Habari ya jioni wana jf. Naomba ushauri. Naishi kwa uncle ambaye ni kama baba yangu kanisomesha toka primary mpaka chuo first year namshukuru kwa hilo sana. Nimeishi nae kutoka 2006 mpaka sasa miezi ya likizo. Uncle hana tatizo lakini kuanzia shangazi, ndugu yake shangazi na wasichana wake wa kazi wamenifanya nichoke kabisa kuishi pale. Nimemwambia uncle kuwa maisha ya pale kwake yamenishinda nataka nikaishi sehemu nyingine tofauti na pale. Kanijibu mtoto wa kike haachi wazazi wake na kupanga pia dharau.