Msaada tutani kuhusu Vodacom

MUSIGAJI

JF-Expert Member
Dec 26, 2014
2,187
2,462
Wanabodi habari nawasimu.

Kuna Jambo limetokea kwa dada fulani kwa kweli imenishangaza nikaona niilete hapa pengine ninaweza kupata mawazo na ushauri nikamfikishia au wahusika VODACOM wanawaza kushughulikia suala lake na kulitatua.

Huyu Dada anasimamia ofisi fulani inayoshughulika na huu uwakala wa MPESA, TIGOPESA n.k

Mwezi uliopita mwanzoni alikuja mtu akamwambia wako na kazi ya kujenga, sasa Kuna upungufu kidogo umejitokeza,Boss wao anaomba atume fedha kidogo kwenye simu yake ya voda (anayoitumia ya kawaida si ile ya uwakala) alafu atoe amkabidhi.

Akakubali huyo boss wao akatuma fedha, alituma mara mbili moja elfu 30 au 30+ na nyingine elfu 70 au 70+.

Baada ya kutumiwa akaitoa akamkabidhi yule bwana fundi.

Kumbe baada ya pale yule bwana aliyetuma (Boss wao) akapiga simu Voda, akasema ile 70 au 70+ ameituma kimakosa.

Sasa ilivyotumwa ndo aliitoa akamkabidhi bwana fundi,lakini alikuwa na fedha Kama laki tatu plus kwenye MPAWA.

Vodacom baada ya kupokea ile simu na wakaona alishaitoa basi wakafunga huduma ya MPESA. (Bila hata kumpigia kusikia kutoka kwake.)

Baada ya siku kadhaa akahitaji kutumia ile fedha iloyoko MPAWA akakuta kazuiliwa huduma,akapiga simu huduma kwa mteja ndo anaelezwa hivyo. Akaambiwa aende police kwanza,akaenda,kule akapewa RB then akaambiwa aende Voda wamfungulie akaunti.

Ameenda Voda,wanadai alipe kwanza ile fedha, kituko ni kwamba yule aliyetoa taarifa kuwa alituma fedha kimakosa,hata hapatikani kwenye ile simu,lakini Bado Voda wanasema aweke kwanza fedha kwenye akaunti yake (inaelekea walifunga huduma ya kutoa tu) ili hiyo fedha itumike kumlipa yule aliyedai ametuma kimakosa( japo hata simu yake haipatikani) alafu ndo afunguliwe huduma.

Alijaribu kwenda VODA makao makuu majibu yakawa yale yale. Binafsi bado nadhani walioshughulikia suala lake pale VODA tangu awali hawakuwa makini Kiieledi, Kwa mambo makuu mawili hivi.

Mosi, walipaswa kumpigia kusikia kutoka kwake punde baada ya kupokea malalamiko.

Pili, Baada ya yeye kigundua kuwa amefungiwa na akajoeleza kwao, walipaswa na wao walipomtafuta mlalamikaji bila kuopata simu yake kwa kitumia busara ya kawaida wangeona upande wa haki.

Wakuu, Je katika hali kama hii, huyu mdau ashauriwe Nini?
 
anatakiwa atoe hiyo hela yote mpawa kisha awakope mpawa na songesha avunje na line.

huu ujinga mwingine sio wa kuuchekea.
Ili aitoe hiyo fedha MPAWA lazima awe amerejeshewa huduma ya MPESA. Ili kurejeshewa MPESA lazima awe amemlipa yule tapeli.
 
Tuache hilo kwa dakkka moja, leo mchana huu nimenunua bando la 2,500/= la 1.5GB la masaa 24, hili bando limeisha kimasihara tu ndani ya 1 hour bila kufanya lolote la maana.

Moja ya mambo ambayo yameharibika sana katika miaka ya hivi karibuni, ni weledi na uaminifu wa makampuni yoooote ya mawasiliano. Nadhani serikali inachangia kwenye hili.
 
Tuache hilo kwa dakkka moja, leo mchana huu nimenunua bando la 2,500/= la 1.5GB la masaa 24, hili bando limeisha kimasihara tu ndani ya 1 hour bila kufanya lolote la maana.

Moja ya mambo ambayo yameharibika sana katika miaka ya hivi karibuni, ni weledi na uaminifu wa makampuni yoooote ya mawasiliano. Nadhani serikali inachangia kwenye hili.
Sina maslahi na kampun yoyote lkn ndg kuna mda nenda setting alafu restrict background data ..app peke ya data itakuwa n ile unayofungua

Alafu nenda play store kama unatumia sim za android toa automatic updates za app kuna mda tunalaumu sana mitandao lkn haya mambo humalza data balaa
 
Mimi kwa kweli nacho weza changia ni kumpa pole tu. Swala zima la mbinu za kujinufaisha kwa kila njia kupitia hizi simu za mkononi lipo juu mno mbinu hazi kwami kila siku. Ila bado mimi moyo wangu una kataa kabisa haya mambo naona kinga kubwa bado ipo haitaji application haitaji pesa ila mbinu ipo kwako wewe mwenye line mwenyewe. Naomba ni wakilishe kama ifwatavyo
1. Kwanini utume pesa kwa namba usio ijuwa? Wanao tuma akili zao huwa zina waza nini?
2. Kwanini mtu atume pesa kupitia namba yako na kuna namba ya wakala?
3.Kwanini umpe mtu simu yako na humfahamu?
4. Watu wana elewa nini maana ya line ya mtu binafsi?
5. Watu wana uelewa kwanini tuna sajili line kwa kitambulisho chako na sio cha ndugu au mke au mume?
kama watu wata weza tumia hata dakika 5 tujiuliza hao maswali hapo juu uta tambua simu yako ya mkononi ni kama jicho lako ni kwa matumizi yako binafsi sio yako na jirani. usimuazime mtu simu kupiga au kubeep au kutuma ujumbe wa maneno kwenda kwa mtu usiye mjuwa maana ina weza kuwa ana mpa taarifa nyeti mwisho ukamatwe wewe mwenye namba husika.
So kama kila mtu akiweza tambua simu ya mkononi sio ya kushare na mtu yoyote ni kwa matumizi binafsi nadhani uwizi utapungua.
 
Sina maslahi na kampun yoyote lkn ndg kuna mda nenda setting alafu restrict background data ..app peke ya data itakuwa n ile unayofungua

Alafu nenda play store kama unatumia sim za android toa automatic updates za app kuna mda tunalaumu sana mitandao lkn haya mambo humalza data balaa

Mkuu hawa watu ni washenzi sana. Sijaanza kutumia simu jana mimi, najua hizo habari za automatic update. Hauwezi kuniambia simu yangu imetumia 1GB kufanya update ya applications ndani ya 1 hour.

Wameniambia eti kuna bundle za 4G, labda nilitumia hiyo, eti hizo huwa zinaenda fasta. Hayo mambo sijaanza kuyasikia leo na ni aina nyingine haya makampuni yanaibia watu.

Kwa kuwa tu internet iko fasta haimaanishi itaenda kutumia mara 3 ya data kufanya kitu kile kile ambacho bundle ya kawaida ingefanya. Huo ni uongo na ni wizi wa mchana. Kama huko kuvuja kwa data kwa sababu ya speed kali inayotumika, itaongezeka kwenye MBs 100 huko na na siyo 1.5 GB ili ku upload video ya 500 MB, halafu tena inakata baada ya 40%.

Washenzi sana haya makampuni yote na wale wanaowalinda.
 
Wakuu,sisi watanzania uwa tuna huruma sana au sijui ni utu na kuaminiana kupita kiasi?
Kwanza ni kosa kutuma au kupokea pesa za mtu usiye mjua,laini yako pia ni akaunti ya kutunza fedha,hivyo usiruhusu kutumiwa au kutuma fedha usizozijua,inaweza kukuingiza matatizoni endapo zitakua fedha chafu.

Pili usikubali kumpa mtu usiemfahamu simu yako atumie kuwasiliana na mtu ambae pia hata wewe aumjui,watapanga uhalifu ama jambo lingine kupitia simu yako mwisho wa siku unabananishwa wewe kwasababu namba yako ndo imetumika.

Kwa mtazamo wa kawaida unaweza ona kama Vodacom kama sio,lakini pengine wanasimama kwenye utaratibu ambao upo.
Uyo dada uwenda akawa yeye ndio mkosaji mkuu.
 
Back
Top Bottom