Msaada wa VISA ya Afrika Kusini

Msaada wa VISA ya Afrika Kusini

Siyo permanent residents permit ni temporary residents permit ambayo kwa jina lingine ni Visa huwa inaanzia miaka miwili na kuendelea.
Nadhani unaongelea residence permit itakayokuruhusu kuishi na kufanya kazi kwa muda wote.

Idara ya uhamiaji ya SA ndiyo wanatoa hiyo kitu ukiwa huko. Jaribu kutafuta tovuti rasmi yao utapata maelezo kamili.

Ikiwa unahitaji kukaa kwa muda usiozidi miezi mitatau yaani kutembea tu bila kufanya kazi mtanzania huhitaji visa.

Ikiwa ndiyo hivyo huhitaji kufanya kazi lakini unataka kukaa muda zaidi ya miezi mitatu basi siku mbili kabla miezi mitatu haijaisha vuka mpaka nchi jirani kisha rejea. Waweza fanya mara nyingi kila miezi mitatu inapokaribia kuisha.
 
Mtu ana smartphone afu anauliza maswali ya kipuuzi
 
Nijuavyo hiyo Visa unaombea ukiwa nje ya SA au nchi jirani sasa kama umeambiwa inawezekana kuomba ukiwa ndani basi ni vema ukajongea ofisi za Uhamiaji ili wakupe muongozo.
 
Nijuavyo hiyo Visa unaombea ukiwa nje ya SA au nchi jirani sasa kama umeambiwa inawezekana kuomba ukiwa ndani basi ni vema ukajongea ofisi za Uhamiaji ili wakupe muongozo.
Hawana mpango wakusaidia matatizo yako Yani uhamiaji ya huku wahahusiki na kutoa visa ni VFS mziki upo ndugu.
 
Nilijaribu kuwapigia simu waliniambia hawausiki na visa za SA sasa sijui kwa uzoefu wako mkuu kuwa uwakika wa kunisadia upo pale ubalozini ni vioja.
Sasa mkuu si uende ofisi za uhamiaji huko Afrika Kusini ukaulizie au hauishi kihalali unaogopa watakudaka? Fungua hata online usome utaratibu wa kuomba viza huko upoje
 
Sasa mkuu si uende ofisi za uhamiaji huko Afrika Kusini ukaulizie au hauishi kihalali unaogopa watakudaka? Fungua hata online usome utaratibu wa kuomba viza huko upoje
Yaani hata mimi namshangaa halafu analazimisha watu wa Jf ndio wamsaidie sasa sijui anataka msaada gani huyu mwenzetu,

Infomation ipo kiganjani mwake lakini anataka watu wengine waumize kichwa kwa shida zake.
 
Yaani hata mimi namshangaa halafu analazimisha watu wa Jf ndio wamsaidie sasa sijui anataka msaada gani huyu mwenzetu,

Infomation ipo kiganjani mwake lakini anataka watu wengine waumize kichwa kwa shida zake.
Nashangaa miaka 58 ya uhuru na yupo huko SA hajui hilo hadi aambiwe na mimi niliopo Nyarugusu...
 
Nashangaa miaka 58 ya uhuru na yupo huko SA hajui hilo hadi aambiwe na mimi niliopo Nyarugusu...
Itakua hayupo kihalali maana hata story yake ya UNHCR nikajua tu yupo kwenye mazingira gani.
 
Nadhani unaongelea residence permit itakayokuruhusu kuishi na kufanya kazi kwa muda wote.

Idara ya uhamiaji ya SA ndiyo wanatoa hiyo kitu ukiwa huko. Jaribu kutafuta tovuti rasmi yao utapata maelezo kamili.

Ikiwa unahitaji kukaa kwa muda usiozidi miezi mitatau yaani kutembea tu bila kufanya kazi mtanzania huhitaji visa.

Ikiwa ndiyo hivyo huhitaji kufanya kazi lakini unataka kukaa muda zaidi ya miezi mitatu basi siku mbili kabla miezi mitatu haijaisha vuka mpaka nchi jirani kisha rejea. Waweza fanya mara nyingi kila miezi mitatu inapokaribia kuisha.
Hapo.mwisho umempa teknik nzuri
 
Wana jamvi habari zenu.

Nipo South Africa nina uhitaji wa Visa ya Masomo au ya kazi. Kwa sasa nipo Capetown nina taarifa zisizo kamili kuwa, kuna uwezekano wa kupata Visa bila ya kurudi Bongo upo.

Kati ya taarifa hizo kuwa Oliver Tambo ninao uwezo wa kuipata.

Msaada kwa wenye uzoefu wa Africa Kusini. Asanteni.
Kuingia SA huhitaji visa. Unakwenda mpakani (au airport) utapata visa hapo hapo ya mwezi mmoja mpaka mitatu, kufuatana na maelezo yako kwa nini unataka kuingia SA. Lakini kwa kusoma lazima uombe ukiwa nje ya SA uambatanishe barua ya chuo kilichokukubali ukasome huko. Vivyo hivyo na kufanya kazi. Unaambatanisha barua ya offer ya kazi. Maombi yote hayo yanachukua mpaka miezi mitatu. Vyuo vinapewa quota ya wanafunzi wageni (haizidi 5%). Ni pale tu chuo kikidhihirisha hakuna mwananchi mwingine aliyeomba kusoma hapo chuoni ndipo wanaweza wakazidisha hiyo quota. Waajiri pia lazima wathibitishe walitangaza kazi hiyo na hakuna raia aliyepatikana kuijaza nafasi waliyoku-offer wewe. Ubalozi wetu hawawezi kukusaidia cho chote kupata visa au study/work permit ya kuingia SA. Wao wanashughulikia wa-SA wanaotaka kuja TZ. Kwa kusoma na kufanya kazi kuna pia fomu ambazo daktari anahitaji kukujazia kuthibitisha huna magonjwa kadhaa yaliyoainishwa. Mbali na hayo kwa kusoma ukikubaliwa utahitaji kuweka dhamana ya Sh. kadhaa (inaweza kufika milioni moja) kwenye ubalozi wao kama dhamana kwamba ukimaliza masomo utatoka nchini kwao. Fedha hizo utazikuta nyumbani kwenye ubalozi wa SA baada ya kutoka nchini kwao. Nina uzoefu wa haya ninayoyasema ingawa uzoefu wangu ni wa zaidi ya miaka 10 iliyopita. Kwa hiyo dhamana inaweza ikawa zaidi ya hiyo milioni.
 
Ubalozi wa Tanzania hauwezi kukusaidia chochote kwenye Visa ya Nchi nyingine......

Zipo nchi ambazo zinaruhusu ku apply Visa ndani ya Nchi but kwa Visa Ndogo... But kwa Resident Visa au Permanent Visa inabidi utoke nje ndo u apply!

Nakushauri.... Nenda kwenye office za Immigration za SA hapo Cape Town.... Nenda kawaeleze nia yako watakupa utaratibu mzuri wa kufata.
 
Baadhi hamjamuelewa mleta uzi, Yes hauhitaji visa kuingia nchi za umoja wa SADC ,SA ikiwa moja wapo ila hii inafanya kazi ndani ya miezi mitatu tu ( 90 days) baada ya hapo unahitaji kibali maalumu, kama unafanya kazi basi utatakiwa upate work permits, au kama unasoma basi lazima upate visa ya uanafunzi. n.k

Kwa maelezo haya ebu tusubiri wajuvi zaidi wafike kutuelezea jinsi ya kufanikisha hilo.
 
Baadhi hamjamuelewa mleta uzi, Yes hauhitaji visa kuingia nchi za umoja wa SADC ,SA ikiwa moja wapo ila hii inafanya kazi ndani ya miezi mitatu tu ( 90 days) baada ya hapo unahitaji kibali maalumu, kama unafanya kazi basi utatakiwa upate work permits, au kama unasoma basi lazima upate visa ya uanafunzi. n.k

Kwa maelezo haya ebu tusubiri wajuvi zaidi wafike kutuelezea jinsi ya kufanikisha hilo.
Karibuni kutoa mchango ni kipi cha kufanya
 
Back
Top Bottom