Msaada: Nyani wanakula kuku wangu

Msaada: Nyani wanakula kuku wangu

Mimi shambani kwangu nafuga kuku na nalima matikiti na jirani yangu analima mpunga , kuna nyani wanakuja wanaanza na mpunga (wali) then wanakuja kwenye kuku alafu wanamalizia na kuyala matikiti. ..yaani full menu ya hotel na nimewapiga na bunduki baada ya siku 3 wanarudi tena kupiga menu yao... dawa kuwatega na wao kuwala tu.
Aisee nimecheka mpaka machozi yamenitoka.. Hao nyani ni wa mwendokasi
 
Kupambana na nyani sio kazi rahisi kwa sababu wana akili kama binadamu kwa hiyo majibu rahisi hayawezi kufanya kazi. Nakumbuka miaka ya nyuma kule Uganda kaskazini kuna mkulima mmoja ambaye alilima nahindi na nyani wakuwa wanakula kila siku. Siku moja aliweka ulinzi akiwa na upinde na mishale. Nyani wakaja kama kawaida yao wakaingia shambani kula mahindi yeye akiwa amejificha sehemu tayari kwa mashambulizi. Basi akavuta upinde na kurusha mshale uliompata barabara nyani mmoja na kumuua.
Wenzake walikimbia kisha baadaye wakarudi kubeba nwili wa "marehemu" na kwenda nao wanakojua wao "kwa ajii ya mazishi". Walikuwa wakiomboleza kama watu.
Basi hao nyani wenye hasira walimjua huyo mkulima na nyumbani kwake walipajua! Chezea nyani weweeee! Wakaitisha kikao cha dharura kutafakari hatua gani wachukue dhidi ya huyo mkulima. Cha ajabu pamoja na hasira walizokuwa nazo walisubiri muda muafaka wa kulipiza kisasi. Bila kukosea walikuja nyani kama 30 hivi usiku wa manane nyumbani kwa huyo mkulima wajavunja mlango na kuingia ndani. Walimtoa kitandani mzega mzega hadi nje wakamchana tumbo na kutoa utumbo nje! Walipohakikisha amekufa wakaondoka zao. Sasa ona kwamba walijua kuwa usiku mnene hangepata msaada wa majirani kwa hiyo wakachagua muda huo kufanya mashambulizi!
Mimi ninachoshauri ni kubadilisha mazao na kupanda vitu ambavyo nyani hawana shida navyo.


mhhhhhh hii chai imezidi
 
Kupambana na nyani sio kazi rahisi kwa sababu wana akili kama binadamu kwa hiyo majibu rahisi hayawezi kufanya kazi. Nakumbuka miaka ya nyuma kule Uganda kaskazini kuna mkulima mmoja ambaye alilima nahindi na nyani wakuwa wanakula kila siku. Siku moja aliweka ulinzi akiwa na upinde na mishale. Nyani wakaja kama kawaida yao wakaingia shambani kula mahindi yeye akiwa amejificha sehemu tayari kwa mashambulizi. Basi akavuta upinde na kurusha mshale uliompata barabara nyani mmoja na kumuua.
Wenzake walikimbia kisha baadaye wakarudi kubeba nwili wa "marehemu" na kwenda nao wanakojua wao "kwa ajii ya mazishi". Walikuwa wakiomboleza kama watu.
Basi hao nyani wenye hasira walimjua huyo mkulima na nyumbani kwake walipajua! Chezea nyani weweeee! Wakaitisha kikao cha dharura kutafakari hatua gani wachukue dhidi ya huyo mkulima. Cha ajabu pamoja na hasira walizokuwa nazo walisubiri muda muafaka wa kulipiza kisasi. Bila kukosea walikuja nyani kama 30 hivi usiku wa manane nyumbani kwa huyo mkulima wajavunja mlango na kuingia ndani. Walimtoa kitandani mzega mzega hadi nje wakamchana tumbo na kutoa utumbo nje! Walipohakikisha amekufa wakaondoka zao. Sasa ona kwamba walijua kuwa usiku mnene hangepata msaada wa majirani kwa hiyo wakachagua muda huo kufanya mashambulizi!
Mimi ninachoshauri ni kubadilisha mazao na kupanda vitu ambavyo nyani hawana shida navyo.
Hadithi za kitambo kile kipindi cha analogy sasa hivi watu wako digital kaka!!! acha fiksii
 
Msichukulie easy jamani nyani hao ni kama elf 10 wakivamia hata niwafukize mm hawaelewi hasa mwanamke ni shamba ninakofugia nyani wana uzito na akili kama watu mpk ugali wanaipua alafu ukiwaua unashtakiwa Mummy!mpka natamani niuze shamba ninunue kwingne lkn maskini hapatakuwa karibu na kazin!
Chukua ushauri wa post #5, acha maneno Mengi!
 
Mtafute mlinzi monkey ungabure akulindie hao kuku wako..
c6a7c10ff823e982b55ececb78102d39.jpg
Kumbe Ualibino hadi kwa wanyama !!! Au ndiye Nyani Ngabu
 
Mimi shambani kwangu nafuga kuku na nalima matikiti na jirani yangu analima mpunga , kuna nyani wanakuja wanaanza na mpunga (wali) then wanakuja kwenye kuku alafu wanamalizia na kuyala matikiti. ..yaani full menu ya hotel na nimewapiga na bunduki baada ya siku 3 wanarudi tena kupiga menu yao... dawa kuwatega na wao kuwala tu.
😀😀😀😀😀😀😀😀😀
 
Fuga mijibwa kama mitatu hivi.. Alaf toa taarifa waje wagongwe risasi tu... Au nunua kiupinde na mshale. Atakeingia kwa 18 ni mishale mvua yan
 
Nyani nawafahamu vizuri sana.ni wasumbufu hatari.jaribu kununua matunda mbali mbali wanayopenda.

Ndizi, ,tikiti, mihogo, viazi.

Kisha weka sumu au sindano wawekee wale wakifa watapotea hapo.
 
Kamata nyani mmoja, usimuue kisha kampake rangi ya ku spray nyekundu na nyeupe (kama jezi ya simba) mwili mzima, akisha kauka mfungulie akimbilie wenzake. Watakuwa nao wanamkimbia hivyo wanaweza kukimbia mpka mikumi toka bagamoyo.
 
Back
Top Bottom