BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,020
Atawarudisha CCM kwa gharama yoyote ile ikiwemo kuwapa rushwa ya mamilioni au vyeo au kuwatishia kuwabambikia kesi nzito ili kuwatia hatiani na kuwaswekwa lupango.
Ni wazi kuwa watu wanarudi ccm sio kwa mapenzi ya moyo wao bali kutokana na vitisho vya jela au uharibifu wa mali zao. Sio wote wana mioyo migumu kama Mbowe ambaye unambomolea kitega uchumi, anaharibiwa shamba lake la kisasa huku watu wanapiga selfie ili wapandishwe vyeo na hujuma zingine lakini hababaiki.
Kwa hili huwezi kusifia ccm kuwa inavutia wananchi ili waiunge mkono bali ni uhalifu wa kisiasa na watu wanaenda huko kujiokoa na dhahma kwa maisha yao. Ni sawa na kumtaka mwanamke huku umeshika panga na akakubali kisha unajisifu unapendwa naye ndio maana kakupa ushirikiano wakati huo ni ubakaji.
CCM inambaka Wema kisiasa.