Msaada mgogoro wa watoto

mrdream

Senior Member
Mar 23, 2014
122
245
Wakuu naomba msaada wenu wa ufafanuzi wa sheria. Nililipa mahari mwaka 2012. Tukapata watoto mapacha mwaka 2014. Tulifunga ndoa ya kiserikali mwaka 2015. Sote ni watumishi wa umma. Tunafanya kazi mikoa tofauti. Mwaka 2016 alikataa kuhamia ninapofanyia kazi tukaingia kwenye mgogoro akabaki na watoto. Mwaka 2018 ameamua kuwabatiza bila kunishirikisha na amegoma kutuma copy za vyeti vya kuzaliwa na copy za vyeti vya ubatizo. Nimejaribu kuhusisha wazee wake kwa hili wapo pamoja na binti yao. Hakuna ushirikiano kabisa. Nifanyeje. Watoto wana miaka mitano sasa. Je nitawapata baada ya kutimiza miaka saba? Je majina waliyowabatiza itakuwaje?
 
well, cha msingi unataka watoto waje kuishi na wewe/wawe chini ya uangalizi wako au unataka kuwabadilisha majina tu? hili haya yote yafanikiwe, unapaswa kujua kwamba ni lazima uivunje hio ndoa, sasa hivi wewe na mzazi mwenzio bado hamjaeleweka, mko separate tu au mmesha achana jumla japo sio kwa utaratibu wa sheria kama talaka na mahakama kutengua ndoa.

custodian ya watoto unaweza kuipata pia kwa wewe kwenda juvenile court/mahakama ya watoto kwa sehem uliyopo/kama dar ipo kisutu, then ukaomba maombi ya uangalizi wa watoto.
 
Back
Top Bottom