msaada wapendwa

msaada wapendwa

I love ur sense of humor lara 1, unatoa bonge la point lkn kimujini mujini. You be blessed kwa msaada unautoa, l am sure ukimfanyia mtu Councilling hata kama ana mlima wa matatizo yaani unakuwa kama mlima wa manyoya vile.

I can't help not to fall in love with you gal.
 
Last edited by a moderator:
nionyeshe jiji basi na mimi dear

Hahaaaa! Jiji baya hili weweee! Si unaona mwenzio hapo keshashibishwa maharage ya mbeya?!!!! Tusichakachue hii thread kuna uhai wa kichanga kisicho na hatia upo hatarini. Acha apate msaada.
 
I love ur sense of humor lara 1, unatoa bonge la point lkn kimujini mujini. You be blessed kwa msaada unautoa, l am sure ukimfanyia mtu Councilling hata kama ana mlima wa matatizo yaani unakuwa kama mlima wa manyoya vile.

I can't help not to fall in love with you gal.
ahahaaa umeona sis eeeh!
 
Hahaaaa! Jiji baya hili weweee! Si unaona mwenzio hapo keshashibishwa maharage ya mbeya?!!!! Tusichakachue hii thread kuna uhai wa kichanga kisicho na hatia upo hatarini. Acha apate msaada.
msaidie bwana apate iyo ada ya mwaka wa tatu malizana nae pm huko! wanaume hawa tutajibebaje jamani?
 
Mwanaume kafanyaje? Ndo kabeba mimba? Yaani kulipiwa ada ya mwaka mmoja tu kampa yoote hadi kikakatikia! Angelipiwa mahari?
Wanawake wasio na akili huwa wananochosha!
lakini ana tatizo jamani ...wanaume hawa ?
 
ahahaaa umeona sis eeeh!

Yaani nimempenda ghafla, mleta mada muendee PM lara ikiwezekana muache achat na huyo shosti wako kupitia ID yako; l am sure tatizo litakuwa limesolvika kwa 75% inayobaki ni utekelezaji tu!
 
Maskini kachezea shiling chooni dah mpe pole 2 asitoe hyo mimba kabisa
 
Mi simlaumu huyo dada kwani hatuwezi kujua huyo mwanaume alimdanganya nini!! Jaman hawa wanaume waongo ohooooo...
Si ajabu mwanzo wa relationship yao alimdanganya atamuoa, na huenda binti hakujua kama jamaa ana mchumba, na huenda alimwambia endapo akibeba mimba atampa huduma zote...! Yawezekana ndio maana binti akawa hana wasiwasi...!

Mwambie tuu afate ushauri wa Lara 1, asithubutu kutoa hiyo mimba...
 
Huu uzi mbona wanaume tumeugwaya?..au unachoma?
By the way mdogo wangu lara 1 hongera kwa ushauri!
Ila wakati mwingine na nyie wadada kuweni macho..sio kila tunda linaliwa ati..mengine sumu!!
 
duuh kwanza asitoe mimba
wanaume jamani?mbona wanyama hivi?
amebakiza muda gani kumaliza chuo? kwao wakijipigapiga iyo hela haitoki kabisa?
tusilaumu yeyeto maana bado kiini cha tatizo hakijajulikana. huyo mwanamume hata akubali kumlipia kulikuwa na sababu na kumwacha kuna sababu pia lkn hatuijui. namshauri aende kwa mshauri wa wa wanafunzi kwanza ajieleze kinaganaga naamini atapata ufumbuzi. mpe pole zake.
 
Lara1 unastahili pongezi
Kijana ukifika mjini lazima uonane na watu kama sisi, kama utakumbuka maneno haya alisema Marehemu Remmy Ongala, yalikuwa na maana sana
Mimi sishauri kutowa mimba kwanza aende alikoelekezwa na Lara1 baadae arudi hapa tuone vipi amesaidiwa na kama anahitaji msaada zaidi
huo ni ushauri wangu
 
Kimsingi me kama Mwanaume mwenye huruma imenipain sana, kwani simlaumu mtoto wa watu kwani haikuwa dhamira yake ni maisha tu ndiyo yamemfanya awe hivyo, me binafsi natamani kujua ada ni shilingi ngapi? na inalipwa kwa installment ngapi na ni lini inatakiwa? Me binafsi natamani tumsaidie amalize shule na mimba asitoe itakuja kumuathiri kisaikolojia.....kama kila mmoja akimsaidia kiasi fulani atasoma na atamaliza na tutakuwa tumefungua ndoto zake, please tusimzimie ndoto zake.....UKITOA UNAPATA ZAIDI
 
Weweeeee ATAHARIBU ISHU!!!! MIMBA NDO DILI LENYEWE HILO!!!! Ukiwaa maskini, UTASAIDIWA KIDOGO, ukiwa MASKINI MWENYE MIMBA ISIO NA BABA, BAAAAAS! USHASAIDIWA!!!!! Huko kote bila mimba HAPATI KITU. Sababu kubwa ya kusaidiwa huko ni ili ASIJIUZE NA MIMBA!!! Sasa kama hana mimba basi ajiuze apate ada!! Acheni kabisa habari ya kutoa mimbaaa, KILA MTOTO ANAKUJA NA RIZIKI YAKE!!!! Bila mimba kumpata, ungekuja kuandika humu, ukanikiuta LARA 1 nikakuelekeza wanakosaidia mabinti wasio na uwezo??? RIZIKI YA MIMBA HIII.

mimi love yu,again!
 
I love ur sense of humor lara 1, unatoa bonge la point lkn kimujini mujini. You be blessed kwa msaada unautoa, l am sure ukimfanyia mtu Councilling hata kama ana mlima wa matatizo yaani unakuwa kama mlima wa manyoya vile.

I can't help not to fall in love with you gal.
mi nishampa manyota siku nyingi!i really love this gal,she love herself na anaamini katika mawazo yake!

huyo binti aliyepata tatizo aitoe hyo mimba,NEVER!aende huko anakoelekezwa na lara 1 atasaidiwa.kwanza lara 1 ampeleke kabisa!
 
Last edited by a moderator:
Jamani tuache story, kama ni kweli huyu mtu anahitaji msaada wa ushauri ili kumweka katika hali nzuri kisaikolojia kwanza, ili aone kuwa na mimba ni changamoto tuu za maisha, na bado atafaulu masomo yake. Mimi nimesoma chuo na ninafahamu mifano mingi ya watu wa aina hiyo na wakishauriwa vizuri atatoka fresh tuu.

Jambo la pili ni msaada wa kifedha (ada). Mleta mada hajaweka hoja vizuri, kwani anapata % ngapi ya HESLB? na yeye atahitaji kutoa ngapi? Alafu watu wa karibu (marafiki, ndugu, wanaotoka naye sehemu moja, wilaya au mkoa, wanaosali naye, class mates wake, etc) wameshindwa kabisa kutoa suluhu ya tatizo hilo? Katika hali ya kawaida siamini katika hilo.

Naomba mtoa mada aweke wazi huyo dada yuko chuo gani, alafu wadau tutatoa ushauri afuate steps zipi ili kumsaidia. Mimi niko chuo kikuu kimoja (sitakitaja) lakini ninaweza kutoa ushauri nini kifanyike katika mazingira hayo. Nasema hivyo kwa sababu kuna ofisi ya dean of student ambayo kazi yake moja kubwa ni kumshauri mwanafunzi katika matatizo, pia kuna academic adviser ambaye ni Lecturer, ambaye pia anamshauri mwanafunzi katika matatizo ya kitaaluma. Pia Kuna social groups kwa mfano wanaotoka mkoa fulani wanakuwa na assocition yao kwa ajili ya kusaidiana mambo kadha wa kadha. Pia kuna vikundi vya dini, anaweza kupata ushauri na kuombewa pia kumtia moyo na kumwomba Mungu afungue njia kwa ajili yake. Mwisho wa siku solution itapatikana tuu hata kama ni kuchangishana vijisenti kidogo miongoni mwa hivyo vikundi na wasamaria mwema na ada itapatikana.

Kama kweli uko serious, naomba mleta mada ni PM kwa mawasiliano zaidi.
 
rafiki zangu nashukuru kwa msaada wenu rafiki angu kwa sasa kaona asitoe mimba na anafuatilia ada anajaribu kuongea na uongozi wa chuo aone itakuwaje
 
kiukweli yeye anakazania kwanza atoe mimba maana hajuiafanyaje mwanaume kaama na mkoa kiukweli kachanganyikiwa kikubwa ni ushauri kwao anashindwa kurudi na mimba nipo nae ninapokaa

Jamani si nimesema naitaka mimi, nenda PM bana!!
 
Asijaribu kutoa mimba, kwani itamtesa sana ktika maisha yake, na atajikuta anaishi kwa majuto, Hayo ni mapito Mungu mwenyezi atamjalia na atamaliza chuo ingawa yaonekana ngumu kwasababu ya kutokua na ada, lakini jibu lipo yahitaji awe na moyo wa subira na uvumilivu.
 
asanteni kwa mawazo uyu msichana nadhani anaitaji psychologist coz yupo confused jana kanambia yuko tayari kutafuta yoyote amuoe kiukweli mi nashindwa sasa
 
Back
Top Bottom