Msaada Tofauti ya RCA cable na HDMI cable

Msaada Tofauti ya RCA cable na HDMI cable

ESPRESSO COFFEE

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2014
Posts
6,146
Reaction score
7,676
Habarini.....Wakuu nina TV star X inch 32,nina sabufa Pinetech,nina king'amuzi cha Dstv......sasa nataka niunganishe hivi vitu 3 kwa pamoja means niwe naona kwenye TV kwa king'amuzi changu na Sauti itoke kwenye Sabufa msaada nafanyaje

Nashindwa kuelewa kama NIKITUMIA HDMI cable nitaunganisha vipi sabufa yangu? Na faida za HDMI ni nini?

Kama nikitumia njia 3 (RCA CABLE) kipi nitakikosa nisipo tumia HDMI nataka kuunga na sabufa msaada Tafadhari
20170204_190142.jpg
20170204_190334.jpg
 
HDMI cable inafanya picha kuwa clear zaidi, utachomeka kwenye tv na king'amuzi, kuhusu suala la sauti isikike kupitia sabufa, inabidi uwe na cable sijui jina lake lakini inakuwa na pin kubwa kama pin za headphone upande mmoja na upande wa pili inakuwa na pin mbili, kwahiyo izo pin mbili utachomeka kwenye sabufa na iyo pin mfano wa head kuna pot kwenye iyo flat pembeni utachomeka, hapo utakuwa umemaliza. Uliza utakapokwama, pia ukifanikiwa lete mrejesho.
 
kama tv yako ina earphone ndio njia raisi zaidi ni kuchomeka tu waya wa sabufa na sauti ukiwa unaangalia tv utaipata.
 
HDMI cable inafanya picha kuwa clear zaidi, utachomeka kwenye tv na king'amuzi, kuhusu suala la sauti isikike kupitia sabufa, inabidi uwe na cable sijui jina lake lakini inakuwa na pin kubwa kama pin za headphone upande mmoja na upande wa pili inakuwa na pin mbili, kwahiyo izo pin mbili utachomeka kwenye sabufa na iyo pin mfano wa head kuna pot kwenye iyo flat pembeni utachomeka, hapo utakuwa umemaliza. Uliza utakapokwama, pia ukifanikiwa lete mrejesho.
Nafikiri hii ndo njia rahisi zaidi ngoja nijaribu
 
Tazama matundu ya sauti ya tv yako ni njia mbili yaani white na red pins au ni njia moja yaani inatumia headphones. Kama ni njia mbili unga dstv kwenda kwenye tv kwa hdmi ,kisha toa nyaya toka kwenye tv za sauti (tazama sehemu zimeandikwa out) *tazama kama ni ya nyaya mbili zichomeke mbili kama ni ya headphone ichomeke* na zipeleke kwenye sub hoofer pin ziingie kwenye input side .
Basi enjoy
 
HDMI cable inafanya picha kuwa clear zaidi, utachomeka kwenye tv na king'amuzi, kuhusu suala la sauti isikike kupitia sabufa, inabidi uwe na cable sijui jina lake lakini inakuwa na pin kubwa kama pin za headphone upande mmoja na upande wa pili inakuwa na pin mbili, kwahiyo izo pin mbili utachomeka kwenye sabufa na iyo pin mfano wa head kuna pot kwenye iyo flat pembeni utachomeka, hapo utakuwa umemaliza. Uliza utakapokwama, pia ukifanikiwa lete mrejesho.
done!!
 
HDMI inaongeza uangafu wa picha Mkuu na NI cable moja tu Ambayo hufanya transmission ya Sauti na Video, RCA hizo zipo tatu Yellow wa picha, Red na white za sauti quality ya RCA sio ya juu kama HDMI,

Back to connection Kama Kama TV yako ina support Slot ya earphone au kingamuzi nunua Y cable Uta plug kwenye Tv na inakuwa na output mbili utapeleka kwenye Subwoofer au Kama Hamna earphone port, Chukua hizo Av or RCA cable mbili geuza Tv angalia palipoandikwa Output chomeka pa red na white halafu peleka katika subwoofer upande wa input Na HDMi itoe from TV to kingamuzi
 
Tazama matundu ya sauti ya tv yako ni njia mbili yaani white na red pins au ni njia moja yaani inatumia headphones. Kama ni njia mbili unga dstv kwenda kwenye tv kwa hdmi ,kisha toa nyaya toka kwenye tv za sauti (tazama sehemu zimeandikwa out) *tazama kama ni ya nyaya mbili zichomeke mbili kama ni ya headphone ichomeke* na zipeleke kwenye sub hoofer pin ziingie kwenye input side .
Basi enjoy
Kwenye DSTV kutakuwa na HDMI tuu si ndio hizo white na red zipo
 
Kwenye DSTV kutakuwa na HDMI tuu si ndio hizo white na red zipo
Hdmi pekee ndio itaconnect king'amuzi na Tv ,kisha hizo white na red utatumia kuconnect Tv na sub woofer yaani hdmi itachukua picha na sauti toka kwenye dstv na kupeleka kwenye tv,kisha white na red zitatoa sauti toka kwenye Tv iende kwenye sub woofer
 
Wakuu hebu niwekeni sawa kuhusu HDMI
Mwanzo nilikuwa natumia cable za kawaida(RCA CABLE) lakini bado picha hazipo kwenye clear ile ya HD Yenyewe msaada kwa mtaalam wa mambo haya
 
We have the same case! Majuzi nimenunua LG Tv nikaunganisha na H/Theatre ikagoma kutoa sauti mpaka nikadhani huenda nimeuziwa Tv mbovu.
 
We have the same case! Majuzi nimenunua LG Tv nikaunganisha na H/Theatre ikagoma kutoa sauti mpaka nikadhani huenda nimeuziwa Tv mbovu.
Hiyo home theatre haina hdmi. Mbona nyingi zina hdmi.
Vip pia ina RCA.
 
Sio mbaya na mimi nikapata msaada hapa ni kwamba juzi kati nliingia k/koo nlikua natafuta tv Turner ili niweze kuconnect laptop yangu kuwa tv ila skufanikiwa kupata kwa ambaye alishafanya connect ion ya namna hii naomba anielkeze pakupatia hiyo tv Turner
 
Wakuu hebu niwekeni sawa kuhusu HDMI
Mwanzo nilikuwa natumia cable za kawaida(RCA CABLE) lakini bado picha hazipo kwenye clear ile ya HD Yenyewe msaada kwa mtaalam wa mambo haya
Japo ni kweli HDMI inatoa picha clear but ukubwa wa resolution ya TV yko pia unahusika. TV zote ambazo zina resolution chini ya 1920 X 1080P hta utumie HDMI huwez faidi uhondo.

Ukitumia HDMI kwa TV ambayo ni UHD ndo utafaidi uhondo! Unaweza ukahesabu had nywele za mtu anayekuwa displayed
 
Japo ni kweli HDMI inatoa picha clear but ukubwa wa resolution ya TV yko pia unahusika. TV zote ambazo zina resolution chini ya 1920 X 1080P hta utumie HDMI huwez faidi uhondo.

Ukitumia HDMI kwa TV ambayo ni UHD ndo utafaidi uhondo! Unaweza ukahesabu had nywele za mtu anayekuwa displayed
Mkuu ina Resolution: 1366x768 je naweza pata picha clear?
 
Back
Top Bottom