Wana kashikashi si mchezo. Hizo jamaa zinahitaji intergrated approach. Iko ivi, tumia njia zote maana ni sahihi. Kwanza hakikisha unawawekea mkakati kama wa miezi sita. Na kila baada ya wiki unafanya hizi njia. Kila week hakikisha unatoa vitu nje, hasa vyenye mavamizi.
Kama wamevamia kwenye makochi ama masofa, we jipange tu kununua mengne mzee baba maana ni shida. Vyumbani sasa, toa vitu nje iwe ni nguo ama stuli na meza kama zipo. Godoro, nguo, out.....loweka kwenye maji ya moto.
Fungua kitanda, peleka mbao nje. Mwagia maji ya moto yaliyowekwa ariel na mafuta ya taa. Maji yawe ya moto hasa. Hizo nguo kwa mwezi toa mara moja. Lakini hii usafi fanya kila wiki kwa miezi sita. Inshort kumaliza kunguni ni ajira isiyo na mkataba wala allowance..na pia kwa wiki zingne tumia maji ya moto na hzo dawa ulizotajiwa na wakuu hata kama kwangu hazikufanya kazi. Pole aisee.