Msaada: Mikataba kwenye nyumba za Kupanga

PAGAMECO

JF-Expert Member
Jul 8, 2016
1,207
1,234
Habarini za mihangaiko? Kazi ni kazi na popote kambi

Natanguliza dua za kumuombea m Tanzania mwenzetu Tundu Antpass Lissu Mungu amfanyie wepesi


Nahitaji msaada wa mikataba ya kwenye nyumba za kupanga naona hawa watu wanataka kunipanda kichwani kutokana na usumbufu wa

  1. Kuchelewa kulipa kodi.
  2. Kila mtu kujiamulia anavyotaka mara atoe pesa ya umeme mara asitoe.
  3. Uharibifu wa thamani za nyumba mfano.rangi za ukuta, socket za umeme na wavu za madirisha.
  4. Kufungulia mziki kwa sauti ya juu nyakati za usiku na kuleta kero kwa wapangaji wengine

Kama utanisaidia kunitumia hata mfno wa page kadhaa in whatsapp nitashukuru

NB: Nyumba za kupanga ni biashara kama biashara nyingine
karibu ni wakuu kwa michango yenu .
 
Nyie ndio wenye Nyumba wenye roho mbaya kama mashetani .... Acha Nyumba zenu ziharibiwe tu hakuna namna
 
jaribu kwenda hata kwenye stationary wakuchapie kwenye computer...unawapa maelezo/ vitu gani unataka viwepo then wanakuchapia halafu unatoa nakala utakazo
 
Hakuna watu kero huku duniani kama wapangaji, tu utakuta analipa sh 40elf lakini kelele zake, hajielewi kama anasaidiwa hapo alipopanga, chini ya elfu 1500 kwa siku bado utasikia naishi kwa hela zangu!!!!, wenye nyumba wana roho njema sana na niwavumilivu, yaani ng'ombe ana faida kuiko mpangaji, chumba kimoja ukiweka ng'ombe wawili aziwa lita hata 8 kwasiku sh16000 toa hata elf 10 matunzo kwa siku bado una faida
 
Hahaha Mkuu Umenichekesha Bora Ufuge Ng'ombe Utakunywa Maziwa


Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app
 
Thanks Mkuu Joserevest Kwa Ushauri But Ule Muundo Wa Mkataba Ndio Sina

Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app
Ukiwauliza wanaweza kuwa nao kwa maana huwa wanachapisha documents za aina mbalimbali au tafuta nyumba za jirani hapo mtaani kwako ongea na mpangaji mmojawapo akupe mkataba then ukapige copy halafu uwape wale wanaochapisha wafatishe mfumo huo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…