Msaada Tafadhali: Nahitaji kazi ya kujitolea kwenye Radio

Limbula

Member
Feb 23, 2016
5
1
Mimi ni kijana ninayeishi ubungo dsm.Nimehitimu chuo kikuu miaka kadhaa nyuma katika moja ya vyuo vikuu hapa hapa nchini.Muda mrefu nimekuwa nikivutiwa na kupenda sana kufanya kazi kwenye radio kwa kuwa navutiwa sana na vipindi vya masuala ya kijamii.

Kwa kutimiza kiu yangu nikatafuta nafasi ya kufanya vipindi vya uchambuzi wa masuala ya kijamii kwenye moja ya radio kubwa lakini inabidi mpaka ualikwe kutokana na mada husika ya kipindi au maudhui ya siku hiyo.Pia wakati nasoma kidato cha tano niliwahi kufanya kipindi kwenye moja ya radio jijini mwanza kilikuwa kipindi kinachohusu masuala ya vijana hivyo nilikuwa nafanya uchambuzi kwa masuala hayo ya vijana.

Kwa sasa kuna sehemu nafanya kazi lakini kiu juu ya kufanya kazi kwenye radio inaongezeka kila kukicha.Hivyo nipo tayari hata kwa KUJITOLEA ili niweze kujifunza vitu muhimu.

Wanajopo mwenye nafasi nipo tayari, mwenye kunielekeza pa kuanzia pia nipo tayari.

PM kwa mawasiliano zaid.
 
safi sana unaweza muona THE KING OF SOCIAL MEDIA Mr. LE MUTUZI yuko katika mbio za kufungua kituo cha redio na Tv.

swissme
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom