Msaada wa kutengeneza SONY XPERIA

Cendy

JF-Expert Member
Joined
Mar 28, 2015
Posts
1,252
Reaction score
2,314
Wakuu awali ya yote nawasalimu kwa jina la muumba mbingu na nchi.
.
Wakuu simu yangu aina ya Sony xperia ina tatizo la kukata network na kuandika hakuna sim card mara kwa mara

Pia inatatizo la kupoteza kumbukumbu (inaondoa program niliokuwepo awali wakati naitumia)

Nilikuwa naomba kujua tatizo ni nini maana nime restore ndio shida imezidi

Pia naomba kujua kama kuna program ya ku upgrade androids yake au ku boost system yake

Nimekuwa nikisaidiwa sana kwenye jukwaa hili natumaini mtanisaidia pia
 
Shida uliyonayo ni kama yangu natumiani nitapata MAJIBU kupitia thread hii
 
Watu wako kimya
 
Hii sio sony hii ni mfano wake.
 
kwa kuiangalia tu kuna uwezekano mkubwa ni clone ya sony, sio xperia original. jaribu kutafuta mtaalamu karibu na kwako ajaribu kukuflashia modem
Kama sio original aki flash itawezekana kweli chief
 
most of now Sony experia are fake .....mi nshawah badilisha sim mbili za aina hiyo tena Z4...... nakushuri uhamie tu huawei
 
most of now Sony experia are fake .....mi nshawah badilisha sim mbili za aina hiyo tena Z4...... nakushuri uhamie tu huawei
Isije kuwa ndo imekufa
 
most of now Sony experia are fake .....mi nshawah badilisha sim mbili za aina hiyo tena Z4...... nakushuri uhamie tu huawei

SONY original ziko nyingi sana ila tatizo ni watu hawajui fake ni ipi na original ni ipi.
 
Ilo tatizo linatokana na simu yako kuwa feki. Angalia GB yake ni ndogo tofauti na orgn
 
Inaonekana ina GB kubwa tu
 
Hiyo sony sio copy!??,angalia kwa makini unaeza ona kuna uwezo wa kuweka chip ya pili,kama sehemu ya memory ni ya line pia ujue kichina hicho
 
Hiyo sony sio copy!??,angalia kwa makini unaeza ona kuna uwezo wa kuweka chip ya pili,kama sehemu ya memory ni ya line pia ujue kichina hicho
Ina chip moja tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…