Msaada wa kisheria kesi ya kupiga muharifu

ntilavano

Senior Member
Mar 10, 2015
136
31
Wakuu natumaini mu wazima wa afya.

Ishu iko hivi, kuna rafiki yangu mmoja alifanyiwa vurugu na jamaa mmoja ivi na kupoteza kitambulisho chake cha kazi hivyo aliniomba niende nikamsaidie katika hizo purukushani.
Tulipofika eneo la tukio tulimpata muhusika na kumchukua lengo kumpeleka polisi ila yule mharifu alituomba sana tumsamehe na sisi tukafanya ivyo ila kwa sharti moja tu tupate kile kitambulisho.

Baada ya kukubaliana atakitafuta kitambulisho na kukileta tukaachana nae mwenzetu kaenda kituo cha polisi na kufungua kesi ya kupigwa na kuibiwa 210000(laki mbili na kumi) kumtafuta kukaa ili yaishe kasema anataka million 3 kama hapewi kesi anapeleka mahakamani.

Sasa shida yangu ni kwamba je hii kesi tunaweza solve vipi akienda mahakamani itafika hiyo 3mil au atalipwa kiasi anachodai kupotelewa 210000 au kuna namna yoyote ya kumshinda huyu jamaa kisheria ukizingatia yeye ndie alikua muharifu ila tatizo tulishindwa kumpeleka polisi na wala hatukukata RB ya polisi.

Nawasilisha kwa wanasheria.
 
Kuna tofaut kati ya kupigwa huyo jamaa na nyie kulipa mil 3. Kupigwa ni jinai. Na ina adhabu ndogo. mil 3 ni hesab zake tu kichwan na si sheria. Laxima pia yaonekane madhara makubwa ya kipigo hicho ili madai yake yawe na maana. La sivyo asubiri tu majibu ya jinai na anaweza kutoambulia malipo yoyote. Inabid athibitishe alikuwa na hizo lak 210000. Bora mwende mahakaman.
 
Kuna tofaut kati ya kupigwa huyo jamaa na nyie kulipa mil 3. Kupigwa ni jinai. Na ina adhabu ndogo. mil 3 ni hesab zake tu kichwan na si sheria. Laxima pia yaonekane madhara makubwa ya kipigo hicho ili madai yake yawe na maana. La sivyo asubiri tu majibu ya jinai na anaweza kutoambulia malipo yoyote. Inabid athibitishe alikuwa na hizo lak 210000. Bora mwende mahakaman.
Shukrani sana mkuu na kwahiyo sanasana itatakiwa faini ya hiyo kesi au kuna kifungo hapo?
 
Back
Top Bottom