Msaada, matibabu ya Anal fissure

Msaada, matibabu ya Anal fissure

profesawaaganojipya

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2015
Posts
1,596
Reaction score
3,437
nikienda haja kubwa napata maumivu makali sana,na damu zinadondoka matone mfululizo,kuna uvimbe sehemu ya haja kubwa,naomba ushauri nitumie dawa gani,ni wiki moja tangu tatizo lianze...msaada tafadhali
 
nikienda haja kubwa napata maumivu makali sana,na damu zinadondoka matone mfululizo,kuna uvimbe sehemu ya haja kubwa,naomba ushauri nitumie dawa gani,ni wiki moja tangu tatizo lianze...msaada tafadhali
Kama una Anal Fissure
Tumia
Lactulose syrup 10mls mara mbili kwa siku ili kusoften stool
Topical Nitroglycerin 0.4% apply mara mbili

Sitz baths(Dettol 20mls kwenye maji ya uvuguvugu kila baada ya kutoka toilet).

Unaweza kutafuta Lidocaine ointment Kwa ajili ya maumivu
 
nikienda haja kubwa napata maumivu makali sana,na damu zinadondoka matone mfululizo,kuna uvimbe sehemu ya haja kubwa,naomba ushauri nitumie dawa gani,ni wiki moja tangu tatizo lianze...msaada tafadhali
Hakikisha katika milo yako motatu kwa siku mlo mmoja uwe wa matunda 100%

Hakikisha unakunywa maji ya kutosha ..

Kama unakunywa uji wa lishe au wa ulezi acha kabisa

Hakikisha unakula matunda mchanganyiko kwa wingi sana
 
Kama una Anal Fissure
Tumia
Lactulose syrup 10mls mara mbili kwa siku ili kusoften stool
Topical Nitroglycerin 0.4% apply mara mbili

Sitz baths(Dettol 20mls kwenye maji ya uvuguvugu kila baada ya kutoka toilet).

Unaweza kutafuta Lidocaine ointment Kwa ajili ya maumivu
asante sana mtaalam,Mungu akubariki..
 
do! hii kitu acha kabisa!
wengine ni kama tulishazoea hivi na tiba yangu kubwa ni papai na maji mengi pia punguza vyakula vya wanga na ukiweza punguza uzito na kazi za kukaa muda mrefu mambo yatakuwa shwari uvimbe unaweza kuwepo lakini hautakusumbua na ukifanya vizuri zaidi unaweza kuondoka. mfano hapa asubuhi nishapiga papai kabla ya chai na kwa muda huu nina maji mbele yangu.
 
do! hii kitu acha kabisa!
wengine ni kama tulishazoea hivi na tiba yangu kubwa ni papai na maji mengi pia punguza vyakula vya wanga na ukiweza punguza uzito na kazi za kukaa muda mrefu mambo yatakuwa shwari uvimbe unaweza kuwepo lakini hautakusumbua na ukifanya vizuri zaidi unaweza kuondoka. mfano hapa asubuhi nishapiga papai kabla ya chai na kwa muda huu nina maji mbele yangu.
Mkuu mie hii Hali ilianza nitokea 2010 mpaka saivi ninayo.
Nilikuwa nakaa Sana nasoma afu ulaji ni wali Sana.
Sema kweli ukilainisha choo inatoka kawaida.
Sema uvimbe huwa unatoka nje unapojikaza wakati wa haja.
Ukiwa unasafisha una feel sema unarudi.
Yaani kama mazoezi nilipitia jakata piga Sana tizi Ila hakuna kupungua..
 
Mkuu mie hii Hali ilianza nitokea 2010 mpaka saivi ninayo.
Nilikuwa nakaa Sana nasoma afu ulaji ni wali Sana.
Sema kweli ukilainisha choo inatoka kawaida.
Sema uvimbe huwa unatoka nje unapojikaza wakati wa haja.
Ukiwa unasafisha una feel sema unarudi.
Yaani kama mazoezi nilipitia jakata piga Sana tizi Ila hakuna kupungua..
Pokea ushauri na uwe serious kuufanyia kazi utapona

Kwa maisha ya kawaida ya watu wengi huwa na milo mitatu kwa siku katika hiyo milo mitatu hakikisha mlo mmoja unakuwa wa matunda pekee

Utachagua mwenyewe kama ni wa asubuhi, mchana au jioni na matunda hayo yawe mchanganyiko mfano Papai, chungwa, tikiti, ...embe, tango parachichi,carrot Nk

Hakikisha unakuwa Rafiki mzuri wa Maji
Yaani hakikisha angalau isipite siku hujanywa walau lita Mbili au zaidi za maji
Japokuwa utaenda haja ndogo mara kwa mara lakini ni Afadhali usumbuke kwenda haja ndogo kuliko upasuliwe na kuchomekwa mipira na plastics

Punguza vyakula vya wanga kama wali mfululizo....punguza sana au acha kabisa kunywa uji wa lishe au wa ulezi kwa maana una tabia ya kukausha choo sana ....
Ili kuthibitisha hili kama umewahi kuona kinyesi cha watoto wadogo wanaokunywa uji wa lishe mfululizo...

Kula vyakula vya mboga kama bamia ...nyanya chungu (ngogwe)...Biringany kwa wingi...kwa maana vina nyuzi nyuzi zinazosaidia kusafisha utumbo mpana na kulainisha choo...

Kama ni mlaji wa Machungwa basi unapokula chungwa usiishie kunyonya maji tu ka kutupa yale manyuzi nyuzi hapo utakuwa unapoteza kitu kikubwa sana..kula na nyama na nyuzi zote za ndani zina faida sana sana

Tatizo lako kwa 90% limechangiwa na ulaji Mbovu usio na mpangilio, pamoja na
Kutokunywa maji kwa wingi...

Zingatia niliyoandika hapa utaona mabadiliko...na utapona.

Ukipuuza shauri yako.
 
Pokea ushauri na uwe serious kuufanyia kazi utapona

Kwa maisha ya kawaida ya watu wengi huwa na milo mitatu kwa siku katika hiyo milo mitatu hakikisha mlo mmoja unakuwa wa matunda pekee

Utachagua mwenyewe kama ni wa asubuhi, mchana au jioni na matunda hayo yawe mchanganyiko mfano Papai, chungwa, tikiti, ...embe, tango parachichi,carrot Nk

Hakikisha unakuwa Rafiki mzuri wa Maji
Yaani hakikisha angalau isipite siku hujanywa walau lita Mbili au zaidi za maji
Japokuwa utaenda haja ndogo mara kwa mara lakini ni Afadhali usumbuke kwenda haja ndogo kuliko upasuliwe na kuchomekwa mipira na plastics

Punguza vyakula vya wanga kama wali mfululizo....punguza sana au acha kabisa kunywa uji wa lishe au wa ulezi kwa maana una tabia ya kukausha choo sana ....
Ili kuthibitisha hili kama umewahi kuona kinyesi cha watoto wadogo wanaokunywa uji wa lishe mfululizo...

Kula vyakula vya mboga kama bamia ...nyanya chungu (ngogwe)...Biringany kwa wingi...kwa maana vina nyuzi nyuzi zinazosaidia kusafisha utumbo mpana na kulainisha choo...

Kama ni mlaji wa Machungwa basi unapokula chungwa usiishie kunyonya maji tu ka kutupa yale manyuzi nyuzi hapo utakuwa unapoteza kitu kikubwa sana..kula na nyama na nyuzi zote za ndani zina faida sana sana

Tatizo lako kwa 90% limechangiwa na ulaji Mbovu usio na mpangilio, pamoja na
Kutokunywa maji kwa wingi...

Zingatia niliyoandika hapa utaona mabadiliko...na utapona.

Ukipuuza shauri yako.
Ndugu mie nakukatalia labda sema ninapokosea ni kuwa sijawahi hata mlo mmoja nikala mlo wa matunda pekee lazima nachanganya.
Ila maji mkuu mie ni mdau mmoja mkubwa Sana nikiwa advance maji Lita 10 yanaisha kwa siku huwezi amini.

Hapa home nikiamka lazima jagi liishe ndo nasafisha kinywa ni desturi Fulani.

Hayo matunda Kuna muda niliyalaga Sana chuoni Ile mfufulzo.
Hapa nikiwa nakula tunda linakuwepo Ila sio frequently. Unaweza ukakuta chungwa tikiti papai grapes kulingana tunda linalopatikana na mfukoni nikoje
 
do! hii kitu acha kabisa!
wengine ni kama tulishazoea hivi na tiba yangu kubwa ni papai na maji mengi pia punguza vyakula vya wanga na ukiweza punguza uzito na kazi za kukaa muda mrefu mambo yatakuwa shwari uvimbe unaweza kuwepo lakini hautakusumbua na ukifanya vizuri zaidi unaweza kuondoka. mfano hapa asubuhi nishapiga papai kabla ya chai na kwa muda huu nina maji mbele yangu.
hospital hakuna msaada?
 
Mkuu mie hii Hali ilianza nitokea 2010 mpaka saivi ninayo.
Nilikuwa nakaa Sana nasoma afu ulaji ni wali Sana.
Sema kweli ukilainisha choo inatoka kawaida.
Sema uvimbe huwa unatoka nje unapojikaza wakati wa haja.
Ukiwa unasafisha una feel sema unarudi.
Yaani kama mazoezi nilipitia jakata piga Sana tizi Ila hakuna kupungua..
tatito mimi kuna kama uvimbe namikwaruzo,ninapoenda haja kubwa ni maumivu makali sana,hata nikikaa tu bi maumivu mkuu,hosp vipi,hawatibu?
 
Pokea ushauri na uwe serious kuufanyia kazi utapona

Kwa maisha ya kawaida ya watu wengi huwa na milo mitatu kwa siku katika hiyo milo mitatu hakikisha mlo mmoja unakuwa wa matunda pekee

Utachagua mwenyewe kama ni wa asubuhi, mchana au jioni na matunda hayo yawe mchanganyiko mfano Papai, chungwa, tikiti, .
sasa karoti tena,si ni ngumu mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom