Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Mutungi awalima barua CHADEMA kwa kufanya maandamano Februari 16, 2018

Ningemuona wa maana kama angeandika barua kuhusu kuvifuta vyama vyote vya siasa ibaki CCM tu.

Mtu anatumika halafu anaendelea kujionesha jinsi anavyotumika.
 
Kwa hiyo unamuona msajili wa vyama vya siasa hana role kwenye uchaguzi?!

Ha ha ha...Nguvu ya polisi ni swala muhimu katika kukabiliana na maandamano yasiyo na kibali.

Kumbuka msajili wa vyama alitoa tamko na maelekezo ya vyama kuhakikisha mawakala wana sifa zote siku saba kabla ya uchaguzi...yaani aliwakumbushia kwa nia njema kwani asingetakiwa kufanya hivyo kwa kuwa liko wazi kiutaratibu.

Jingalao naona unatafuta ushindi lakini huna hoja, na unajua kwanini unazidiwa hoja? Wanaccm wengi hamna uwezo wa kujenga hoja kwani mmezoea kutumia jeshi la polisi kuwasaidia kujibu hoja. Matokeo yake mnapoingia kwenye eneo la mijadala huru isiyo na mbeleko ya polisi mnaishia kuchemsha. Sasa imefika siku ya mwisho ya kampeni, kesho yake asubuhi kila wakala anatakiwa awe ameapishwa na hili bado halijafanyika. Msimamizi wa vyama unamjulisha ili akawaapishe hao mawakala? Najua ni mjinga ila sitarajii uwe mjinga ziadi ya hivi. Hilo jeshi la polisi unalisifia kwa kuwa linatumika kama tawi la ccm hivyo lazima uunge mkono kile walichofanya ili kupotosha umma kuhusu mauaji waliyofanya na ukatili wanaowafanyia wapinzani ili ccm iendelee kubaki madarakani kinyume na ridhaa ya umma.
 
Msajili wa vyama vya siasa nchini awaibukia chadema

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amekiandikia barua Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akitaka kijieleza kwa nini asikichukulie hatua kwa kufanya maandamano Februari 16, 2018

Akizungumza na Mwananchi leo Februari 22, 2018, Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema amesema barua hiyo ya msajili waliipokea jana na wanapaswa kuijibu kabla ya Februari 25, 2018.

Jaji Mutungi alipoulizwa kuhusu hilo amesema hawezi kusema lolote kwani yeye anawasiliana moja kwa moja na vyama vya siasa na si vyombo vya habari.

Chadema waliandamana Februari 16 mwaka huu wakishinikiza kupewa viapo vya mawakala wao kabla ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kinondoni.


Chanzo: Mwananchi[/
Jaji Mutungi nakumbuka neno lako ulilonena wakati tupo kwenye lift pale jengo la posta tukielekea kwenye ofisi za tume ya uchaguzi miaka imepita sasa, kwa mantiki ya barua yako kwa chadema naelewa nini kilichomo ndani ya moyo wako sina haja ya kufafanua zaidi.
 
Aliyemtuma hana tatizo na huyo aliyesababisha cdm wakaamua kuandamana maana walikuwa wanatekeleza adhima yake ya kuua upinzani. Huyo aliyemtuma msajlli aiandikie barua anataka kuhakikisha cdm haindelei kufanya siasa hapa nchini na hata ikibidi ifutwe, kwani ni hatari kwa chama chake, na kwa mazingira yalivyo chama chake hakiwezi tena kupambana na cdm kisiasa. Hivyo njia pekee ni hii ya kutumia vyombo vya kimlaka kutekeleza dhamira yake.

Hata wakikifuta ni kujidanganya tu. Kwani tatizo lao kuu ni "upinzani" wanaoupata, na upinzani hauwezi kuisha kwa kufuta chama, kwasababu chama ni mkusanyiko wa watu na sio jina tu. Sasa wafute CHADEMA halafu watu waliojikusanya kwa jina hilo la chama watafute mkusanyiko mwingine mahala pengine, kivingine, na kuendeleza mapambano...
 
Mkuu upinzani madhubuti na makini una sifa gani?
Je upinzani unaopanga mikakati ya kuharibu uchaguzi ndio upinzani madhubuti na makini?

je upinzani unaokiuka kwa makusudi taratibu na sheria zilizoweka ndio upinzani madhubuti na makini?

Je ilikuwa sahihi kwa Chadema kufanya maandamano nje ya muda uliopangwa tena bila kibali?

Unadhani wakati sheria hizi zinawekwa wataalamu walikuwa hawajui tabia chafu kama hizi za Chadema zitatokea?

Boss @ Mimi sio Team Ufipa wala Team Lumumba, Nachoomba Busara na Hekima kutumika. Maswali yako mimi sina majibu yake, Labda wengine wanisaidie kukujibu, Ila kama Chadema walitaka kuharibu Uchaguzi na Kukiuka makusudi taratibu na sheria na kufanya maandamano nje ya muda, kwanini hamkuwachukulia Hatua???
 
Ivi maandamano Tz ni kosa la jinai?? Kwanini zama zile walikubali mfumo wa vyama vingi?
 
Hoja ni kwamba Chadema walipokosa accreditation ya mawakala wao hawakuwa na option yoyote zaidi ya kuvunja sheria?
Je hakukuwa na option ndani ya Sheria wakati na baada ya uchaguzi.??
Wajua sababu ya Civil War ni Watawala Wapumbavu na Waonevu ndio jibu
 
Watu waki za Binadamu, waunde tume ya kufuatilia Wafugwa wote alio wafunga wakati alipokua jaji. Kwani naamini atakua aliwahukumu kimakosa. Jaji gani wa hivi.
 
HUYU JAJI ANAIABISHA TAALUMA YAKE.BORA AACHIE NGAZI KULINDA HESHIMA YAKE.HAIWEZEKANI JAJI ASIJUE KWANN CHADEMA WALIANDAMANA.
 
Acha kupanic mkuu!
Nimekuuliza swali muhimu sana kwa manufaa ya Tanzania...usikurupuke kulijibu ,tulia na utafakari na ukishindwa kujibu kalale halafu ujibu kesho.

CHADEMA inajitanabaisha kuwa ni chama mbadala cha kufanya mema na mazuri nchi zaidi ya CCM.

Chadema inapotaka kuingia kwenye madaraka kwa njia za kihuni na ukiukwaji wa sheria sio jambo sahihi na ni bora mara 10000 kuwa na CCM inayovunja Sheria kuliko kuwapa nchi Chadema halafu wafanye mambo yote unayohisi ni mabaya.

SHeria ya uchaguzi na vyama vya siasa au iwe sheria kwa ujumla wake haikubali maandamano bila kibali au kampeni nje ya muda uliotajwa...viongozi wa Chadema wanavyoamua kwa makusudi kukiuka sheria hata kama ni mbaya inaasharia kuwa CHADEMA inajiaandaa kukiuka Sheria hata pale wananchi watakapoipa fursa.

Nikuulize swali tu je CCM ndio ingeamua kuandamana na Polisi wakawaacha waandamane nje ya muda Chadema ingeona ni sawa tu?

Kwa nini Chadema ikiuke sheria ili kubadilisha mambo?

Chadema inalo la kuamua...kama wanaamua kuwa wavunja sheria au waasi basi ijulikane hivyo na wafanyiwe ubaya kama waasi na kama imeamua kuwa ni wafuata demokrasia hawatakiwi hata chembe kukiuka misingi ya demokrasia.
Mbona Maandamano ya CUF waliyoyafanya baada ya muda wa kampeni tena bila kibari hayakuwa tatizo???? CDM wamekuwa na utaratibu wa kusindikiza wagombea wao tangu siku ya kwanza ya kampeni na haikuwahi kuwa tatizo kwa yeyote.

Msajiri asiwalime CCM waliobeba box la kura na kukimbia nalo na baadae kulirudisha, aje kuwaandikia barua CDM at maandamano??? Hizi ni hila za kijinga haziwezi kuiogopesha CDM. Akitaka amrete Barozi asiye na ubarozi maalumu akafanye yale ya Lipumbavi
FUTA LICHAMA LA WAHUNI


Sent from my M40 using JamiiForums mobile app
 
Binafsi nimefurahishwa sana na hii barua ya msajili wa vyama vya siasa kwa hichi chama cha wahuni kinachoongozwa na muhuni namba moja "Mbowe". Tena hii ni hatua ya kwanza kwenda kukifungia hichi chama cha "kihuni" ambacho kimedhamiria kumwaga damu ya Watanzania ili tu kipate nafasi ya kutawala nchi hii. Hotuba zote alizozitoa Mbowe siku ile ya maandamano ya kihuni zimerekodiwa na ushahidi wa video upo na kila kitu alichoongea kimehifadhiwa.

Safari hii CHADEMA hawana ujanja maana ni lazima wafutwe tu. Hakika nitafurahi sana siku hiyo ikifika.


msajili.PNG
 
Hoja ni kwamba Chadema walipokosa accreditation ya mawakala wao hawakuwa na option yoyote zaidi ya kuvunja sheria?
Je hakukuwa na option ndani ya Sheria wakati na baada ya uchaguzi.??
Itaje iyo option unayo dhani ingekuwa nzr kwao kuchukua kwa wakati huo, ili ujibiwe vzr.
 
hili ni jambo zuri; lakini asiishe hapo vile vile aandike barua kuulizia kwanini mawakala wa CHADEMA hawakupatiwa hati zao hadi dakika za majeruhi. Haya mambo mengine yanaudhi tu. Maana inalazimisha kuhoji kama CDM wasingefanya maandamano (ambayo kwa kweli yalikuwa nje ya muda na sidhani kama yalikuwa na kibali) na yule binti asingeuawa, kweli CDM wangepata lini accreditation ya mawakala wao?
Nia ya viongozi wa chadema walokuwepo mkutanoni mbowe included; ... ktk suala la kudai hizo hati ilikuwa njema kabisa ... tatizo ni pale ALIPOTOA KAULI ZA KUCHOCHEA wanachama wa CDM na ksha kwa pamoja kuingia barabarani ....

SWALI FIKIRISHI: ... Kwani wangefikia MAAZIMIO pale pale mkutanoni kuwa WABUNGE/VIONGOZI walokuwepo pale mkutanoni wakiongozwa na Mw/kiti waende kwa mkurugenzi kumuuliza juu ya hizo hati ingeshindikana? maana si ajabu wangetumia tu magari yao tena machache .... PASINGEKUWEPO MAANDAMANO
 
Akili za matope eti huyu naye ni professor.

Umewajima watu mia sita barua za uwakala sasa wakija kukudai barua utaita maandamano.
Eti hivi watu wakitoka kwenye mechi ya mpira wa yanga na simba utasema wanaandama kisa wamekuwa wengi
Ingekuwa amenyimwa barua mmoja halafu wakaenda nyomi hapo tena kidogo sawa kusema wameandamana japo mimi ningesema wamemsindikiza tu mshikaji
 
Aandike ya kwake Kwanzaa ya kujiuzulu na apewe kifungo jela kwa kusababisha watu waandamane. Kwa sababu ya kutokutoa barua za mawakala kwa wakati.
 
Back
Top Bottom