Msaada: Swali la Ufahamu

Faana

JF-Expert Member
Dec 12, 2011
31,659
32,964

Dan 6:16 SUV​

Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akanena, akamwambia Danieli, Mungu wako unayemtumikia daima, yeye atakuponya.

Luka 16:19-31 BHN​

“Palikuwa na mtu mmoja tajiri, ambaye alikuwa anavaa mavazi ya bei kubwa sana ya rangi ya zambarau na ya kitani safi, na kufanya sherehe kila siku. Na, mlangoni pa huyo tajiri kulikuwa na maskini mmoja jina lake Lazaro, ambaye alikuwa amejaa vidonda. Lazaro alitamani kupewa makombo yaliyoanguka kutoka mezani pa huyo tajiri; na zaidi ya hayo, mbwa walikuwa wanakuja na kuramba vidonda vyake! “Basi, huyo maskini akafa, nao malaika wakamchukua, wakamweka karibu na Abrahamu. Na yule tajiri pia akafa, akazikwa. Huyo tajiri, akiwa na mateso makali huko kuzimu, akainua macho yake, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro karibu naye. Basi, akaita kwa sauti: ‘Babu Abrahamu, nionee huruma; umtume Lazaro angalau achovye ncha ya kidole chake katika maji, auburudishe ulimi wangu, maana ninateseka mno katika moto huu.’ Lakini Abrahamu akamjibu: ‘Kumbuka mwanangu kwamba ulipokea mema yako katika maisha, naye Lazaro akapokea mabaya. Sasa lakini, yeye anatulizwa, nawe unateswa. Licha ya hayo, kati yetu na nyinyi kumewekwa shimo kubwa, ili wanaotaka kuja kwenu kutoka huku wasiweze, na wanaotaka kutoka kwenu kuja kwetu wasiweze.’ Huyo aliyekuwa tajiri akasema: ‘Basi babu, nakuomba umtume aende nyumbani kwa baba yangu, maana ninao ndugu watano, ili awaonye wasije wakaja huku kwenye mateso.’ Lakini Abrahamu akamwambia: ‘Ndugu zako wanao Mose na manabii; waache wawasikilize hao.’ Lakini yeye akasema: ‘Sivyo babu Abrahamu, ila kama mtu atafufuka kutoka kwa wafu na kuwaendea, watatubu.’ Naye Abrahamu akasema: ‘Kama hawawasikilizi Mose na manabii, hawatajali hata kama mtu angefufuka kutoka kwa wafu.’”

Yohane 11:1-25 BHN​

Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake. Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa). Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!” Yesu aliposikia hivyo, akasema, “Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe.” Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro. Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi. Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Twendeni tena Yudea!” Wanafunzi wakamwambia, “Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?” Yesu akajibu, “Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu. Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.” Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.” Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.” Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro. Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa; lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.” Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!” Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne. Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu, umbali upatao kilomita tatu. Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao. Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani. Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa! Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.” Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.” Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.” Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uhai. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi
BHN: Biblia Habari Njema

Maswali:
  1. Hao simba waliishia wapi hata leo wasiwepo, tunashuhudia watu kutoka nchi hizo kuja kutazama wanyama Afrika wakieemo hao simba
  2. Huyu Lazaro alikufa mara mbili? Ilikuwaje akawepo wakati wa Abraham (Agano la Kale) na wakati wa Yesu (Agano Jipya)?
  3. Je kwanini hivi vitabu vya imani visiwe vinapewa ithibati na BAKITA ili kuilinda lugha dhidi ya kupoteza maana yake, mfano; humu kwenye Biblia limetumika neno ramba ambalo katika Kamusii ya BAKITA linatambuliwa kama lamba, binafsi naiona hii siyo afya katika ustawi wa lugha yetu adhimu.
 
Najibu swli namba Moja.
Hao simba walikuwepo mwaka 605K.K na hapo ni mesopotamia 70 kilometer toka mji wa Baghdad Iraq.
Nchi ilikuwa ikiitwa Babeli (machafuko/Uovu)
Achana na ile ya Nimrod. Hii ni Neo Babilonian empire. Chini ya utawala wa Nebukadreza .
Hao simba waliuawa na wamedi na waajemi wakati wa Dario.

Miaka ijayo Simba wataisha huku kwetu. Tutakua tunaenda quatar kuona twiga waliopanda Ndege.
 
Ufufuo wa Lazaro ni uthibitisho kua wafu hawajui lolote pia ukifa unakua usingizini.. hauendi kuchomwa moto kuzimu kama dini fulani zinazofundisha
 
Najibu swli namba Moja.
Hao simba walikuwepo mwaka 605K.K na hapo ni mesopotamia 70 kilometer toka mji wa Baghdad Iraq.
Nchi ilikuwa ikiitwa Babeli (machafuko/Uovu)
Achana na ile ya Nimrod. Hii ni Neo Babilonian empire. Chini ya utawala wa Nebukadreza .
Hao simba waliuawa na wamedi na waajemi wakati wa Dario.

Miaka ijayo Simba wataisha huku kwetu. Tutakua tunaenda quatar kuona twiga waliopanda Ndege.
Asante sana Mkuu, nimekuelewa vema sana, ubarikiwe mno
 
Ufufuo wa Lazaro ni uthibitisho kua wafu hawajui lolote pia ukifa unakua usingizini.. hauendi kuchomwa moto kuzimu kama dini fulani zinazofundisha
Tunaambiwa Lazaro alikufa na akaenda kukaa mikononi mwa Abrahamu ikimaanisha ilikuwa BC, na baadaye alikuja kuwa rafiki yake Yesu na alipokufa akafufuliwa na Yesu (comfusion)
 
Najibu swli namba Moja.
Hao simba walikuwepo mwaka 605K.K na hapo ni mesopotamia 70 kilometer toka mji wa Baghdad Iraq.
Nchi ilikuwa ikiitwa Babeli (machafuko/Uovu)
Achana na ile ya Nimrod. Hii ni Neo Babilonian empire. Chini ya utawala wa Nebukadreza .
Hao simba waliuawa na wamedi na waajemi wakati wa Dario.

Miaka ijayo Simba wataisha huku kwetu. Tutakua tunaenda quatar kuona twiga waliopanda Ndege.
Mods: Active

Nawezaje ku star, flag au bookmark hili jibu?
 
Kuna vitu naona unachanganya pengine ni kwa sababu hujatuliza kichwa...

Fuatilia hapa:
1. Ibrahim/Abraham aliishi kale, akafa na kutokana na utakatifu wake akaenda peponi...

2. Mathayo, Marko, Luka na Yohana ni vitabu vinavyoelezea maisha ya Yesu, waandishi wakiwa ni tofauti na simulizi nyinginezo ambazo kotekote zinatajwa kwa namna au uandishi tofauti.

3. Hivyo, Lazaro anayetajwa kwenye vitabu hivyo vinne ni Lazaro yuleyule isipokuwa namna ya simulizi ndiyo inatofautiana, ni sawa na mtu mmoja aandike "Rais Samia aenda Dubai" na mwingine aandike "Dubai yajiandaa kumpokea Rais Samia".

4. Katika kitabu cha Luka kinataja kufa kwa Lazaro, na nini kiliendelea baada ya kifo chake (yaani akiwa peponi), ndipo hapo anapotajwa Ibrahimu ambaye hapo kale alipokufa naye alienda peponi na sasa kakutana na Lazaro huko peponi.

5. Wakati huo huo katika kitabu cha Yohana, kisa cha Lazaro kinaelezwa lakini kinataja mandhari ya huku duniani, kitu gani kiliendelea baada ya kuwa mfu kwa siku nne.
 
Hao Lazaro ni wawili tofauti. Mbona wapo wengine wanaofanana majina mf. Yohana, Yuda, Mariam, Yusuph n.k

3. Hivyo, Lazaro anayetajwa kwenye vitabu hivyo vinne ni Lazaro yuleyule isipokuwa namna ya simulizi ndiyo inatofautiana, ni sawa na mtu mmoja aandike "Rais Samia aenda Dubai" na mwingine aandike "Dubai yajiandaa kumpokea Rais Samia".

N
4. Katika kitabu cha Luka kinataja kufa kwa Lazaro, na nini kiliendelea baada ya kifo chake (yaani akiwa peponi), ndipo hapo anapotajwa Ibrahimu ambaye hapo kale alipokufa naye alienda peponi na sasa kakutana na Lazaro huko peponi.
Asante Mkuu

You mean baada ya Lazaro kufa na kufufuliwa na Yesu, baadaye alipokufa wakati Yesu hayupo duniani ndipo ikisimuliwa maisha aliyoishi huko peponi, na je huyo mwandishi wa hayo maisha ya Lazaro peponi aliupata wapi huo ushuhuda?
 
Abraham alikutana nae peponi

Biblia zinachapishwa na watu tofauti tofauti hayo ni makosa madogo madogo ya uchapishaji tu..
Hata Wana sayansi na Wana falsafa wanachapia
Huyu mwandishi alizipataje habari za maisha ya Lazaro, Abraham na tajiri huko peponi?

Au Laazaro alisimulia baada ya kufufuliwa na Yesu?
 
N

Asante Mkuu

You mean baada ya Lazaro kufa na kufufuliwa na Yesu, baadaye alipokufa wakati Yesu hayupo duniani ndipo ikisimuliwa maisha aliyoishi huko peponi, na je huyo mwandishi wa hayo maisha ya Lazaro peponi aliupata wapi huo ushuhuda?

Lazaro alikufa na kufufuliwa na Yesu Kristo kabla angali Yesu yupo duniani...yaani ile miaka wakati Yesu Kristo akifanya miujiza yake duniani, ndipo wakati huo huo huyo Lazaro alipofikwa na mauti na akapata kufufuliwa

Waandishi wa maisha ya Yesu ni watu waliokuwa na Yesu kwa wakati huo, mfano Luka alikuwa tabibu
 
Lazaro alikufa na kufufuliwa na Yesu Kristo kabla angali Yesu yupo duniani...yaani ile miaka wakati Yesu Kristo akifanya miujiza yake duniani, ndipo wakati huo huo huyo Lazaro alipofikwa na mauti na akapata kufufuliwa

Waandishi wa maisha ya Yesu ni watu waliokuwa na Yesu kwa wakati huo, mfano Luka alikuwa tabibu
Ningetamani kujua connection ya kifo cha Lazaro na kufufuliwa kwake na kufa kwa lazaro na kukaa mikononi mwa Abraham (flow ya habari hii kwa ujumla ikibidi mpaka kufahamu nani alileta ushuhuda wa yaliyojiri huko walikokutana Abraham na Lazaro)
 
Back
Top Bottom