Msaada wa kuokoa nyumba, wadudu wanaharibu mbao

Teleskopu

JF-Expert Member
May 5, 2017
702
763
Wakuu naomba msaada wa maarifa na jinsi ya kufanya.

Kuna wadudu wanatafuna mbao za nyumba, milango, makochi, vitanda na chochote kilichotengenezwa kwa ubao.

Wanapokula utadhani mtu anapitishisha msumeno. Utakapoona ni unga tu ukipukutika chini.
Maana yake, kama wakiendelea paa litakuwa weak; litazidiwa na uzito; na hatimaye
litananihii .... naogopa hata kusema!!

Ukibomoa sehemu iliyoliwa, unakuta shimo na unga wa kutosha unamwagika chini.
Na wadudu wenyewe ni aina ya cartepillar.

Msaada tafadhali. Suluhisho lake ni nini?


Huyu ndio mhalifu mwenyewe.​
 
Mkuu chakii hii ni kwa ajili ya mbao ambazo hazijavamiwa (ili kukinga) au hata kuponya zile ambazo tayari wadudu wamo ndani?
 
Hao wadudu wanaokusumbua kwetu mboga nshangaa unasumbuliwa na kitoweo niuzie hiyo nyumba pamoja nasamani chakavu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…