Mungu alipoumba maumbile yetu aliumba na vitu ambavyo vitasaidia katika kufanikisha kila hitaji letu,tatizo hapa ni watu kukurupuka kufanya ngono huku wakiwa hawako tayari kwa tendo lenyewe,mnatakiwa muwe tayari kwa kufanya tendo lenyewe sio mmoja anataka huku mwingine hataki au anaogopa kuumia.
Inaonekana kabisa hauna elimu ya uzazi na malezi kwa ujumla maana haiwezekani ufikie hadi kufanya tendo huku ukiwa hujui nini cha kufanya ili tendo lifanikiwe bila kuwa na matatizo.
Nakuonea huruma maana wanakuambia upake mafuta utatue tatizo hilo kumbe wanakuharibu maana hata ukikutabna na mwanamke ambaye sio bikira inawezekana ukashindwa kumfanya afurahie tendo,cha msingi tafuta waliokuzidi umri wakuelekeze nini cha kufanya.
Utandawazi una raha yake na shida zake,enzi zetu ukitoka jando unajua kila kitu cha kufanya siku hizi vijana hawajui kitu.