Msaada: Natafuta mkopo wa bank 20M

WENYELE

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
1,415
1,379
Wakuu,nina shamba la familia la ekari 4 lenye hati ya kimila tuliyopewa 2010 mwezi wa saba.
Kulingana na hali ya kiuchumi ya sasa,ninataka niunganishe familia yangu yenye watu wazima 6 km kikundi cha familia,tuandae business plan,katiba na tuweze kwenda bank kuomba mkopo wa shilingi miliini 20.
Nina malengo yafuatayo,baada ya kupata mkopo,
1.Kuchimba kisima cha kina kirefu
2.Kununua pamp ya maji
3.Kufunga drip irrigation system
4.Kuanza kilimo hai (organic farming) cha umwagiliaji,mazao ni
-mboga mboga
-nyanya
-Vitunguu nk
Pia tutalima chakula ikiwemo mahindi,mtama nk
Bila kusahau maharage na mazao jamii ya kunde.

Mimi ni mhitimu kutoka SUA na nilikua nafanya kazi kwenye shirika binafsi lakini naona naweza tumia fursa hii na naamini familia yangu nitaitoa,Familia yangu iko Bariadi,wilaya ya Itilima.
Bank nazowaza kupata mkopo ni CRDB na NMB kama mawazo yangu yatakubaliwa.
Kama nikipata huu mkopo,mie ni mtoto wa pili,nimeoa na kaka yangu pia kaoa,mdogo wetu wa kike naye kaolewa lakini waliachana na mme wake.
Katika familia kiwango cha elimu ni hivi
1.Baba na Mama ni la saba
2.Kaka na mke wake ni la saba
3.Mimi degree na mke wangu ni degree(mwalimu)
4.Mdogo wangu wa kike ni form 4
5.Mdogo wangu mwingine wa kike ni form four lakini amefaulu kujiunga kidato cha tano hapo badae mwezi wa saba kama sikosei.
6.Waliobaki ni wadogo wetu watatu bado ni under 18 so hawatakuwepo kwenye mambo ya kisheria lakini haki na gawiwo la kifamilia watakua wanapata hasa likielekezw8a katika gharama za shule na mahitaji yao muhimu.

Kwa kuwa kidogo mie nina uelewa wa juu kielimu,nataka niwe ndio Chief operating Manager wa familia,kuwangoza ndugu zangu na kusimamia operation zetu za familia.Baba yangu atakua mwenyekiti tu lakini atakua na maamuzi katika mikakati ya kufamilia na kuamua kesi ndogo ndogo za kufamilia punde zikitokea,lakini mambo ya biashara,kusimamia marejesho ya mkopo na uwajibikaji mie nitajitwika mzigo huu.Naamini baada ya miaka 5-10 nitakua nimemaliza kulipa mkopo na faida juu.

Naomba ushauri wa kisheria,kiuchumu,kijamii na kimawazo,je hili wazo langu linaweza likafanikiwa? Kma ndio nifanye nini ili nipate mkopo haraka? Kama hapana nirekebishe wapi ili nitimize lengo hili?

Kama wazo langu ni zuri naomba mnielekeze taratibu za kufauta nipate mkopo,lakini kabla ya hapo naomba mtu wakuniandalia project plan na business plan,nitahitaji pia mwanasheria wa kuniandalia katiba na partnership deed
Nitashukru sana,mimi ni mtaalam wa usindikaji wa mazao ya chakula km na wewe unahitaji kiwanda cha kusindika chakula cha binadam nitafute tu nikusaidie,nikuandalie kila kitu ikieemo kusajiriwa na taasisi za kiserikali TBS,TFDA,OSHA etc
Asanteni wakuu,pia unaweza ukanifuata PM kwa kunishauri zaidi
 
Wazo zuri sana,lakini kwa hali iliyopo kwenye taasisi za kifedha kwasasa sina uhakika wa moja kwa moja juu ya kupatiwa mkopo huo. Kwa ushauri wangu ungeenda tawi la bank mojawapo lililo karibu nawe uone watasemaje. Kwasababu mfumo umebadirika sana na bank nyingi walisitisha mikopo kwa kipindi fulani.
 
Wazo zuri sana,lakini kwa hali iliyopo kwenye taasisi za kifedha kwasasa sina ihakika wa moja kwa moja juu ya kupatiwa mkopo huo. Kwa ushauri wangu ungeenda tawi la bank mojawapo lililo karibu nawe uone watasemaje. Kwasababu mfumo umebadirika sana na bank nyingi walisitisha mikopo kwa kipindi fulani.
Asante kwa ushauri kaka,vipi kabla ya kwenda bank nifanyaje kwanza ili nikienda waweze kunielewa? Kumbuka nataka kuchimba kisima cha kina kirefu sana ili nisioate shida ya maji
 
Nina heka nne hapo bariadi matongo.changamoto ni kisima tu.nikipata nimetajirika teyari
 
Watakababaisha tu.. Bank zetu wala hazisomi hizo Business Plan na wala hawazihitaji hasahasa kama biashara yenyewe ni mpya..

Pia kabla ya kupewa pesa ni lazima uwe na Leseni ya biashara uifanyayo na TIN Number..
 
Watakababaisha tu.. Bank zetu wala hazisomi hizo Business Plan na wala hawazihitaji hasahasa kama biashara yenyewe ni mpya..

Pia kabla ya kupewa pesa ni lazima uwe na Leseni ya biashara uifanyayo na TIN Number..
Wanahitaji nini hasa? Maana dhamana nitaweka hilo hilo shamba
 
Wakuu,nina shamba la familia la ekari 4 lenye hati ya kimila tuliyopewa 2010 mwezi wa saba.
Kulingana na hali ya kiuchumi ya sasa,ninataka niunganishe familia yangu yenye watu wazima 6 km kikundi cha familia,tuandae business plan,katiba na tuweze kwenda bank kuomba mkopo wa shilingi miliini 20.
Nina malengo yafuatayo,baada ya kupata mkopo,
1.Kuchimba kisima cha kina kirefu
2.Kununua pamp ya maji
3.Kufunga drip irrigation system
4.Kuanza kilimo hai (organic farming) cha umwagiliaji,mazao ni
-mboga mboga
-nyanya
-Vitunguu nk
Pia tutalima chakula ikiwemo mahindi,mtama nk
Bila kusahau maharage na mazao jamii ya kunde.

Mimi ni mhitimu kutoka SUA na nilikua nafanya kazi kwenye shirika binafsi lakini naona naweza tumia fursa hii na naamini familia yangu nitaitoa,Familia yangu iko Bariadi,wilaya ya Itilima.
Bank nazowaza kupata mkopo ni CRDB na NMB kama mawazo yangu yatakubaliwa.
Kama nikipata huu mkopo,mie ni mtoto wa pili,nimeoa na kaka yangu pia kaoa,mdogo wetu wa kike naye kaolewa lakini waliachana na mme wake.
Katika familia kiwango cha elimu ni hivi
1.Baba na Mama ni la saba
2.Kaka na mke wake ni la saba
3.Mimi degree na mke wangu ni degree(mwalimu)
4.Mdogo wangu wa kike ni form 4
5.Mdogo wangu mwingine wa kike ni form four lakini amefaulu kujiunga kidato cha tano hapo badae mwezi wa saba kama sikosei.
6.Waliobaki ni wadogo wetu watatu bado ni under 18 so hawatakuwepo kwenye mambo ya kisheria lakini haki na gawiwo la kifamilia watakua wanapata hasa likielekezw8a katika gharama za shule na mahitaji yao muhimu.

Kwa kuwa kidogo mie nina uelewa wa juu kielimu,nataka niwe ndio Chief operating Manager wa familia,kuwangoza ndugu zangu na kusimamia operation zetu za familia.Baba yangu atakua mwenyekiti tu lakini atakua na maamuzi katika mikakati ya kufamilia na kuamua kesi ndogo ndogo za kufamilia punde zikitokea,lakini mambo ya biashara,kusimamia marejesho ya mkopo na uwajibikaji mie nitajitwika mzigo huu.Naamini baada ya miaka 5-10 nitakua nimemaliza kulipa mkopo na faida juu.

Naomba ushauri wa kisheria,kiuchumu,kijamii na kimawazo,je hili wazo langu linaweza likafanikiwa? Kma ndio nifanye nini ili nipate mkopo haraka? Kama hapana nirekebishe wapi ili nitimize lengo hili?

Kama wazo langu ni zuri naomba mnielekeze taratibu za kufauta nipate mkopo,lakini kabla ya hapo naomba mtu wakuniandalia project plan na business plan,nitahitaji pia mwanasheria wa kuniandalia katiba na partnership deed
Nitashukru sana,mimi ni mtaalam wa usindikaji wa mazao ya chakula km na wewe unahitaji kiwanda cha kusindika chakula cha binadam nitafute tu nikusaidie,nikuandalie kila kitu ikieemo kusajiriwa na taasisi za kiserikali TBS,TFDA,OSHA etc
Asanteni wakuu,pia unaweza ukanifuata PM kwa kunishauri zaidi


ulishawai kukopa kabla?


mil 20 ulipe kwa mda gani?
 
ulishawai kukopa kabla?


mil 20 ulipe kwa mda gani?
Sijawahi kukopa bank,huwa nakopa kazini tu.Mwaka juzi nilikopa 2M nikazirudisha kwa 6months,mwaka jana nikakopa 4M nikazirudisha kwa miezi 8 na mwaka huu na mwaka huu nina mkopo wa 6M naumalizia mwezi nane kuurejesha japo mikopo hii inakua haina riba kabisa
 
Wanahitaji nini hasa? Maana dhamana nitaweka hilo hilo shamba
Mkuu dhamana si tatizo sana, hicho ni kitu cha mwisho kabisa wanaangalia baada ya kuwaonyesha biashara yako na kama ipo kihalali (unalipa kodi). Ukienda kwa afisa mikopo yeyote cha kwanza ni kutembelea biashara yako..

Trust me, hata ukiweka mali ya million 100 uombe hata million 5 wakati huna biashara iliyosajiliwa na ina leseni zote hawawezi kukupa mkopo.

Pia, biashara zinazokopesheka ni zile ambazo zinaingiza kipato kila mwezi/siku.. Yaani ile pesa wanayokupa wanataka iwe in circulation ili iwe rahisi kurudisha marejesho. Sasa wewe kulima it means mpaka uvune, uuze ndio upate pesa. Hapo ni ngumu kukupa mkopo wa biashara maana huna source kufanya marejesho ya kila mwezi. Ungekuwa mfanyakazi au una kibiashara kingine za kuzugia ungeweza fanya hivyo lakini kama huna biashara kabisa hapo mkuu hakuna pesa utapata.

Sisemi haya kwa kukukatisha tamaa ila nakusaidia usipoteze muda wako kwenda kupanga foleni, na vile maafisa mikopo wanavyowadharau wajasiriamali wadogo unaweza toka na matusi huko ofisini..
 
Mkuu dhamana si tatizo sana, hicho ni kitu cha mwisho kabisa wanaangalia baada ya kuwaonyesha biashara yako na kama ipo kihalali (unalipa kodi). Ukienda kwa afisa mikopo yeyote cha kwanza ni kutembelea biashara yako..

Trust me, hata ukiweka mali ya million 100 uombe hata million 5 wakati huna biashara iliyosajiliwa na ina leseni zote hawawezi kukupa mkopo.

Pia, biashara zinazokopesheka ni zile ambazo zinaingiza kipato kila mwezi/siku.. Yaani ile pesa wanayokupa wanataka iwe in circulation ili iwe rahisi kurudisha marejesho. Sasa wewe kulima it means mpaka uvune, uuze ndio upate pesa. Hapo ni ngumu kukupa mkopo wa biashara maana huna source kufanya marejesho ya kila mwezi. Ungekuwa mfanyakazi au una kibiashara kingine za kuzugia ungeweza fanya hivyo lakini kama huna biashara kabisa hapo mkuu hakuna pesa utapata.

Sisemi haya kwa kukukatisha tamaa ila nakusaidia usipoteze muda wako kwenda kupanga foleni, na vile maafisa mikopo wanavyowadharau wajasiriamali wadogo unaweza toka na matusi huko ofisini..
Dah sasa afanye nini mkuu au ndio wazo lake haliwezekani kabisa
 
Good business idea nakushauri kwa hali iliyopo kwenye Banking industry ni vigumu kupata mkopo ila nsikuvunje moyo Go and test.
 
Mkuu dhamana si tatizo sana, hicho ni kitu cha mwisho kabisa wanaangalia baada ya kuwaonyesha biashara yako na kama ipo kihalali (unalipa kodi). Ukienda kwa afisa mikopo yeyote cha kwanza ni kutembelea biashara yako..

Trust me, hata ukiweka mali ya million 100 uombe hata million 5 wakati huna biashara iliyosajiliwa na ina leseni zote hawawezi kukupa mkopo.

Pia, biashara zinazokopesheka ni zile ambazo zinaingiza kipato kila mwezi/siku.. Yaani ile pesa wanayokupa wanataka iwe in circulation ili iwe rahisi kurudisha marejesho. Sasa wewe kulima it means mpaka uvune, uuze ndio upate pesa. Hapo ni ngumu kukupa mkopo wa biashara maana huna source kufanya marejesho ya kila mwezi. Ungekuwa mfanyakazi au una kibiashara kingine za kuzugia ungeweza fanya hivyo lakini kama huna biashara kabisa hapo mkuu hakuna pesa utapata.

Sisemi haya kwa kukukatisha tamaa ila nakusaidia usipoteze muda wako kwenda kupanga foleni, na vile maafisa mikopo wanavyowadharau wajasiriamali wadogo unaweza toka na matusi huko ofisini..
Asante mkuu kwa ushauri
 
Wakuu,nina shamba la familia la ekari 4 lenye hati ya kimila tuliyopewa 2010 mwezi wa saba.
Kulingana na hali ya kiuchumi ya sasa,ninataka niunganishe familia yangu yenye watu wazima 6 km kikundi cha familia,tuandae business plan,katiba na tuweze kwenda bank kuomba mkopo wa shilingi miliini 20.
Nina malengo yafuatayo,baada ya kupata mkopo,
1.Kuchimba kisima cha kina kirefu
2.Kununua pamp ya maji
3.Kufunga drip irrigation system
4.Kuanza kilimo hai (organic farming) cha umwagiliaji,mazao ni
-mboga mboga
-nyanya
-Vitunguu nk
Pia tutalima chakula ikiwemo mahindi,mtama nk
Bila kusahau maharage na mazao jamii ya kunde.

Mimi ni mhitimu kutoka SUA na nilikua nafanya kazi kwenye shirika binafsi lakini naona naweza tumia fursa hii na naamini familia yangu nitaitoa,Familia yangu iko Bariadi,wilaya ya Itilima.
Bank nazowaza kupata mkopo ni CRDB na NMB kama mawazo yangu yatakubaliwa.
Kama nikipata huu mkopo,mie ni mtoto wa pili,nimeoa na kaka yangu pia kaoa,mdogo wetu wa kike naye kaolewa lakini waliachana na mme wake.
Katika familia kiwango cha elimu ni hivi
1.Baba na Mama ni la saba
2.Kaka na mke wake ni la saba
3.Mimi degree na mke wangu ni degree(mwalimu)
4.Mdogo wangu wa kike ni form 4
5.Mdogo wangu mwingine wa kike ni form four lakini amefaulu kujiunga kidato cha tano hapo badae mwezi wa saba kama sikosei.
6.Waliobaki ni wadogo wetu watatu bado ni under 18 so hawatakuwepo kwenye mambo ya kisheria lakini haki na gawiwo la kifamilia watakua wanapata hasa likielekezw8a katika gharama za shule na mahitaji yao muhimu.

Kwa kuwa kidogo mie nina uelewa wa juu kielimu,nataka niwe ndio Chief operating Manager wa familia,kuwangoza ndugu zangu na kusimamia operation zetu za familia.Baba yangu atakua mwenyekiti tu lakini atakua na maamuzi katika mikakati ya kufamilia na kuamua kesi ndogo ndogo za kufamilia punde zikitokea,lakini mambo ya biashara,kusimamia marejesho ya mkopo na uwajibikaji mie nitajitwika mzigo huu.Naamini baada ya miaka 5-10 nitakua nimemaliza kulipa mkopo na faida juu.

Naomba ushauri wa kisheria,kiuchumu,kijamii na kimawazo,je hili wazo langu linaweza likafanikiwa? Kma ndio nifanye nini ili nipate mkopo haraka? Kama hapana nirekebishe wapi ili nitimize lengo hili?

Kama wazo langu ni zuri naomba mnielekeze taratibu za kufauta nipate mkopo,lakini kabla ya hapo naomba mtu wakuniandalia project plan na business plan,nitahitaji pia mwanasheria wa kuniandalia katiba na partnership deed
Nitashukru sana,mimi ni mtaalam wa usindikaji wa mazao ya chakula km na wewe unahitaji kiwanda cha kusindika chakula cha binadam nitafute tu nikusaidie,nikuandalie kila kitu ikieemo kusajiriwa na taasisi za kiserikali TBS,TFDA,OSHA etc
Asanteni wakuu,pia unaweza ukanifuata PM kwa kunishauri zaidi
vema zaidi. Ila nikusaidie kitu ukitaka kupata mkopo vizuri usisajili kama kikundi.sajili ka biashara,kampuni au kiwanda na mgawane his a mfano mpo 10, his a 100÷10=his a 1. kwa msaada zaidi 0754566564
 
Back
Top Bottom