Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,498
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imetoa muda wa wiki moja kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kiwe kimewasilisha maelezo kuhusu malalamiko ya mjumbe wa Baraza Kuu wa chama hicho, Lembrus Mchome.
Mchome aliwasilisha malalamiko kwa msajili wa vyama akilalamikia kikao cha Baraza Kuu Taifa kilichofanyika Januari 22, 2025 kwamba kilikuwa batili kwa sababu hakikutimiza masharti ya Katiba ili kuwa kikao halali.
Soma, Pia: Team Mbowe wajidhatiti kumkwamisha LISSU, wapinga uteuzi wa Wajumbe watano wa kamati kuu aloufanya Lissu, waandika Barua kwa msajili wa Vyama
Pia, Mchome alidai kikao hicho ndani ya ukumbi walikuwepo wanachama ambao siyo wajumbe na baadhi ya watu hao walipiga kura kinyume na matakwa ya katiba ya chama hicho.
Barua iliyosainiwa na Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza imekitaka Chadema kujibu barua ya Mchome kwa muda usiozidi Machi 31, 2025.
Soma:
Chanzo: Mwananchi
Soma, Pia: Team Mbowe wajidhatiti kumkwamisha LISSU, wapinga uteuzi wa Wajumbe watano wa kamati kuu aloufanya Lissu, waandika Barua kwa msajili wa Vyama
Pia, Mchome alidai kikao hicho ndani ya ukumbi walikuwepo wanachama ambao siyo wajumbe na baadhi ya watu hao walipiga kura kinyume na matakwa ya katiba ya chama hicho.
Soma:
Chanzo: Mwananchi