Habari za mchana wana ndugu
Jana usiku nikiwa nimepimzika na mke wangu kipenzi; gafla nilipokea simu kutoka kwa mmoja Wa wanandoa akiniambia kuwa amemua kuachana na mwana ndoa mwezie; na kesho asubuhi (Leo asubuhi) kitakuwa na kikao cha kugawana mali na tunakuomba ufike ukiwa kama mwanafamilia.
Nilichukua muda kutafakari juu ya hili; asubuhi nikajihimu mapema kwa lengo LA kwenda nyumbani kWa wahusika japo tayari mmoja Wa wanandoa ameshaondoka yupo kwa ndugu zake. Kabla sijafanya hivyo ilibidi nimpigie mmoja Wa wanandoa (mwanaume) ili nipate nafasi ya kuonana nae mapema kabla ya kikao hicho nikiwa na lengo la kunusuru kutokuvunjika kwa ndoa hiyo. Nashukuru Mungu niliongea na mwanandoa huyo na akakubari kuonana nae kwa masharti ya kuwahi kufika Nyumbani kwake!
Nikifika eneo hilo; kwanza nikamsifia kwa ujenzi Wa nyumba nzuri na kujuliana habari za Maisha.
Then; tulianza mazungumzo ya kina juu ya matatizo hayo! Lakini ikumbukwe kwa muda wote huo tulikuwa wawili tu! Alinieleza mambo mengi sana yanayomuhusu mke wake. Ikiwemo mke kupishana kimaneno na mkwe wake, mwanamke kuwa na mawasiliano na mpenzi wake Wa zamani, tuhuma za uchawi, lakini kubwa zaidi ni mke kuchelewa kurudi nyumbani Mara kadhaa yeye mume akiwa amslesafiri kikazi na habari hizo kuzipata kwa majirani.
Wakati tukiwa katikati ya mazungumzo; mke akiingia na tukaungana ktk mazungumzo; baadae nilimpa nafasi mwaname kuongea ilionekana kuwa mwanaume ana mwanamke mwingine na amemjengea nyumba na anamezaa nje ya ndoa.
Pia mwanamke amelalamika kuwa anazaidi ya miezi Tisa hajakutana kimwili na Mme wake na kila akihitaji unyumba kutoka kwa Mme wake Mme hataki; wakati mke akiendelea kuongea mume alikuja juu akataka kumpiga mke kwa lengo la kutokutaka mwanamke asiendelee kuongea; bahati nzuri nikadhibiti hari hiyo!
Binafsi niliwasihi na hususani Mme nilimsihi ahairishe maamuzi yake ya kutaka kuuza nyumba na kugawana fedha na Mali zingine; nilimsihi hivyo coz ana watoto wawili ambao watahitaji kuendelea kuishi ktk hiyo nyumba.
Sikutaka kuingilia maamuzi ya Mme kubatilisha maamuzi ya taraka alompa mke wake!
Lakini Mme hataki kabisa mke wake arudi ktk nyumba hiyo hari kadharika mke hataki kuendelea na ndoa pia
Lakini niligundua pia; taraka ilotolewa ikikuwa batiri coz haina mashaidi na sahihi zake na wala haitaji tarehe ya kuachana na sababu za kuachana
Ninakuja kwenu kuomba msaada Wa mawazo nifanyeje kusaidia kuinusuru ndoa hii au kuwapa ushauri utakaowafaa.
Jana usiku nikiwa nimepimzika na mke wangu kipenzi; gafla nilipokea simu kutoka kwa mmoja Wa wanandoa akiniambia kuwa amemua kuachana na mwana ndoa mwezie; na kesho asubuhi (Leo asubuhi) kitakuwa na kikao cha kugawana mali na tunakuomba ufike ukiwa kama mwanafamilia.
Nilichukua muda kutafakari juu ya hili; asubuhi nikajihimu mapema kwa lengo LA kwenda nyumbani kWa wahusika japo tayari mmoja Wa wanandoa ameshaondoka yupo kwa ndugu zake. Kabla sijafanya hivyo ilibidi nimpigie mmoja Wa wanandoa (mwanaume) ili nipate nafasi ya kuonana nae mapema kabla ya kikao hicho nikiwa na lengo la kunusuru kutokuvunjika kwa ndoa hiyo. Nashukuru Mungu niliongea na mwanandoa huyo na akakubari kuonana nae kwa masharti ya kuwahi kufika Nyumbani kwake!
Nikifika eneo hilo; kwanza nikamsifia kwa ujenzi Wa nyumba nzuri na kujuliana habari za Maisha.
Then; tulianza mazungumzo ya kina juu ya matatizo hayo! Lakini ikumbukwe kwa muda wote huo tulikuwa wawili tu! Alinieleza mambo mengi sana yanayomuhusu mke wake. Ikiwemo mke kupishana kimaneno na mkwe wake, mwanamke kuwa na mawasiliano na mpenzi wake Wa zamani, tuhuma za uchawi, lakini kubwa zaidi ni mke kuchelewa kurudi nyumbani Mara kadhaa yeye mume akiwa amslesafiri kikazi na habari hizo kuzipata kwa majirani.
Wakati tukiwa katikati ya mazungumzo; mke akiingia na tukaungana ktk mazungumzo; baadae nilimpa nafasi mwaname kuongea ilionekana kuwa mwanaume ana mwanamke mwingine na amemjengea nyumba na anamezaa nje ya ndoa.
Pia mwanamke amelalamika kuwa anazaidi ya miezi Tisa hajakutana kimwili na Mme wake na kila akihitaji unyumba kutoka kwa Mme wake Mme hataki; wakati mke akiendelea kuongea mume alikuja juu akataka kumpiga mke kwa lengo la kutokutaka mwanamke asiendelee kuongea; bahati nzuri nikadhibiti hari hiyo!
Binafsi niliwasihi na hususani Mme nilimsihi ahairishe maamuzi yake ya kutaka kuuza nyumba na kugawana fedha na Mali zingine; nilimsihi hivyo coz ana watoto wawili ambao watahitaji kuendelea kuishi ktk hiyo nyumba.
Sikutaka kuingilia maamuzi ya Mme kubatilisha maamuzi ya taraka alompa mke wake!
Lakini Mme hataki kabisa mke wake arudi ktk nyumba hiyo hari kadharika mke hataki kuendelea na ndoa pia
Lakini niligundua pia; taraka ilotolewa ikikuwa batiri coz haina mashaidi na sahihi zake na wala haitaji tarehe ya kuachana na sababu za kuachana
Ninakuja kwenu kuomba msaada Wa mawazo nifanyeje kusaidia kuinusuru ndoa hii au kuwapa ushauri utakaowafaa.