Mimi nimekoma kabisa siwezi tena kuhagaika na hawa jamaa! Mwishoni mwa mwaka jana nili order laptop na kisha nililipia kupitia utaratibu wao wa Tigopesa. Nimesubiri karibu mwezi ndiyo wananiambia order yangu imefutwa! Sikuwaelewa hata kidogo. Niliambiwa seller hana bidhaa hiyo tena. Wakaniambia nitafute laptop nyingine yenye thamani hiyo,nami nikafanya hivyo na kuongeza bidhaa nyingine kwa seller mwingine. Nako mambo ni yale yale! Safari hii nimeongea na watumishi kama watatu ambao kila mtu ni mbabaishaji tu. Nayo nikaambiwa order yangu imefutwa! Waliamua kunirudishia pesa zangu baada ya kwenda ofisini kwao. Walinirudishia pesa zangu kwa tigopesa ambapo nilipata hasara ya chargers wakati wa kuchukuwa taslimu. Ukweli ni wababaishaji na sijui matawi yao mengine katika nchi zingine yako kama hili la Tanzania!