Kilele9
JF-Expert Member
- Jun 1, 2017
- 1,452
- 1,091
Wasomi /wakuu habari za siku,
Mimi ninatatizwa na usemi hapo juu maarufu "kujichukulia sheria mkononi"
Hivi karibuni kumetokea baadhi ya wananchi kufanya maamuzi kinyume na sheria
(nionavyo mimi) na hapa ndipo ninaomba ufafanuzi/ kufahamishwa.
Mifano ni mingi ila kwa sasa ninanukuu huu hapa:
"Dar es Salaam. Watu watano wanaodaiwa kuwa ni wahalifu wameuawa katika eneo la Toangoma jijini Dar es Salaam, katika majibizano ya risasi na Polisi yaliyotokea usiku wa kuamkia leo Ijumaa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Emmanuel Lukula amesema walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwa kuna njama za uhalifu zimepangwa kufanyika maeneo hayo usiku wa jana, hivyo wakajipanga kwa ajili ya kudhibiti.
Amesema ilipofika muda walioambiwa kweli wahalifu hao ambao idadi yao haikuweza kupatikana, lakini walikuwa wengi, wakafika eneo la tukio na kupambana na polisi.
“Majibizano ya silaha yalikuwa makubwa kwa sababu walikuwa na silaha nzito, lakini Jeshi la Polisi lilijipanga imara kuwadhibiti na kufanikiwa kuua watano na wengine wakatokomea kusikojulikana,” amesema."
Kama hiyo hapo juu ni kweli watuhumiwa watano wameshahukumiwa kabla ya kufika
mahakamani na hakukamatwa hata mmoja wa kuendesha kesi .
Swali langu:
Mimi ninatatizwa na usemi hapo juu maarufu "kujichukulia sheria mkononi"
Hivi karibuni kumetokea baadhi ya wananchi kufanya maamuzi kinyume na sheria
(nionavyo mimi) na hapa ndipo ninaomba ufafanuzi/ kufahamishwa.
Mifano ni mingi ila kwa sasa ninanukuu huu hapa:
"Dar es Salaam. Watu watano wanaodaiwa kuwa ni wahalifu wameuawa katika eneo la Toangoma jijini Dar es Salaam, katika majibizano ya risasi na Polisi yaliyotokea usiku wa kuamkia leo Ijumaa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Emmanuel Lukula amesema walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwa kuna njama za uhalifu zimepangwa kufanyika maeneo hayo usiku wa jana, hivyo wakajipanga kwa ajili ya kudhibiti.
Amesema ilipofika muda walioambiwa kweli wahalifu hao ambao idadi yao haikuweza kupatikana, lakini walikuwa wengi, wakafika eneo la tukio na kupambana na polisi.
“Majibizano ya silaha yalikuwa makubwa kwa sababu walikuwa na silaha nzito, lakini Jeshi la Polisi lilijipanga imara kuwadhibiti na kufanikiwa kuua watano na wengine wakatokomea kusikojulikana,” amesema."
Kama hiyo hapo juu ni kweli watuhumiwa watano wameshahukumiwa kabla ya kufika
mahakamani na hakukamatwa hata mmoja wa kuendesha kesi .
Swali langu:
- Je hivi ndivyo utawala wa sheria unavyotaka !?
- Je wananchi mmoja mmoja au kikundi wakifanya hivyo jeshi letu na mahakama zetu zitaamuaje?