Msanii Joseph Haule (Prof. Jay) ajiunga CHADEMA

Msanii maarufu wa bongo flava Joseph Haule aka Proffesor Jay, leo hii amejiunga na chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA na kukabidhiwa kadi yake ya uanachama mjini Dodoma.

View attachment 94612 View attachment 94613

Huyu alikuwa ameisha jiishia zamani, hana tena Dili ndani ya muziki wa bongo fleva, alikuwa hana option zaidi ya hiyo , ili kujiliwaza kwani hata ndani ya medani ya muziki wa kizazi kipya hayumo tena , wakina Diamond wameisha mmaliza na kufanya jina lake lisahaulike. Kwa heri, kwa heri baba, kila wafu huzika wafu wenzao.
 


hapo nilipo-bold in red naomba "UWAOMBE RADHI WANANCHI WA ZANZIBAR KWA KUUSEMA KATIKA HALI YA KUDHALILISHA USOMI WA KIONGOZI WAO MKUU HAYAT KARUME SENIOR"

PIA INAKINZANA KWA HALI YA JUU SANA NA MATENDO YA KISHUJAA ALIYOWAHI KUYAFANYA HAYATI KARUME NA PIA IKUMBUKWE MBALI NA KUWA BAHARIA ASIYESOMA ALIKUWA NI MTENDAJI NA MFUATILIAJI WA MAMBO MPAKA LEO HAKUNA ALIYEWEZA KUVUNJA REKODI YA HAYATI KARUME YA UTENDAJI WA MAMBO MAKUBWA KWA KIASI KIDOGO CHA PESA NA KWA MUDA MFUPI WA UTENDAJI....

NA USIPOKUWA MAKINI UNAWEZA KUHATARISHA MUUNGANO WETU ULIODUMU MIAKA DAHARI NA DAHARI...BUT MIND YOUUUU...NI MUASISI PIA WA CCM YAKOOOOOOO....SO DOGO UNAPO-ONGELEA ELIMU UNARUSHA JIWE NYUMBA YA JIRANI WAKATI YA KWAKO NI YA VIOOOOOOO.
 
Kwangu ni mapinduzi mapya kuelekea kuwafanya vijana kuelewa nini tunataka 2015! Kudos Prof Jay binafsi nitaunga mkono harakati zako.
 
Hongera prof.J,Njoo mikumi umpe tafu DR. aliyegombea uchaguzi uliopita achukue jimbo.
 
Sasa Mkuu wa Kaya anavyopenda Bongo flava atasikiliza za akina nani? Na CDM now ni ya wasaniiii auuuuu

Msanii wa bongo fleva mwenye mvuto na kupendwa na watu wote ni Diamond, wengine hakuna kitu kwa sasa. Na yeye ndiye anaye ongoza kwa kipato ndani ya bongo fleva. Prof. Jay hakuna kitu tena, ni oil chafu hiyo mkuu
 
Siasa si dhambi lkn pamoja na ushujaa lakini siku chache zijazo utasikia anabambikwa kesi na kuswekwa rumande, kisa mpinzani... Siku moja majiwe yatanena...
 
hapo prof jay anamwambia jk "aikemee serikali yake katika madudu inayoyafanya".

Lakini jk alidhani masihara, ikabidi jay ahamie kwa watu wanaotaka ukombozi wa kweli.

Cc: mohamedi mtoi, molemo, @crushwise, bujibuji, ben saanane, ndibalema

huyo dogo aliyepo-katikati ya prof j na dr. Jk mie huwa simuamini hata kidogooo..ni kigeugeu ndani ya dakika sifuri anawasaliti...pleaseee prof kama umekuja huku kwenye movement muambie huyo dogo wa kati anahitaji kupevuka ki-fikra na kuwa na upeo mkubwa kisiasa ingawa tayari anao upeo huo ki-muziki ndipo afikirie kujiunga huku ulikotukuta na tukakupokea.
 
Naona hamna aliyemkaribisha JF!

Jay, kama umeingia rasmi kwenye siasa za wazi na mapambano ya hoja pia tunakukaribisha JF.
Kuna wadau watakupika hapa, pia utaweza kuiona kwa upana siasa ya tz tokea kwenye jicho la mitandao ya kijamii.....
Bado Master J na Salama.
 
Huwa ni nadra kuchangia mada humu JF. Lakini kwa maamuzi magumu na sahihi kama haya aliyoyafanya Prof. Jay sina budi kusema "BIG UP Prof. Jise"
 

Msanii wa bongo fleva mwenye mvuto na kupendwa na watu wote ni Diamond, wengine hakuna kitu kwa sasa. Na yeye ndiye anaye ongoza kwa kipato ndani ya bongo fleva. Prof. Jay hakuna kitu tena, ni oil chafu hiyo mkuu

Huyu aliyefunzwa lugha na Wema
 
Ubunge huooo unakuja, mng'oe John Komba
 
hii habari imenishtua sana ckuitegemea, nilitegemea j kujiunga na ccm jinc alivyokaribu na jk
 



  • Wasanii wengi walioko SISIEMU hawako huko kwa matakwa yaoo isipokuwa njaa mangi ndo inawasumbua, wengi wapo akina Vicks Kamatakamata a.k.a shakula ya mzee, akina Keptanini Kombela na wengine wengi.
  • Kamanda Jembe letu karibu kwetu chama la wapambanaji, wapiganaji wa haki za wanyonge waliogandamizwa na sera za watawala wa magamba,
  • Hakika utayanogesha mapambano na nahisi ulichelewa lakini huu ndiyo muda wake
  • Aruta continua......................
  • Mchakamchaka mpaka 2015 mpaka kieleweke hakuna kulala au kusinzia.
 
Mbona unaongea mengi aisee!!!Tatizo nini kijana mwenzetu??Prof J. ni legendary wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, historia inasema hivyo na itaendelea kuwa hivyo! Si busara hata kidogo kumlinganisha gwiji huyu na chipukizi wanaojitokeza sasa. Kazi za sanaa zina generations! Prof J na Sugu sio wa generation hii katika tasnia ya muziki wa Bongo Flavor
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…