MSAADA: Nimekuwa 'addicted' sana na mitandao ya kijamii,nashindwa kujizuia

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
Wakuu habarini.

Kutokana na sarakasi , habari, matukio na vioja mbalimbali vinavyoendelea duniani hasa hapa kwetu Tanzania, nimekuwa nikitumia muda mwingi sana kufuatilia habari, matukio, mikasa, vitimbwi na sarakasi zinazoendelea kila kukicha. Yaani kuna matukio mengi yanayoibuka kila siku ya Mungu na kusambaa haraka sana kwenye mitandao ya kijamii hasa fb, Instagram, tweeter, WhatsApp, you tube na hapa JF. Nashindwa kujizuia kupitwa. Muda mwingi nataka niwe updated kwa mambo yanayotokea nchini hasa ya kisiasa.

Kuna series za matukio nyingi sana na zinagusa watu potential nchini so inabidi nipakue tu nijue nani kasema nini na wapi. Nikikaa masaa 6 bila kupekua kitu,sijisikii vzr kabisa. Huwa naanza na magazeti then naserereka taratibu fb, insta, tweeter, you tube na baadae namalizia hapa kwetu nyumbani JF.

Kuna wakati wife mpk anagomba yaani ,usiku nachelewa sana kulala na pia kazini nako ufanisi naona unapungua.


Wenzangu mnawezaje kucontrol mood na time ya kufuatilia vitu kwenye social media hasa mitandaoni?

Asanteni.
 
Huu ni ugonjwa wa wengi sana, lakini mara nyingi unatokana na uhaba wa shughuli muhimu za kufanya.

Sasa nakushangaa wewe vipo vya kukupa ubize lakini bado unayapa uzito sana matumizi ya internet.
 
Wakuu habarini.

Kutokana na sarakasi , habari, matukio na vioja mbalimbali vinavyoendelea duniani hasa hapa kwetu Tanzania, nimekuwa nikitumia muda mwingi sana kufuatilia habari, matukio, mikasa, vitimbwi na sarakasi zinazoendelea kila kukicha. Yaani kuna matukio mengi yanayoibuka kila siku ya Mungu na kusambaa haraka sana kwenye mitandao ya kijamii hasa fb, Instagram, tweeter, WhatsApp, you tube na hapa JF. Nashindwa kujizuia kupitwa. Muda mwingi nataka niwe updated kwa mambo yanayotokea nchini hasa ya kisiasa.

Kuna series za matukio nyingi sana na zinagusa watu potential nchini so inabidi nipakue tu nijue nani kasema nini na wapi. Nikikaa masaa 6 bila kupekua kitu,sijisikii vzr kabisa. Huwa naanza na magazeti then naserereka taratibu fb, insta, tweeter, you tube na baadae namalizia hapa kwetu nyumbani JF.

Kuna wakati wife mpk anagomba yaani ,usiku nachelewa sana kulala na pia kazini nako ufanisi naona unapungua.


Wenzangu mnawezaje kucontrol mood na time ya kufuatilia vitu kwenye social media hasa mitandaoni?

Asanteni.

Kwahiyo hata ukiwa unaibandua Mbunye au pengine unabanduliwa Wewe na Mkuyenge napo pia huwa unakuwa addicted na Social Media platforms Mkuu?
 
ukiwa idle na una bundle iyo c addiction ila kama una kazi unaacha unaanza kuchat unahitaji viboko na uanze kutumia kitochi
 
Siyo addicted, umekuwa mbobezi yaani professional/expert. Jipe hongera
 
Pole sana wengi wanahuo ugonjwa wa kisasa unaitwa "Don't let the train pass syndrome". Yaani unahisi unapitwa unataka ujue kinachoendelea japo hamna cha maana sio kama unafanya biashara ya hisa unafuatilia soko.

Ni tatizo na ni vyema umeligundua, hebu fikiria muda huo ungewekeza kusoma vitabu au kujifunza kitu fulani, ungekijua kwa ustadu na kuwa mbali sana.

Ukweli mchungu ni kuwa watu haswa ambao hawajafanikiwa wanapoteza muda sana kufuatilia michezo (premier league), vipindi vya tv na mitandao jamii. Waliofanikiwa wengi hawafanyi hivi wanatumia muda wao vizuri wanapata habari za maana kwenye magazeti n.k. Kwa Tz hili tatizo ni kubwa sana ndio maana kuna kila aina ya ngonjera huko mtandaoni.

Nakushauri nunua au azima kitabu cha jambo unalopenda usome na vile vile uwe unazima data.
Muda ni wa thamani sana usipoutumia vizuri utakuja kukumbuka shuka wakati kuna kucha wakati huo hata nguvu za uzalishaji huna. Ikiwa ni hobi yako kabisa basi anzisha hata 'blog' ya udaku ili upate chochote usipoteze wasaa bure kama wafanyavyo kina shilawadu.
 
Back
Top Bottom