Msaada wa kuweza kupata mtoto

Msaada wa kuweza kupata mtoto

pole sana kaka inawezekana mara nyingi uapofanya mapenzi, shahawa huwa hiziki sehemu husika kulingana staili unayotumia.. ili yai lilutubishwe linahitaji mbegu wastani wa kijiko cha chakula ambacho huwa na wastani wa mbegu 1000000.
 
mungu awatangulie na awatimizie haja ya mioyo yenu.

Lakini.....

Mumejiandaa kulea mwanaaaaaa?...au mnataka mtoto kesho muanze kugombana..karo ya nursery school, matibabu mavazi, shule za academy, vyuo vikuu vya malysia na india etc...mumeyaona haya wakuu au ndio mnataka kutengeneza watoto wanaofuta vioo vya magari kwenye traffic lights.

Tafakarini kisha muchukuwe hatua na mungu awaongoze kwenye tafakuri zenu.

Tunakushukuru kwa ushauri wako kaka, lakini suala sio kujisifia, ila tuna uwezo mzuri sana mimi na mwenzangu, wote ni wafanyakazi tunalipwa vzr under pensionable and permanent conditions.
Hapa tulipo kaka tuna familia kubwa kama watu 6 na wengine tunawasomesha lkn hatuna mtoto, ila sio haraka sana. Mungu ndio muweza wa vyote.
 
Nawashukuru sana wanajamvi, tumetoka hosp. tunamshukuru Mungu tumepewa majibu lkn sio complete, mengine mpaka next week, lakini tumepata mwanga na matumaini makubwa sana. Nadhani wiki ijayo mambo yataenda sana. Nawashukuru sana.
Nakushukuru sana “king kong III” kwa kunipa ujasiri mkubwa sana.
Lakini yote namshukuru Mungu coz yote ndio anayaweza yeye. M`barikiwe sana
 
Yaani mwaka 1 unalalamika nina dada mmja alikaa 12yrs bila mtoto na mwaka huu january 2013 kapata mtoto
 
Mkuu,

Nilishawahi kutoa ushauri kama huu kwa mtu fulani simkumbuki. Basi ngoja nishare na wewe pia nahisi itakusaidia.

Mimi na mke wangu kuna kipindi mwaka jana tulijaribu sana kutafuta mtoto(na yeye ndiye alikuwa na hamu zaidi). Ndugu tulihangaika wapi. Tulitegesha siku zote wapi...... Kwanini hatukuamini(hata mimi sikuamini) kuwa labda tuna matatizo.

1. Mke wangu alishawahi kubeba ujauzito zamani kidogo ila akamiscarry mapema sana. Kwahiyo uwezo wa kushika mimba anao.

2. Mimi pia nilishawahi katika pitapita zangu kujaza wadada fulani hivi so mimi pia uwezo wa kuzalisha ninao.

Tatizo nini??

Stress!!!!! Kufanya mapenzi na kutafuta mtoto kwa stress ndugu haupati kitu!! Yani mtoto anatungwa mwenyewe taratibu bila hata kuwa na mawazo lukuki.

Cha kufanya
Kuna vidonge fulani(ingawa sishauri sana) vya hormones. Nenda pale Kairuki kuna Dr. mmoja mmama hivi(jina nimesahau) ila ukimuulizia utampata. Dr mmama kwa ajili ya kina mama!! Vidonge vyenyewe ni bei ndogo sidhani kama vinazidi Tsh 2000/-

Hii iwe last option ila potezeeni kabisa mambo ya ujauzito. Nyie kuleni raha na tendo la ndoa kwa furaha zote. Badilisheni sehemu, positions ila mkiwa na lengo la kufurahishana. Mawazo ya mtoto weka kapuni.

Amini nakwambia utapewa suprise na utakuja hapa ukiwa na furaha tele.

Je itakuwaje kama hali itaendelea kwa kipindi cha mwaka mmoja ujao?
Hapo niashauri mkaonane na Daktari bingwa.

Natumai nitakuwa nimekusaidia
 
Mwenyezimungu mtukutu muumba mbingu na ardhi na vilivyomo duniani amesema hivi:-
"Hakika sisi ndio tunamjalia mtu watoto wa kiume watupu wengine tunawapa wakike watupu wengine tunawachanganyia wakike na wakiume na wengine tunawanyima kabisa na tunampa mtu bila ya hisabu"

Muombe mungu atakujaalia na ujue kua kuna namna ya kuomba ili dua yako ijibiwe jitahidi kula halali na epuka sana haramu
 
pole sana kaka inawezekana mara nyingi uapofanya mapenzi, shahawa huwa hiziki sehemu husika kulingana staili unayotumia.. ili yai lilutubishwe linahitaji mbegu wastani wa kijiko cha chakula ambacho huwa na wastani wa mbegu 1000000.
Kutopata mtoto kunasababishwa na mambo mengi,Nendeni hospitali mkapimwe na kama wewe au mkeo hamna tatizo lolote, ni PM nikupatie dawa fulani ya chakula mtakayotumia wote ambayo inachochea uzazi.
 
Ukienda CCBRT ULIKOSHAURIWA na KAMA hukuona mafanikio au kama hamjaenda haraka sana kumbilieni MIKOCHENI HOSPITAL KWA SASA KAILUKI hospital mkaonane na DR Clementina ni mtoto wa KAILUKI mwenye hospital ni GYNO Na ni MWISHO wa matatizo ya uzazi.Niamini mimi yule dada amesomea URUSI kwenye mabingwa wa mambo hayo!na anajua sana niamini mimi na hata kama una BIMA YA AFYA AU PRIVATE VYOTE SAWA!UTANIPA JIBU!
 
Naungana na Madamex huo ni muda mfupi sana. Ila napenda kuwatia moyo katika Bwana kuwa mtoto ni baraka na zawadi toka kwa Bwana ila si sehemu ya ndoa yenu hivyo kuweni waangalifu jambo hilo lisije kula raha ya ndoa yenu mimi nina rafiki zangu wengi wengine miaka kumi, mitano, mitatu hawana watoto bado wana imani siku moja Mungu atawapa kwani yeye hakawihi wala hachelewi na pia jifunze kwa Abraham jinsi alivyopata mtt katika miaka karibia mia na maandiko yanasema Sara mkewe siku zake zilikuwa zimesha koma kama ilivyodesturi ya wanawake. hii yote inaonyesha uweza wa Mungu. Heri wamtumainio Bwana hawatatayahari.
 
Mkuu jenereta, kama walivoshauri wengine, inawezekana bado ni mapema kwa wewe kuwazia sana mtoto kama ndoa yenu ina mwaka mmoja tu....hasa kama tukienda na ile dhana ya kwamba mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu

kwa upande mwingine, una haki kujiuliza labda miezi 12 yote kumetokea nini hadi sasa hamjapata mtoto?

Sina uhakika sana na ufahamu wenu wa elimu ya uzazi, na huenda pia daktari wa CCBRT amewaambia, ila kwenye kupata mimba mambo mengi yanahusika

  • kwanza msiwe na msongo wa mawazo, kwa maana ya stress
  • Mfahamu vizuri cycle ya mkeo.....ili mjue ni wakati gani hasa wa kufanya mapenzi..jua ana mzunguko wa siku ngapi, ana enda hedhi siku ngapi, na hivyo unaweza kukadiria kwamba siku ya kuchavusha yai ni siku gani (kama hana tatizo la kiafya na wewe huna pia)
  • hakikisheni kwamba kwe mkeo je, hajawahi kutoa mimba, au kuwa na miscarriage, na sababu ilikuwa nini
  • Siku hizi kuna 'mlipuko' wa fibroids kwa wanawake wengi, na hii kwa wengine inasababisha wasipate mimba kirahisi
Nisingeshauri muanze kutumia dawa zozote kabla hamjajiridhisha na hayo hapo juu

Nawatakia kila la heri
 
Last edited by a moderator:
Yaani mwaka 1 unalalamika nina dada mmja alikaa 12yrs bila mtoto na mwaka huu january 2013 kapata mtoto

Nivea, sidhani kama ni furaha kufurahia tatizo na kuli-entertain, sio kwamba dadaako kakaa muda mrefu basi wote iwe hivyo, sidhani, nashukuru watu baadhi wamenishauri na nafurahi, matatizo mengine ni sisi wenyewe kutojua, mfano suala la damu kutoendana, haipelekei tusubiri miaka 12 km dadaako. Lakn nashukuru pia na mpe HONGERA huyo dada.
 
Mkuu,

Nilishawahi kutoa ushauri kama huu kwa mtu fulani simkumbuki. Basi ngoja nishare na wewe pia nahisi itakusaidia.

Mimi na mke wangu kuna kipindi mwaka jana tulijaribu sana kutafuta mtoto(na yeye ndiye alikuwa na hamu zaidi). Ndugu tulihangaika wapi. Tulitegesha siku zote wapi...... Kwanini hatukuamini(hata mimi sikuamini) kuwa labda tuna matatizo.

1. Mke wangu alishawahi kubeba ujauzito zamani kidogo ila akamiscarry mapema sana. Kwahiyo uwezo wa kushika mimba anao.

2. Mimi pia nilishawahi katika pitapita zangu kujaza wadada fulani hivi so mimi pia uwezo wa kuzalisha ninao.

Tatizo nini??

Stress!!!!! Kufanya mapenzi na kutafuta mtoto kwa stress ndugu haupati kitu!! Yani mtoto anatungwa mwenyewe taratibu bila hata kuwa na mawazo lukuki.

Cha kufanya
Kuna vidonge fulani(ingawa sishauri sana) vya hormones. Nenda pale Kairuki kuna Dr. mmoja mmama hivi(jina nimesahau) ila ukimuulizia utampata. Dr mmama kwa ajili ya kina mama!! Vidonge vyenyewe ni bei ndogo sidhani kama vinazidi Tsh 2000/-

Hii iwe last option ila potezeeni kabisa mambo ya ujauzito. Nyie kuleni raha na tendo la ndoa kwa furaha zote. Badilisheni sehemu, positions ila mkiwa na lengo la kufurahishana. Mawazo ya mtoto weka kapuni.

Amini nakwambia utapewa suprise na utakuja hapa ukiwa na furaha tele.

Je itakuwaje kama hali itaendelea kwa kipindi cha mwaka mmoja ujao?
Hapo niashauri mkaonane na Daktari bingwa.

Natumai nitakuwa nimekusaidia

Nimeipenda sana kaka, hata jana kuna daktari mmoja alishauri hivyo, safi sana kaka. Ni kweli kbs sometimes tunakamia, hata wife analia akiziona siku zake tena. NASHUKURU SANA KAKA
 
Mwenyezimungu mtukutu muumba mbingu na ardhi na vilivyomo duniani amesema hivi:-
"Hakika sisi ndio tunamjalia mtu watoto wa kiume watupu wengine tunawapa wakike watupu wengine tunawachanganyia wakike na wakiume na wengine tunawanyima kabisa na tunampa mtu bila ya hisabu"

Muombe mungu atakujaalia na ujue kua kuna namna ya kuomba ili dua yako ijibiwe jitahidi kula halali na epuka sana haramu

SURE ndugu yangu
 
Ukienda CCBRT ULIKOSHAURIWA na KAMA hukuona mafanikio au kama hamjaenda haraka sana kumbilieni MIKOCHENI HOSPITAL KWA SASA KAILUKI hospital mkaonane na DR Clementina ni mtoto wa KAILUKI mwenye hospital ni GYNO Na ni MWISHO wa matatizo ya uzazi.Niamini mimi yule dada amesomea URUSI kwenye mabingwa wa mambo hayo!na anajua sana niamini mimi na hata kama una BIMA YA AFYA AU PRIVATE VYOTE SAWA!UTANIPA JIBU!

Nashukuru ndugu yangu. Nitakujulisha
 
Mkuu jenereta, kama walivoshauri wengine, inawezekana bado ni mapema kwa wewe kuwazia sana mtoto kama ndoa yenu ina mwaka mmoja tu....hasa kama tukienda na ile dhana ya kwamba mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu

kwa upande mwingine, una haki kujiuliza labda miezi 12 yote kumetokea nini hadi sasa hamjapata mtoto?

Sina uhakika sana na ufahamu wenu wa elimu ya uzazi, na huenda pia daktari wa CCBRT amewaambia, ila kwenye kupata mimba mambo mengi yanahusika

  • kwanza msiwe na msongo wa mawazo, kwa maana ya stress
  • Mfahamu vizuri cycle ya mkeo.....ili mjue ni wakati gani hasa wa kufanya mapenzi..jua ana mzunguko wa siku ngapi, ana enda hedhi siku ngapi, na hivyo unaweza kukadiria kwamba siku ya kuchavusha yai ni siku gani (kama hana tatizo la kiafya na wewe huna pia)
  • hakikisheni kwamba kwe mkeo je, hajawahi kutoa mimba, au kuwa na miscarriage, na sababu ilikuwa nini
  • Siku hizi kuna 'mlipuko' wa fibroids kwa wanawake wengi, na hii kwa wengine inasababisha wasipate mimba kirahisi
Nisingeshauri muanze kutumia dawa zozote kabla hamjajiridhisha na hayo hapo juu

Nawatakia kila la heri

Tunashukuru ndugu yangu. Kweli nimekuwa mwenye faraja sana, tena ndoa yenyewe hata one yr anniversary baso wiki 4 tu. Ni kweli kaka, labda msongo wa mawazo unatuumiza pia.
Thanx ndugu yangu
 
Last edited by a moderator:
nendeni hospitali mtapata majibu ya tatizo mungu atawasaidia mtapata mtoto
 
WanaJF, naombeni msaada wenu
Nimeoa mwaka jana, na nampenda sana mke wangu, nampenda sana, lakini toka mwaka jana sijabahatika kupata mtoto, ingawaje kuna siku nilimkuta analia, nikamuuliza unalia nn akasema, ameingia kwenye siku zake while ana hamu ya kupata mtoto, nikamwomba a-calm down though hata mm iliniuma sana.
Hatujaenda bado hosp, lakini naombeni msaada kama kuna watu mna xperience na haya mambo kabla sijaenda hospitali, na tumevizia siku za hatari lakini wapi, please, naombeni msaada wenu wapendwa, natamani sana mtoto.
Asante[/QU
 
Back
Top Bottom