Wakuu,
Kampuni yangu ina ugomvi na serikali ya mamlaka ya mji mdogo kwenye moja ya wilaya zetu. Juhudi za kutumia njia za kawaida kutatua tatizo zimeshindikana. Wanagoma kutoa leseni ya biashara kwasababu za kipuuzi mno. Naamini walikuwa wanataka rushwa kwa kujifanya kuchelewesha mambo na kuja na madai ya ajabu ajabu. Mimi nimeweka msimamo wazi, sitoi na wala sitatoa, bora hata waninyime kabisa hiyo leseni.
Je unaweza kuwapeleka hawa watu mahakamani? Hapo unawashitaki mamlaka ya mji mdogo au unaishitaki halmashauri ya wilaya.
Pia kesi kama hiyo unaifungua kwenye mahakama gani? Kama imeshindikana kupata haki kwenye vikao vya watendaji basi tuende hata mahakamani.
Nitashukuru kwa mabingwa wa sheria kunipatia elimu tosha. Hapa au kwa PM kote sawa tu.
Kampuni yangu ina ugomvi na serikali ya mamlaka ya mji mdogo kwenye moja ya wilaya zetu. Juhudi za kutumia njia za kawaida kutatua tatizo zimeshindikana. Wanagoma kutoa leseni ya biashara kwasababu za kipuuzi mno. Naamini walikuwa wanataka rushwa kwa kujifanya kuchelewesha mambo na kuja na madai ya ajabu ajabu. Mimi nimeweka msimamo wazi, sitoi na wala sitatoa, bora hata waninyime kabisa hiyo leseni.
Je unaweza kuwapeleka hawa watu mahakamani? Hapo unawashitaki mamlaka ya mji mdogo au unaishitaki halmashauri ya wilaya.
Pia kesi kama hiyo unaifungua kwenye mahakama gani? Kama imeshindikana kupata haki kwenye vikao vya watendaji basi tuende hata mahakamani.
Nitashukuru kwa mabingwa wa sheria kunipatia elimu tosha. Hapa au kwa PM kote sawa tu.