Msaada: Ndugu yangu amepooza kuanzia kiunoni kushuka miguuni

Invigilator

JF-Expert Member
Aug 16, 2016
3,207
5,990
Wakuu Salaam,

Ndugu zangu ni mwezi wa tano sasa tangu ndugu yangu (Me) amepata tatizo la afya la kupooza kuanzia maeneo ya kiunoni hadi miguuni.

Kiuno na miguu haifanyi kazi kabisa, hawezi kufanya chochote bila kupata usaidizi,kama familia tunaumia sana maana ni kijana mdogo (20s).

Tumejaribu kutafuta tiba Muhimbili imeshindikana, vipimo vikubwa vimefanyika lakini hakuna majibu ya kuridhisha juu ya hatima ya afya yake.

Nilikuwa nawaomba,ikiwa kuna mtu ana ufahamu juu ya tiba ya tatizo hili,au ikiwa kuna mtu anamjua mtu yeyote anayetibu matatizo ya kupooza atusaidie, sisi kama wana familia inatuumiza sana.

Natanguliza shukrani, karibuni kwa ushauri na maoni.
 
Kuna mtu mmoja namjua aliwahi kupata tatizo kama hilo na alipona kwa dawa za kienyeji... Nenda kwa wataalam hasa wa kisuni utapata suluhisho.
Nashukuru sana Mkuu,baada ya kuhangaika miezi nne hospital (Muhimbili) na jopo la madaktari bingwa likathibitisha kuwa uwezo wa kurecover ni mdogo,ndio maana nikaona ni busara nilete jambo hili mbele za watu,kwenye watu wengi hakushindikani jambo,ikiwa hutajali,niunganishe na huyo mtu aliyepona ndugu pengine tunaweza kupata ABC'S.
 
Nashukuru sana Mkuu,baada ya kuhangaika miezi nne hospital (Muhimbili) na jopo la madaktari bingwa likathibitisha kuwa uwezo wa kurecover ni mdogo,ndio maana nikaona ni busara nilete jambo hili mbele za watu,kwenye watu wengi hakushindikani jambo,ikiwa hutajali,niunganishe na huyo mtu aliyepona ndugu pengine tunaweza kupata ABC'S.
Amekwambia nenda kwenye maduka ya kisunna..
 
Pole sana miezi kama miwili iliyopita Mama yangu alipata ugonjwa wa kupooza plesha ilipanda juu tiba zilizosaidia ni hospital na miti shamba pia kuna aina ya vyakula hatakiwi ale hasa jamii ya mimea inayotambaa kama kunde pia kuku asile mpaka atakapo pata afueni kuna mtu ana weza kutibu huo ugonjwa wa kupooza kwani ninapoandika hapa Mama yangu kapona kabisa na ni mzee tulijua italeta shida sababu ya umri
 
Pendeleeni sana kumchua mgonjwa kila wakati na mafuta ya mzaituni,mafuta ya nazi pia kabla viungo vyake muamfanyishe mazoezi
Tunafanya hivyo mkuu,ni mwezi wa tano sasa,kinachotutisha zaidi ni kuwa hata mabadiliko madogo hakuna,kadri siku zinavyozidi kwenda,mwili unakuwa unadhoofu zaidi,hakuugua, kalala mzima,kaamka hawezi kutembea,mwezi mmoja baada ya kugraduate.
 
Yaani hii dunia nashindwa hata kuelewa,pesa imepotea nyingi mno,hali haileti hata matumaini,tatizo halijulikani yaani basi tu,Mungu aingilie kati.
Pole mkuu huo ugonjwa msipokuwa makini mtamaliza pesa na asilimia 80 ugonjwa huo unatibiwa kwa miti shamba dawa za kunywa na kuchua
 
Back
Top Bottom