Habari za leo natumai wote ni wazima, poleni na majukumu. Jaman ndugu zangu yamenifika hapa na hii ni baada ya kuwa na mahusiano na mfanyakazi mwenzangu ambae tupo wote pamoja katika taasisi fulani.
Ipo hivi huyu mwanaume tulipoonana Kwa mara ya Kwanza kila mtu alimpenda mwenzake lakini sikufanya papara ya kuanzisha mahusiano kwani nilisubiri aanze kuonesha interest yeye, kwa kuwa yeye ni mwanaume kwani niliamini nikianza kumtongoza Mimi itanigharimu
Basi haikuchukua muda mrefu kwani mapenzi hayajifichi baina ya watu ilibidi aniambie kuwa ananipenda hivyo nikajikuta nimeingia kwenye mahusiano naye huku tukipeana ahadi ya kuja kufunga ndoa.
Tatizo linaanza hapa, huyu mwanaume ameshajifahamu kuwa yeye ni mzuri na wanawake wengi wanamtaka na kumtamani na hata kabla sijawa naye kuna wanawake walikua wakimtaka kimapenzi lakin aliwapotezea
Sasa kama mwezi mmoja umepita nimegundua kuwa kuna mwanamke anampa maneno huyu mpenzi wangu kunihusu Mimi ili tugombane kwani hapo mwanzo alishamtongoza jamaa Na jamaa akachomoa
Ila sasa kama wiki mbili nyuma tulikwaruzana na huyu mwanaume ghafla nikaona kaanza kuwa na ukaribu na huyo mwanamke na ukizingatia wote tupo sehemu moja ya kazi na watu wanafahamu uhusiano wetu ko ikabidi nimuulize mpenzi wangu kulikoni naona kawa mkali na hataki kunipa ushirikiano
Kwenu JamiiForum najua humu kuna watu wazima na wengine wengi ambao wamepata changamoto mbalimbali naombeni mnipe ushauri nifanyaje ili ninusuru hili penzi na kama nitashindwa kunusuru penzi basi walau mnipe msaada wa mbinu za kutumia ili nimuachie huyo mwanamke awe na huyo mwanaume pasipo mimi kuumia kwani tupo mazingira ya kazi na muda mwingi tunaonana na mwanamke kaanza kunifanyia visa.
Ipo hivi huyu mwanaume tulipoonana Kwa mara ya Kwanza kila mtu alimpenda mwenzake lakini sikufanya papara ya kuanzisha mahusiano kwani nilisubiri aanze kuonesha interest yeye, kwa kuwa yeye ni mwanaume kwani niliamini nikianza kumtongoza Mimi itanigharimu
Basi haikuchukua muda mrefu kwani mapenzi hayajifichi baina ya watu ilibidi aniambie kuwa ananipenda hivyo nikajikuta nimeingia kwenye mahusiano naye huku tukipeana ahadi ya kuja kufunga ndoa.
Tatizo linaanza hapa, huyu mwanaume ameshajifahamu kuwa yeye ni mzuri na wanawake wengi wanamtaka na kumtamani na hata kabla sijawa naye kuna wanawake walikua wakimtaka kimapenzi lakin aliwapotezea
Sasa kama mwezi mmoja umepita nimegundua kuwa kuna mwanamke anampa maneno huyu mpenzi wangu kunihusu Mimi ili tugombane kwani hapo mwanzo alishamtongoza jamaa Na jamaa akachomoa
Ila sasa kama wiki mbili nyuma tulikwaruzana na huyu mwanaume ghafla nikaona kaanza kuwa na ukaribu na huyo mwanamke na ukizingatia wote tupo sehemu moja ya kazi na watu wanafahamu uhusiano wetu ko ikabidi nimuulize mpenzi wangu kulikoni naona kawa mkali na hataki kunipa ushirikiano
Kwenu JamiiForum najua humu kuna watu wazima na wengine wengi ambao wamepata changamoto mbalimbali naombeni mnipe ushauri nifanyaje ili ninusuru hili penzi na kama nitashindwa kunusuru penzi basi walau mnipe msaada wa mbinu za kutumia ili nimuachie huyo mwanamke awe na huyo mwanaume pasipo mimi kuumia kwani tupo mazingira ya kazi na muda mwingi tunaonana na mwanamke kaanza kunifanyia visa.