kiutendaji kwako na ufanisi wa serikali yako.
Mhe Rais umefanya ziara tatu kubwa nje ya mipaka ya Tanzania ndani ya kipindi cha miezi miwili.
1. Mkutano na Rais wa Msumbiji Felipe Nyusi mji wa Pemba mkutano ulizungumzia hali ya siasa na matishio ya ugaidi.
2. Umeitembelea Ufaransa na Ubegiji na kufanya mazungumzo na viongozi wakubwa zaidi Duniani wakuu wa Taasisi kubwa na washauri mashuhuri mbalimbali.
3. Ukiwa Belgium umekutana na Mhe. Lissu hali iliyoleta matumaini kwa wengi juu ya muuafaka wa kisiasa na kuliunganisha Taifa.
Pamoja na yote haya mazuri uliyoyafanya bado kuna idara isiyotimiza wajibu wake kwa utendaji wako. Kuna idara inayopokea taarifa nje na maelekezo zaidiyako Mhe. Mwenyekiti kuna sauti inayowaambia msifanye hayo. Si kwasababu wana nguvu kukuzidi ila sababu ni upofu wa madaraka.
Pamoja na serikali yako kujitahidi kuendeleza miradi iliyoachwa na mtangulizi wako kwa kasi na ukubwa na viwango na mingine ipo mbioni kumalizika. Jitihadi kabambe zinafanyika kufifisha jitihadi zako nzuri.
Mambo yamekuwa yakifanyika gizani umenyimwa Fursa ya kutamba kwa Wema wako Taifa hili. kwa Leo sitawataja majina ila napenda niweke wazi. Baadhi ya ofisi zinazoshindwa kwenda na kasi yako.
Ofisi ya msemaji Mkuu wa serikali./ kurugenzi Idara habari Maelezo.
Sijui nani ndiye muhusika wa kusema na Kutoa Taarifa juu ya utendaji wa serikali lakini kwa hapa nikujulishe wazi hakuna msemaji bali unamtimiza majukumu tu. Why?
Incident ya kwanza Rais alisafiri kutoka Zanzibar hadi Paris na ndege ya abiria wa kawaida, jambo hili lilikuwa wazi halikusemwa likafichwa kutengeneza mazingira Rais anatumia Pesa za walipa kodi vibaya. Kibinadamu tulijua kapitiwa ila kutenda kosa si kurudia kosa. Pwani tunasema kosa moja haliichishi mke.
Accident tunamaanisha kama hakutarajia nasi jambo la pili lilikuwa ni ajali. Rais alirejea na ndege ya abiria kutoka Brussels hadi Tanzania hakuna Taarifa iliyotolewa badala yake ikajenga picha Rais amerudia kufuja Pesa.
Jambo la tatu huu ni mpango wa wazi (Planning ambushing) kuingia kwa kichwa cha Treni ya majaribio nchi inafahamika wazi kabla ya mkandarasi kukabidhi mradi lazima afanye majaribio ya njia katika mradi wa reli ya Mwendokasi (Reli ya Umeme).
Taarifa ya ujio wa kichwa cha majaribio ilikuwa wazi kwa maelekezo ya upotoshaji Taarifa haikuwekwa bayana. Aliyekuwa msemaji aliwahi kuhudumu Kama Mkuu wa kitengo cha mawasiliano ya Rais Ikulu anafahamu aina ya kichwa kitakachokuja kama usafiri na mkataba upo na kampuni ya Korea.
Hatakiwi kuwa defensive alitakiwa kuhabarisha umma kuwa tunayatarajia haya siku na muda huu kitakachofika si mali yetu ni kwa ajili ya majaribio.
Mhe Rais Dawati lina jukumu la kufuatilia na kutambua mienendo ya wanasiasa viongozi na watu wote katika taifa, inahusisha mawasiliano yao, email zao, mizunguko yao ya kila siku, vipato vyao nk.
Idara bila shaka inazo Taarifa muhimu kwa kutelekezewa Wizara ya Nishati kwa Mhe Waziri peke yake. Umeme ni wa Waziri na kukatika umeme ni kwa Waziri. Utakapokatika umeme ni Waziri, hakuna utendaji wa collective efficacy kimuundo wa serikali.
Upo mchezo wa baadhi ya Ofisi inazopokea Taarifa nyeti Na kuzitumia kujinufaisha nazo wenyewe kwa maslahi yao binafsi.
Ni uhujumu na usaliti endapo ofisi ya msemaji Mkuu wa serikali itafanya kazi kwa maslahi ya kikundi cha watu wachache. Idara ya usemaji wa serikali si mdomo wa ofisi ya watu wachache ni jukumu la kusemea na kutolea ufafanuzi kila jambo muda wote na wakati wote wa uhai wa serikali.
Kwa Taarifa katika maonyesho ya kibiashara umefanya mengi yameonekana kwenye picha najua tutapewa machache mengine yatafichwa kwa ajili ya propaganda chafu dhidi yako.
Asante Mwenyekiti.