Yanakukubalisha kwamba kinachoonekana ndicho kweli kinatokea na kinatokea kwa sababu ya uchawi.
It is like seeing a mirage in a desert, you see an oasis where there is none, and when you get there and see there is none, you think it is some supernatural forces.While it is a perfectly natural phenomena.
Nimegundua mambo juu ya kile unachofikiri kuhusu ulimwengu wa kiroho.
1. Inaonekana una namna flani ambavyo ungetaka uchawi uwe ila kwa bahati mbaya vimbwanga vyoote ambavyo watu wanasema ni uchawi/shirki havitoshi katika tafsiri uliyonayo. Yaani watu wanachoita uchawi we unaita extraodinary phenomena n.k.! Neno uchawi hulitaki kabisa. Sijui we ungetaka kitokee kitugani ili uite uchawi. Ni sawa na mtu ambaye hataki kusikia kuna Mungu ila ukimwambia supernatural force anakwambia hapo sawa kwasababu kuna namna ambavyo anataka Mungu awe na si hivyo alivyo huyo Mungu anayeabudiwa na wengi.
2. Kuamini uchawi upo si kukata tamaa ya kujua theory-behind ya hiyo teknolojia. Ni kukubali tu kuwa ni jambo lisilo la kawaida. Something mysterious or a science which is intellectualy complexed. Ila laweza kufundishika na kueleweka.
Na hicho kilichopelekea mawazo kunipa tafsiri hiyo ni kipi?
Uchawi ni nini?
Ulivyoandika hapo ni kama umekubali kwamba jambo usilolijua ni uchawi.
Utajuaje kwamba ni uchawi wakati hujalijua?
Arthur C. Clarke alisema "any advanced technology is indistinguishable from magic".
Mababu zetu walioishi kabla ya usafiri wa ndege wangeona ndege inabeba watu na inaruka leo wangesema uchawi, wakati ni physics tu.
Utajuaje kwamba unachofikiri uchawi wewe leo si kitu kinachoweza kuelezewa vizuri tu bila ya kuhitaji habari ya uchawi?
Ujinga.
Hehehehe. Nakubaliana na Arthur.
Kuna mwanasaikolojia mmoja wa Tanzania aliitwa Munga Tehenan na alikuwa Mhariri wa gazeti la Jitambue. Huyu jamaa alikuwa anafundisha hata kumuita mwanamke unayempenda kwa mazingara, unachukua unyoya wa tausi...blah blah, akawa anawasihi wanafunzi wake wajaribu tu kuona kama mambo hayo yanawezekana. Kujua na kujaribu na kufanya kitu kama hicho hakufuti maana ya kuwa ni uchawi. Kwahiyo nakiri kuwa kuna jambo ambalo leo naliona ni uchawi na kesho sitoliona hivyo lakini teknolojia kama hiyo ya kumvuta mwanamke ambaye hata hakujui kwa kuchukua unyoya wa tausi, ukaweke kwenye maji, saa flani, n.k. Halafu kesho huyo mwanamke anakuja from no where huo ni uchawi tu.
Hehehe ishakuwa ujinga tena!
Na kuna mtu kenya ameamka asubuhi na kujikuta hana sehemu zake za siri,sasa sijui nao ni ujinga au vp.
HeyKuna ishu imenikumba juzi kati wakati nilipokuwa nafuatilia shamba la mzee wangu kwa ajili ya kulifanyia mchakato wa kulisafisha.
Kufika huko nimekutana na kitu tofauti na matarajio yangu.Yaani shamba limemegwa na mama mmoja na taarifa zikadai hajauziwa ila amekuja kuvamia.
Nilichokifanya nilimchukua anko wangu tukaanza kumtafuta huyo mama bahati nzuri tulikutana naye njiani siku moja.
Anko alipomuhoji kwanini amevamia eneo sio lake hakutujibu badala yake alimrushia anko jini akabaki anagalagala chini na yule mama akaondoka zake mpaka sasa anko kapooza na shamba limemegwa na nikiangalia msimu wa kilimo umekaribia.Je nifanyeje wadau ili niweze pata haki yangu.
N.B
Shamba lina hati zote ila uchawi tu ndio unanitisha.
Mtu ana supernatural gani?
Wapi umepata habari hii?
Comprehension please!
Ujinga ni neno tu. Sisi wote ni wajinga, kwa jambo moja au jingine. Kitu usipokijua una ujinga nacho. Ignorance.
Amejikuta hana sehemu za siri kivipi? Imethibitishwa vipi?
Siku hizi stories kibao watu wanataka kuuza magazeti.
Hii habari kabla ya kuimeza nzimanzima umeithibitisha vipi?
Unajuaje kwamba alikuwa nazo kabla mpaka leo useme leo amejikuta hana sehemu za siri, hata kama kweli leo hana sehemu zake za siri?
Hata kama alikuwa nazo jana na leo hana, is that enough to say "this is uchawi"?. How do you get to this conclusion before knowing what happenned?
Ujinga ni neno tu. Sisi wote ni wajinga, kwa jambo moja au jingine. Kitu usipokijua una ujinga nacho. Ignorance.
Amejikuta hana sehemu za siri kivipi? Imethibitishwa vipi?
Siku hizi stories kibao watu wanataka kuuza magazeti.
Hii habari kabla ya kuimeza nzimanzima umeithibitisha vipi?
Unajuaje kwamba alikuwa nazo kabla mpaka leo useme leo amejikuta hana sehemu za siri, hata kama kweli leo hana sehemu zake za siri?
Hata kama alikuwa nazo jana na leo hana, is that enough to say "this is uchawi"?. How do you get to this conclusion before knowing what happenned?
Usipende kuamini reference saana wakati mifano ipo kwako wewe
Mifano ya nguvu asili kutoka kwako ni kuhisi kitu fulani kitatokea then kinatokea kweli...,
Umeota umeona pesa nyingi then baada ya siku kadhaa unafanikiwa katika hilo
Kujua ni vp mtu anafanya hadi inaonekana kweli anakata kichwa cha mtu haifanyi iwe kitendo kile si cha kichawi tena.
Hapa ulichoandika ni sawa na kuandika "Kujua kwamba movies zinakuwa na dummies wanaokatwa vichwa na kufanya ionekane mtu kakatwa kichwa haifanyi kitendo kile si cha kichawi tena".
Nguvu asili ndiyo supernatural?
Hivi unaelewa hata maana ya supernatural?
Unafahamu ndoto zinaanzaanzaje na kwa nini si ajabu mtu kuota unapata pesa nyingi halafu baada ya siku nyingi ukafanikiwa katika hilo?
We unazungumzia movie?
Tusiende mbali sana mkuu kwa upeo wako super natural forces ni zipi ???
Tizama video ya jamaa aliyepotelewa na sehemu zake za siri.
http://m.youtube.com/watch?v=nH5Tq2...=&client=mv-google&hl=en-GB&gl=US