Msaada wa kisheria tafadhari.

Uduvi

JF-Expert Member
Sep 3, 2012
738
518
Ni hatua gani ambayo natakiwa kufuata.Nilimpa pikipiki jamaa mmoja hivi awe anaendesha kwa mkataba wa kuwa ananipa sh elfu 10 kwa siku baada ya miezi Nane pikipiki ingekuwa yake,baada ya wiki tatu tokea nimempa pikipiki akanipigia simu mida ya saa 11 alfajiri kuniambia pikipiki imeibiwa sikukubaliana nae nikamuweka ndani polisi kilwa road kwa siku mbili siku ya tatu akapelekwa mahakamani temeke pale karibu na usalama.Kesi ikendeshwa na mwisho wa siku nikashinda na jamaa akafungwa kifungo cha nnje cha mwaka mmoja na miezi miwili kila siku alikuwa anatakiwa kwenda kuripoti mahakamani na ndani ya iyo miezi miwili alitakiwa anilipe.inshu inakuja kwa mkuu wa iyo mahakama inaonekana amepata mlungula na hafuatilii kujua jamaa kama amelipa au hata kama alilipoti siku aliyopangiwa.nimehangaika sana na jamaa namuona tu mtaani afu mahakama haitendi haki.nilikuwa naomba wabobezi wa sheria mnieleze ni taratibu gani naweza kuzifuata kudai haki yangu,maana nilijbana ili nitusue lkn ndio hivyo navutwa shati nyuma.Msaada tafadhari
 
Mpaka kupata ushindi mahakamani mlikuwa tayari mmeandikishana na huyo jamaa, nikimaanisha mkataba wowote?
 
Mkuu hapa msaada wa haraka ni kumuita Mng'oa kucha tu, hakimu atamtafuta mtuhumiwa wako haraka sana baada ya huyo bwana kusema lolote.
 
Mpaka kupata ushindi mahakamani mlikuwa tayari mmeandikishana na huyo jamaa, nikimaanisha mkataba wowote?
Ndio tuliandikishana mkataba na mashahidi walikuja kutoa ushahidi kwamba ni kweli nilimkabidhi pikipiki mbele yao ila jinsi ilivyoibiwa wao hawajui.
 
Mkuu hapa msaada wa haraka ni kumuita Mng'oa kucha tu, hakimu atamtafuta mtuhumiwa wako haraka sana baada ya huyo bwana kusema lolote.
Mahakama zinatakiwa zitende haki vinginevyo mtu unaweza chukua hatua mwenyewe ikaja kuwa balaaa.
 
Ndugu ukifika muda wake kama hajalipa nenda mahakamani anawekwa tena ndani na kifungo kinaendelea
 
Mkuu kesi yako ilisha hukumiwa inaitwa (probation sentence) ambapo adhabu ni kifungo cha nje kwa matazamio asipo tekereza hukum io analudishwa tena mahakani suara LA kutofika MAHAKAMAN si lako iachie mahakama kimsingi inatakaiwa udai alipe hela yako akishindwa unaomba kukaza hukum na pesa ilibaki sh ngp na yey ni binadamu km we tu ...pengine aliibiwa kweri mfano ingenue's kwako vip.OBITER DICTUM #
 
Mkuu kesi yako ilisha hukumiwa inaitwa (probation sentence) ambapo adhabu ni kifungo cha nje kwa matazamio asipo tekereza hukum io analudishwa tena mahakani suara LA kutofika MAHAKAMAN si lako iachie mahakama kimsingi inatakaiwa udai alipe hela yako akishindwa unaomba kukaza hukum na pesa ilibaki sh ngp na yey ni binadamu km we tu ...pengine aliibiwa kweri mfano ingenue's kwako vip.OBITER DICTUM #
Shukrani kwa ushauri mkuu.pesa ni 2.25m hajalipa hata senti hadi sasa.mahakamani wananiambia nichukue samansi kwa mara ya pili kama vipi?
 
Nenda kachukue summons ili mkutane mahakamani km hakuna utekelezaji mahakama iko huru haingiliwi maamuzi yake. ila mahakama inaigiliana yenyewe kwa mahakama nyingine kuna procedure ya kufanya kam kuna ujanja unafanyika hapo mahakamani na utafanikiwa ,( quid pro quo)*
 
Acha ubahili....find a lawyer....kuna watu wamesomea izo kazi...sasa kufa kufaana...shida zako ndo zinafanya waishi mjini
 
Nlitaman nichat naww maana kukushaur kuna maelezo ya ziada yanahitajika, kwan mda alopewa kulipa umeisha wa kulipa? Kama ndio kakaze hukum ili uweze kushikilia mali zake na ikiwezekana uuze ili kurecover deni lako. Pole sana
 
Nlitaman nichat naww maana kukushaur kuna maelezo ya ziada yanahitajika, kwan mda alopewa kulipa umeisha wa kulipa? Kama ndio kakaze hukum ili uweze kushikilia mali zake na ikiwezekana uuze ili kurecover deni lako. Pole sana
Shukrani kwa ushauri.mahakama inaniambia nikachunguze Mali za huyo mtu sasa mm nitachunguzaje adui yangu wakati hilo naona ni suala la kipolisi kufanya uchunguzi.nashukuru kwa ushauri wa wadau wengine Jana nimefanikiwa kuchukua samansi nyingine na leo nafanya utaratibu wa kumkabidhi mbele ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa.
 
Ipo hivi kuna kijana ni mtumishi wa uma alikuwa anashukiwa kwa wizi, ijapokuwa ushahidi wote uliotolewa polisi ulithibitika hakuhusika, polisi wali amuru kesi hiyo itolewe polisi ipelekwe halmashauri ambako mshukiwa ameajiriwa, wazee wetu mnawajua, wakamshauri na kumlazimisha akubali kulipa yaishe ili asije kurudishwa rumande, kutokana na woga na kutokujuasheria yule kijana alikubali kwakuweka sahihi ya malipo katika barua iliyo andikwa na afisa mmoja pale almashauri, sasa imefika hatua yule kijana ameshindwa kulipa na mdai wake anamsumbua sana, pindi anapopeleka huo ushaidi kwenye kituo chochote nchin yule kijana hukamatwa na kuwekwa ndani popote anapokuwa, sasa amechoka na anateseka, Mimi nilikuwa pamoja nae mwanzo wa hili jambo hadi sasa na niko tayari kusimamia mahakaman kam shahidi wake maana nashuhudia hakika hakutenda ilo tukio sasa yeye ameamua kwenda mahakamani maana mdai wake hataki kwenda, Anaomba msaada kwenu wana JF manguli wa sheria je afanyeje au apitie hatua gani ili kufungua madai yake?
maana anaamini kabisa ushahidi anao wakumvusha kwenye hili jaribuuu!
 
Shukrani kwa ushauri.mahakama inaniambia nikachunguze Mali za huyo mtu sasa mm nitachunguzaje adui yangu wakati hilo naona ni suala la kipolisi kufanya uchunguzi.nashukuru kwa ushauri wa wadau wengine Jana nimefanikiwa kuchukua samansi nyingine na leo nafanya utaratibu wa kumkabidhi mbele ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa.
Ok sawa subir polis ikufanyie hyo kazi
 
We subiri muda wa kifungo chake kwisha akitoka ndo upeleke ile ukumu ambayo alitakiwa akulipe hapo sasa unafungua kesi nyingine ya madai.
 
We subiri muda wa kifungo chake kwisha akitoka ndo upeleke ile ukumu ambayo alitakiwa akulipe hapo sasa unafungua kesi nyingine ya madai.
 
We subiri muda wa kifungo chake kwisha akitoka ndo upeleke ile ukumu ambayo alitakiwa akulipe hapo sasa unafungua kesi nyingine ya madai.
kama anatumikia kifungo cha nje cha kwenda kufagia tu maeneo ya umma, kwanini asipata nakala ya hukumu akafungua madai leoleo?

pia, tembelea web za wanasheria wanauza vitabu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom