Msaada kwenye umeme jua (Solar Electricity)

Msaada kwenye umeme jua (Solar Electricity)

Hikma

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2012
Posts
497
Reaction score
415
Habari wanajukwaa.

Naombeni ushauri wa kitaalamu kwenye mada tajwa.
Nataka kufunga system mbili zenye kujitegemea za solar nyumbani kwangu.

1. System yenye uwezo wa kuwasha taa 20 za wats 9 (energy savers) kwa masaa 12 bila kwikwi.

2. System yenye uwezo wa kuwasha tv ya inchi 32 (flat), king'amuzi, dvd player, feni ndogo, na redio ndogo.

Nyumba imeshafanywa wiring ya kawaida.

Nitashukuru kama nipatiwa orodha ya vifaa vitakavyotakikana kwa kila system, makadirio ya gharama, pamoja na ushauri wa dealer mzuri anayeviuza.

Natanguliza shukrani
 
Panel watt200 inatosha kwa ona yangu. Hizo panel ziwe ktk pisi mbili yaani watt100 + 100= 200 au zaidi. Na battery mbili pia. Inverter watt300
 
ili uweze kuwasha taa bila shida itakulazimu kutumia taa za dc. maitaji ni betri ya watt 120 .panel watts 150 na chaja cotroo
 
1.Nunua panel mbili za watt 100 kila moja
2.Betri za mbili za N 200+ kila moja
3.Inverter watt 1000
5.Tumia taa za DC
Kuhusu bei uliza mwenyewe dukani
 
Mm kwa ushauri wangu nikushauru ukitaka kununua pannel nzuri ya solar nunua pannel yenye ile lebo inayoonyesha wtts za solar iwe ndani ya kioo cha pannel(isiwe imebandikwa kwa nje) pia kuhusu upande wa battery ambazo zina uhakika kidogo ni hz za maji dry wanachakachua sana uwe makini ukitaka kuchukua dry , taa nunua za dc za wtts 2, 3 na 1 mchanganyiko, kwa maana chumban weka ya wtts 1, seblen wtts 2 nje wtts 3 itategemeana na mpangilio wako,..cjajua flat screen unayotumia inakula moto kiasi gan, ila kwa haraka haraka nafikiri pannel ya wtts 180 au 200 itakufaa battery chukua ya ah 200, inverter tafta ya wtts 350. Mm nina pannel zinazo sambazwa na steps made in Germany ya wtts 120 na battery ya solar chloride oxide hz za maji zinazo tengenezwa Kenya, inverter ya 150 wtts,huwa nawasha flat screen inch 22 ambayo 2 in 1 (dc na ac), receiver ya king'amuzi,taa 2 za watts 1 @ 1,bufa ambayo ni DC na AC na laptop zaidi ya masaa 10 bila moto kuisha, huo ndo uzoefu wangu tusubiri wataalam zaidi waje.
 
Nawashukuru sana ndugu zangu mliojitokeza kutoa msaada wenu wa ushauri wa kitaalamu na uzoefu.
Angalau sasa nimepata pa kuanzia.

Karbuni na wengine kwa mawazo zaidi.
 
Mimi nina pannel watts 300 battery n 100x2 za chloride exide kaa mdau alivyosema dry zinachakachuliwa sana na original haipungui 500000 kwa n100 wakati ya maji original ni kama laki2 hivi. Nna charger control ya amp 30 invertor ya watts 300 tv led ya watts 22 na taa mchanganyiko za ac na dc ambapo dc nawasha mpaka asubuhi ac nazima na nimezifunga ndani ili nisichoshe invertor. Taa zipo zaidi ya 10 decoder 2 radio ya watts 56 laptop watts 65 na vitu vidogo vidogo. Umeme hauleti shida labda kipindi cha mawingu mazito na mvua. Vya msingi ni kujumlisha watts zote za vifaa vyako na visizidi uwezo wa pannel na battery. Na hapohapo battery ili ijae vizuri inabidi watts za pannel ziwe nyingi kuliko uwezo wa battery mf mimi ni panel watts 300 battery n200 na c.control amp 30 invertor watts 300.vitu vyangu vyote havifiki watts 200 na sio rahisi kuwasha z vyote at a time
 
Umeme wa jua hauna stress kwakweli ukishamaliza kufanya manunuzi ya vifaa Kitaeleweka
 
Last edited by a moderator:
You can use the installed solar system as the AC lighting direct your lights at home. You need to have a change over switch to be used to change between the power from utility company (Tanesco) and your solar system, using the same wiring and installed lights without installing another wiring for the DC.
What you need to do is to switch of things like Cooker, Frigde, water heater etc.
Requirements;
to lights 20 lights, Hifi system, microwave, Tv 32", and Radio system: Solar panel 3pcs of 80W, Solar batteries maintenance free 3pcs @150HA, Charger controller 45A, Inverter 1000w preferably Magnum inverters.
 
Umeme wa jua hauna stress kwakweli ukishamaliza kufanya manunuzi ya vifaa Kitaeleweka
Naenjoy sana kwa sasa na unanipa kipato pia kwani nautumia kuonesha game zote za dstv na azam hivyo inanipa na kipato pia sasa kama jana hapa mpwapwa umeme ulikua unafluctuate a sana game wengine hawakuzifaidi kwa umeme wa tanesco ila solar ni raha sana.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom