Msaada maji shingoni

Msaada maji shingoni

Ooooh.......sasa itakuwaje........?.......
 
naamini wewe ni mtu mzima unaejitambua, ulijua unachokifanya na huyo binti hapo kitandani. so usikatae damu yako. Asitoe hiyo mimba... ni hatari, ni dhambi, na hicho kiumbe hakina hatia.
 
Mwanamke mwingine tena ataumizwa moyo.

We jipange namna ya kutoa taarifa mbaya kwa huyo mpenzio, na ujiandae kwa maamuzi yake. Lakini pia jiandae kulea mwanenu ndo mavuno hayo.
 
Ndio matatizo ya kuchepuka!Itabidi uone huyo mwenye mimba na ukubali kumtenda mchumba wako.
 
sijui nifanyeje..ninamchumba angu tuko kwenye mahusiano miaka mitatu sasa na tumeahidiana kuoana lakin mapenz ni ya long distance ye anafanya kazi mkoa mwingine.Tatizo liko kwangu huku nliko niliingia kwenye mahusiano na kabint flani nikijua kakupooza tu lakin miez minne sasa nimenogewa na kabinti haka na kameshika mimba hata sijui iweje nikimwambia tutoe anasema hatoi kama sitak mtoto nisimjue atalea mwenyewe..najiuliza nifanye uamuz gan katika hili..

tuliza akili kwanza fikiria nin wataka, usikurupuke kama mwanzo.

Next time kumbuk condom mkuu
 
kaka hapo huna choice jipange kulea kama Mimi.hiyo imenitokea pia hivo hivo nilikua nataka kupita ooh nikaona mwez mmoja baadae bint Mara maembe mabich,Mara ukwaju Mara malimao nikasema tayari.nilichokifanya sikupanic bro nikakubaliana na hali halisi ninae mpaka sahiz bint mimba ina miezi mitano broo.kubali matokeo broo
 
Nakupa Hongera Kwa Kuwa Baba Kijacho
Fungua Moyo Wako Na Umpe Baraka Zote Mwanao
Huyo Ndo Mkeo Kwani Haujui Kesho Itakuwaje
Mimba Utaitoa, Huyo Wa Mbali Haujui Yu Katika Hari Gani!.... Labda Naye Kazama Kwa mwingine??
Hesabu Ndo Ushaangukia Ulipopataka , Mshukuru Mungu Wako
Ahsante Jigo
 
Back
Top Bottom