Msaada: Nahitaji mtu wa kunifundisha gari

Ndugu kuwa muelewa.. gari usipoendesha muda mrefu unaloose control.. ndio maana kazi za madereva zinataka experience.. yaani asome veta mwezi mmoja ajue kisha akae mwaka mzima bila kugusa gari.. halafu asikosee kweli?
Kwamba hata kufuata barabara itakuwa shida mpaka aishi mtaroni? Nimemshauri aongee na bosi afanye mazoezi kwa kutumia gari ya kazi.
 
Kama una muda uwe unaenda mitaa ya Bandarini kuanzia geti namba 5 muda ya saa 10 foleni ikianza.

Jichanganye uongee na wale madogo wa kuuza karanga/sigara uwa wanaachiwa kusogeza gari za trip town zenye container empty.

Kule utapata uzoefu mzuri wa manual maana madereva wenye Mishe zao huacha gari wasogezewe, utapata kujiamini kwa kuendesha manual vigongo za Madina 2001 na Motichand.
Hii imenifanya nicheke, kwa hiyo madereva wanaenda wapi na kuwaachia wachuuzi wa barabarani wajibu wa kuyasogeza magari yao?
 
VETA nilifanya mazoezi na mtihani pia nimefanya ila unapokuja suala la control barabarani kwa aliyepitia hapo VETA ataniunga mkono,
Kwa sheria na alama za barabarani nipo vizuri sana tena sana, na ndio kipaumbele chuoni.
Pia ahsante kwa ushauri wako mzuri nitaufanyiakazi mungu akubariki
Kweli mkuu veta tunafata cheti tu ila gari kujua ngumu sana maana practical zao ni muda mchache sana
 
Gari ushajua Ila tatizo nikama ilivyoanza KUSEMA umetokea familia maskini, ndiyo kinachokunyima Amani bado minyororo ya UMASKINI wa familia imekuzonga. Kuna watu hawaendelei kwa kwakuwa hawaamini Wanachokifanya. Usikute hata kuacha huo ulinzi UNAOGOPA. Kuukata UMASKINI NI sawa na kujitoa kwenye unyororo. Unahitaji pia moyo wa kijasiri.
Hapana mkuu, nishafanya kazi nyingi sana kulingana na elimu yangu na pia sijawahi kuogopa kuacha kazi kikubwa ni maslahi gani napata kulingana na kazi nnayofanya.
Kuhusu umaskini ni kweli unaleta hali ya mtu kutojiamini, na sio umaskini tu hata elimu pia mfano nchi zetu za kiafrika hatujiamini kwasababu ni maskini na kiwango cha wenye elimu kubwa ni kidogo kulingana na wenzetu ulaya.
 
Nimekuonea huruma. Kama bado hujapata mtu. Nicheki nikupe namba za mwamba bosi wa garage. Atakufundisha bure tena hata kwa gari manual. Mchawi itakua kuweka mafuta. Tena yupo Kigamboni hukohuko.
Ubarikiwe na mungu akuzidishie palipo pungua
 
Habari Wakuu,

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 30 elimu yangu ni form IV natokea kwenye familia ya kimaskini iliyopo Kigamboni jijini Dar.

Kutokana na changamoto na ugumu wa maisha nikaamua kujiunga na kazi ya ulinzi (nimepitia kazi nyingi za msoto).

Hivyo kutokana na changamoto nikaona nisave kipato changu ili angalau niwe na fani yoyote, nashukuru mungu nilifanikiwa kusave nikaenda VETA kusomea udereva (basic driving course) na nikafanikiwa kupata cheti na leseni.

Sasa hapa lindoni kwangu ninapolinda (nalinda nyumba ya mtu binafsi masaki) huyu boss nimejaribu kumwelezea changamoto za maisha ninayopitia alichoniambia kama naweza kuendesha gari nimpelekee cheti na leseni yangu, hivyo vyote nnavyo tatizo sina experience/control hasa vurugu za barabarani naogopa kulitia mtaroni gari la watu nikapata lawama zaidi.

Mwenye nia na uwezo wa kunisaidia niweze kupata uzoefu naomba anisaidie.
Kuhusu pesa ya mafuta nitakuwa nachangia kadri jinsi tutakavyokubaliana.

Naombeni msaada wenu please.
Ahsanteni
Kwa hiyo VETA wanawapa watu Vyeti na Leseni bila uwezo wa kuendesha gari? Ina maana vijana wetu wanapoteza pesa bure kusoma VETA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom