3squere
JF-Expert Member
- Aug 2, 2011
- 925
- 181
Msanii aliyekufa 'afufuka' Afrika Kusini
6 Februari 2012 23:23
Mtu mmoja nchini Afrika Kusini anayedai kuwa ni mwanamuziki
mashuhuri aliyekufa, anashikiliwa na mamlaka za nchi hiyo hadi
watakapothibitisha utambulisho wake kwa vipimo vya DNA,
wamesema polisi.
Mtu huyo anasema yeye ni Khulekani "Mgqumeni" Khumalo -
mwanamuziki wa nyimbo za kiasili za Kizulu ambaye alifariki
mwaka 2009.
Anadanganya
Hata hivyo alizuka katika nyumba ya familia yake wiki iliyopita
akidai kuwa alikuwa ametekwa na mizuka.
Familia yake wakiwemo wake zake wawili, wanasema
anaonekana kuwa ndio mwenyewe - lakini polisi wamesema
atashtakiwa kwa udanganyifu iwapo vipimo vya DNA
vitaonesha anadanganya.
Mwandishi wa BBC mjini Johannesburg, Nomsa Maseko
amesema polisi wanatarajia kupata majibu ya vipimo vya DNA
baadaye wiki hii - na mpaka wakati huo mtu huyo atasalia
kizuizini.
Mashabiki
Mwandishi wetu anasema iwapo vipimo vya DNA vitaonesha
kweli ni Bw Khumalo, polisi watalazimika kwenda mahakamani
kupata kibali cha kufukua maiti, ili kujua nani hasa alizikwa,
katika mazishi yaliyokuwa ya hali ya juu ya Bw Khumalo
ambayo yalihudhuriwa na wanasiasa, vyombo vya habari na
mashabiki wake.
Mwandishi wetu anasema kesi hiyo imezua kizazaa nchini
Afrika Kusini - na siku ya Jumapili iliyopita, maelfu ya mashabiki
walikwenda Kwazulu-Natal kushuhudia "kutolewa" rasmi kwa
mtu huyo.
Polisi walitumia maji yenye nguvu kutawanya watu baada ya
msongamano kutokea kutokana na kila mtu kutaka kumuona
mtu anayejiita Bw Khumalo.
Upelelezi
Akitumia kisemeo, aliwaambia mashabiki wake kuwa hakuwa
amekufa - lakini alipotea baada ya kuchukuliwa na wachawi.
Amesema alifungiwa katika pango na mizimu kwa miaka
miwili, na alilazimishwa kuimba na kulazimika kula matope ili
asife kwa njaa.
"Nimekuwa hai muda wote," amekaririwa akisema na gazeti la
The Times la Afrika Kusini.
"Nimepoteza uzito mwingi lakini ni mimi," alisema.
Mtu huyo, ambaye hakuwa na mtindo wa nywele wa rasta
ambao Bw Khumalo alikuwa nao, alipuuza ombi la mashabiki la
kumtaka aimbe, badala yake alitaja majina ya ukoo wake, kwa
mujibu wa gazeti la The Times.
Polisi wa Afrika Kusini wamesema wanashughulikia mkasa huo
kwa kufanya upelelezi wa kesi ya uhalifu.
Alamisha hii
6 Februari 2012 23:23
Mtu mmoja nchini Afrika Kusini anayedai kuwa ni mwanamuziki
mashuhuri aliyekufa, anashikiliwa na mamlaka za nchi hiyo hadi
watakapothibitisha utambulisho wake kwa vipimo vya DNA,
wamesema polisi.
Mtu huyo anasema yeye ni Khulekani "Mgqumeni" Khumalo -
mwanamuziki wa nyimbo za kiasili za Kizulu ambaye alifariki
mwaka 2009.
Anadanganya
Hata hivyo alizuka katika nyumba ya familia yake wiki iliyopita
akidai kuwa alikuwa ametekwa na mizuka.
Familia yake wakiwemo wake zake wawili, wanasema
anaonekana kuwa ndio mwenyewe - lakini polisi wamesema
atashtakiwa kwa udanganyifu iwapo vipimo vya DNA
vitaonesha anadanganya.
Mwandishi wa BBC mjini Johannesburg, Nomsa Maseko
amesema polisi wanatarajia kupata majibu ya vipimo vya DNA
baadaye wiki hii - na mpaka wakati huo mtu huyo atasalia
kizuizini.
Mashabiki
Mwandishi wetu anasema iwapo vipimo vya DNA vitaonesha
kweli ni Bw Khumalo, polisi watalazimika kwenda mahakamani
kupata kibali cha kufukua maiti, ili kujua nani hasa alizikwa,
katika mazishi yaliyokuwa ya hali ya juu ya Bw Khumalo
ambayo yalihudhuriwa na wanasiasa, vyombo vya habari na
mashabiki wake.
Mwandishi wetu anasema kesi hiyo imezua kizazaa nchini
Afrika Kusini - na siku ya Jumapili iliyopita, maelfu ya mashabiki
walikwenda Kwazulu-Natal kushuhudia "kutolewa" rasmi kwa
mtu huyo.
Polisi walitumia maji yenye nguvu kutawanya watu baada ya
msongamano kutokea kutokana na kila mtu kutaka kumuona
mtu anayejiita Bw Khumalo.
Upelelezi
Akitumia kisemeo, aliwaambia mashabiki wake kuwa hakuwa
amekufa - lakini alipotea baada ya kuchukuliwa na wachawi.
Amesema alifungiwa katika pango na mizimu kwa miaka
miwili, na alilazimishwa kuimba na kulazimika kula matope ili
asife kwa njaa.
"Nimekuwa hai muda wote," amekaririwa akisema na gazeti la
The Times la Afrika Kusini.
"Nimepoteza uzito mwingi lakini ni mimi," alisema.
Mtu huyo, ambaye hakuwa na mtindo wa nywele wa rasta
ambao Bw Khumalo alikuwa nao, alipuuza ombi la mashabiki la
kumtaka aimbe, badala yake alitaja majina ya ukoo wake, kwa
mujibu wa gazeti la The Times.
Polisi wa Afrika Kusini wamesema wanashughulikia mkasa huo
kwa kufanya upelelezi wa kesi ya uhalifu.
Alamisha hii