Kwa mie ninavyo fahamu neno la kiswahili lazima lihishiwe na irabu mwishoni kama jami-i,lugh-a,jukwa-a,n.k. Lakini neno RAIS halina irabu. Je ni neno la kiswahili
Hilo ni neno la kiswahili ambalo halina asili ya kibantu, Kama sijakosea lina asili ya Kiarabu
kimaandishi hilo neno mara nyingine linaandikwa na kuwekwa i mwisho Raisi na mara nyingine linakuwa bila i kama ulivyoliandika wewe
maneno ya aina hiyo yapo mengi tu,
mfano: Marehem (Marehemu)
Maalum (Maalumu)