Kupambana na nyani sio kazi rahisi kwa sababu wana akili kama binadamu kwa hiyo majibu rahisi hayawezi kufanya kazi. Nakumbuka miaka ya nyuma kule Uganda kaskazini kuna mkulima mmoja ambaye alilima nahindi na nyani wakuwa wanakula kila siku. Siku moja aliweka ulinzi akiwa na upinde na mishale. Nyani wakaja kama kawaida yao wakaingia shambani kula mahindi yeye akiwa amejificha sehemu tayari kwa mashambulizi. Basi akavuta upinde na kurusha mshale uliompata barabara nyani mmoja na kumuua.
Wenzake walikimbia kisha baadaye wakarudi kubeba nwili wa "marehemu" na kwenda nao wanakojua wao "kwa ajii ya mazishi". Walikuwa wakiomboleza kama watu.
Basi hao nyani wenye hasira walimjua huyo mkulima na nyumbani kwake walipajua! Chezea nyani weweeee! Wakaitisha kikao cha dharura kutafakari hatua gani wachukue dhidi ya huyo mkulima. Cha ajabu pamoja na hasira walizokuwa nazo walisubiri muda muafaka wa kulipiza kisasi. Bila kukosea walikuja nyani kama 30 hivi usiku wa manane nyumbani kwa huyo mkulima wajavunja mlango na kuingia ndani. Walimtoa kitandani mzega mzega hadi nje wakamchana tumbo na kutoa utumbo nje! Walipohakikisha amekufa wakaondoka zao. Sasa ona kwamba walijua kuwa usiku mnene hangepata msaada wa majirani kwa hiyo wakachagua muda huo kufanya mashambulizi!
Mimi ninachoshauri ni kubadilisha mazao na kupanda vitu ambavyo nyani hawana shida navyo.