Msaada wa tatizo la mtoto wa jicho

Msaada wa tatizo la mtoto wa jicho

Kendrick Rama

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2019
Posts
409
Reaction score
458
Habari zenu wakuu,

Naomba mwenye uelewa au mtaalamu wa mambo ya magonjwa ya macho anisaidie hili.

Hapo juzi kati niligundua kuna kauvimbe kadogo ndani ya macho yangu ambacho hakana maumivu yoyote, ila baada ya kuchunguza kwa umakini na kuulizia baadhi ya watu walinambia kuwa huyo ni mtoto wa jicho na ndio kwanza anaanza, wengi wamenielekeza dawa mbalimbali za asili ila hadi sasa hakuna niliyotumia kwani siwezi kujaribu kila dawa kwenye macho yangu kwani ni kiungo muhimu.

Naomba kama kuna mwenye uwezo wa kunisaidia haya:
- Kujua chanzo chake kikuu ni nini?
- Kujua kama hapa naweza kuwahi tiba na kama nikichelewa Madhara yake ni nini?
- Kujua kama kuna uwezekano wa kupona?
- Madhara yake kwa ujumla?
 
Mkuu nina tatzo kama lako,ngoja nisubiri ushauri nisinzishe uzi mwingne.But Kwangu mimi naomba kujua kama kuna dawa mbadala out of surgery.Nimewahi kufika hospital nikaambiwa nifanyiwe upasuaji kiukweli niliogopa.
 
Mtoto wa jicho (Cataracts) kwa ninavyojua mimi, zipo za aina mbili.

Ya kwanza husababishwa na mionzi ya jua ambayo huathiri moja kwa moja protein zilizokuwepo machoni.

Ya pili, hutokana na mlundikano wa sukari kwenye lenzi za macho ambapo mara nyingi hutokea kwa watu wenye kisukari au watu wazima (wazee).

Inakuwa kama unafanya ukungu mweupe kwenye jicho au macho.

Njia ya kutibu hili tatizo mara nyingi huwa ni upasuaji mdogo (minor surgery).

Kama usipofanya hivyo, kuna uwezekano wa kupungua uwezekano wa kuona taratibu na mwisho upofu kabisa.

Hata hivyo unaweza kuwa nao kwa muda mrefu bila ya madhara yoyote kama utakuwa hausumbui maana kuna baadhi ya watu mtaani wapo na mtoto wa jicho lakini wanaishi nao kwa muda sasa.

Ila cha muhimu zaidi ni kufika hospitali. Usiidharau hiyo hali hata kidogo.
 
MalcolM XII,
shukrani mkuu,

Ila kwangu mimi ndio kwanza anaanza hivi hakuna njia mbadala kama dawa za kuzuia kwa sababu bado mdogo sana, na vipi kuhusu hiyo surgery haina madhara yoyote na ikitokea nimefanya ubora wa macho utakuwa vilevile au kuna vitu vitapungua kidogo?
 
Mkuu nina tatzo kama lako,ngoja nisubiri ushauri nisinzishe uzi mwingne.But Kwangu mimi naomba kujua kama kuna dawa mbadala out of surgery.Nimewahi kufika hospital nikaambiwa nifanyiwe upasuaji kiukweli niliogopa.
ngoja waje mkuu, ila kuhusu upasuaji hata mimi nina hofu sana
 
Mkuu nina tatzo kama lako,ngoja nisubiri ushauri nisinzishe uzi mwingne.But Kwangu mimi naomba kujua kama kuna dawa mbadala out of surgery.Nimewahi kufika hospital nikaambiwa nifanyiwe upasuaji kiukweli niliogopa.
Aisee kuna mdogo wangu tunashiriki baba mmoja alipata tatizo la mtoto wa jicho tena ilikuwa inakuwa kwa kasi sana.
Karibu sehemu nyeusi yote iingie ile rangi nyeupe ya ukungu.

Kuna ndugu yake kwa mama yake alimpa dawa ya asili ya majani unakamulia maji yake jichoni, siku ya pili tu mtoto wa jicho alianza kupotea. baada ya siku 4 alifutika kabisa bila kuacha alama.

Sijui kama huyo alietoa dawa yupo hai, lakini mtu alie enda kuchukua dawa ameshafariki.
Nashauri nendeni CCBRT kwanza kabla ya kutumia madawa ya tiba mbadala.
 
MalcolM XII,
shukrani mkuu,

Ila kwangu mimi ndio kwanza anaanza hivi hakuna njia mbadala kama dawa za kuzuia kwa sababu bado mdogo sana, na vipi kuhusu hiyo surgery haina madhara yoyote na ikitokea nimefanya ubora wa macho utakuwa vilevile au kuna vitu vitapungua kidogo?
Wanapofanya Operation wanakuwa wanabadili lenzi iliyoharibika na kuweka nyingine ya bandia.

Kabla ya kufanya uamuzi, daktari lazima akuambie consequence zake.

Kwa kawaida, hutokea upungufu wa muono wa macho au jicho ukilinganisha na hapo mwanzo. Japokuwa ni kwa kiwango kidogo sana. Ila hivyo ni bora zaidi kuliko kubaki nao.

Kumbuka maneno ya waswahili, USIPOZIBA UFA, UTAJENGA UKUTA.
 
Aisee kuna mdogo wangu tunashiriki baba mmoja alipata tatizo la mtoto wa jicho tena ilikuwa inakuwa kwa kasi sana.
Karibu sehemu nyeusi yote iingie ile rangi nyeupe ya ukungu.

Kuna ndugu yake kwa mama yake alimpa dawa ya asili ya majani unakamulia maji yake jichoni, siku ya pili tu mtoto wa jicho alianza kupotea. baada ya siku 4 alifutika kabisa bila kuacha alama.

Sijui kama huyo alietoa dawa yupo hai, lakini mtu alie enda kuchukua dawa ameshafariki.
Nashauri nendeni CCBRT kwanza kabla ya kutumia madawa ya tiba mbadala.


Duuh mkuu nisaidie kuulizia hyo dawa inawezekana alifariki na alimwachia mtu dawa.CCBRT nishaenda option waliyotoa ni surgery.
 
Mkuu nina tatzo kama lako,ngoja nisubiri ushauri nisinzishe uzi mwingne.But Kwangu mimi naomba kujua kama kuna dawa mbadala out of surgery.Nimewahi kufika hospital nikaambiwa nifanyiwe upasuaji kiukweli niliogopa.
Hapana hamna mbadala

Sent using .... who cares anyway
 
Habari zenu wakuu,

Naomba mwenye uelewa au mtaalamu wa mambo ya magonjwa ya macho anisaidie hili.

Hapo juzi kati niligundua kuna kauvimbe kadogo ndani ya macho yangu ambacho hakana maumivu yoyote, ila baada ya kuchunguza kwa umakini na kuulizia baadhi ya watu walinambia kuwa huyo ni mtoto wa jicho na ndio kwanza anaanza, wengi wamenielekeza dawa mbalimbali za asili ila hadi sasa hakuna niliyotumia kwani siwezi kujaribu kila dawa kwenye macho yangu kwani ni kiungo muhimu.

Naomba kama kuna mwenye uwezo wa kunisaidia haya:
- Kujua chanzo chake kikuu ni nini?
- Kujua kama hapa naweza kuwahi tiba na kama nikichelewa Madhara yake ni nini?
- Kujua kama kuna uwezekano wa kupona?
- Madhara yake kwa ujumla?
Usipoteze muda MgumuNgara wahi CCBRT haraka sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee kuna mdogo wangu tunashiriki baba mmoja alipata tatizo la mtoto wa jicho tena ilikuwa inakuwa kwa kasi sana.
Karibu sehemu nyeusi yote iingie ile rangi nyeupe ya ukungu.

Kuna ndugu yake kwa mama yake alimpa dawa ya asili ya majani unakamulia maji yake jichoni, siku ya pili tu mtoto wa jicho alianza kupotea. baada ya siku 4 alifutika kabisa bila kuacha alama.

Sijui kama huyo alietoa dawa yupo hai, lakini mtu alie enda kuchukua dawa ameshafariki.
Nashauri nendeni CCBRT kwanza kabla ya kutumia madawa ya tiba mbadala.
shukrani ndugu
 
Wanapofanya Operation wanakuwa wanabadili lenzi iliyoharibika na kuweka nyingine ya bandia.

Kabla ya kufanya uamuzi, daktari lazima akuambie consequence zake.

Kwa kawaida, hutokea upungufu wa muono wa macho au jicho ukilinganisha na hapo mwanzo. Japokuwa ni kwa kiwango kidogo sana. Ila hivyo ni bora zaidi kuliko kubaki nao.

Kumbuka maneno ya waswahili, USIPOZIBA UFA, UTAJENGA UKUTA.
sawa mkuu itabidi niwahi kabla tatizo halijawa kubwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom