Msaada kuhusu visimbuzi(ving'amuzi)

Msaada kuhusu visimbuzi(ving'amuzi)

Kaluluma

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2019
Posts
474
Reaction score
622
Habari za leo wakuu,

Ninaomba mwenye ufahamu kuhusu ving'amuzi vya Tanzania yaani DSTV, AZAM, ZUKU nk. Kipi kina unafuu katika vifurushi; kwa upande wangu napendelea tamthilia za Kitanzania kama Huba, Kitimtim n.k.

Itapendeza kama utanitajia na bei za kununulia visimbuzi hivyo pamoja na gharama za ufungaji. Napatikana Dodoma.

Natanguliza shukrani
 
Baki na hicho hicho ulichoangalia huba , au unaendaga kwa jirani?
 
Baki na hicho hicho ulichoangalia huba , au unaendaga kwa jirani?
🤣🤣Noma mkuu jirani kasema mwisho leo kwenda kwake namchafulia sofa zake,si unajua wengine ili tupate raha ya tamthilia mpaka tupandishe miguu yetu juu ya sofa😂😂
Only joking mkuu
Nilikua natumia cable mkuu,sasa nimehamia Dom ndo nataka kufunga king'amuzi mkuu
 
Tamthilia ulizozitaja hapo juu zinapatikana kupitia DSTV, kwenye kifurushi cha bomba 19,000.Pamoja na Tamthilia nyingine nyingi.
Bei ya DSTV full set ni Tsh 99,000 ufundi 20,000. Unapata kifurushi cha Family 29,000 mwezi mmoja bure.

Kazi kwako Mkuu Kaluluma
 
Habari za leo wakuu,

Ninaomba mwenye ufahamu kuhusu ving'amuzi vya Tanzania yaani DSTV, AZAM, ZUKU nk. Kipi kina unafuu katika vifurushi; kwa upande wangu napendelea tamthilia za Kitanzania kama Huba, Kitimtim n.k.

Itapendeza kama utanitajia na bei za kununulia visimbuzi hivyo pamoja na gharama za ufungaji. Napatikana Dodoma.

Natanguliza shukrani
TAMTHILIA ZOTE ULIZOZITAJA HAPO, ZINAPATIKANA KISIMBUZI CHA DSTV AMBACHO NDIO KINA VIFURUSHI VYA BEI KUBWA KULIKO HIVYO VISIMBUZI VINGINE, DSTV KIFURUSHI KIDOGO ZAIDI NI CHA SHILINGI 19000/= KWA AZAM HATA 10000/= UNAPATA SINEMA ZETU MWEZI MZIMA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TAMTHILIA ZOTE ULIZOZITAJA HAPO, ZINAPATIKANA KISIMBUZI CHA DSTV AMBACHO NDIO KINA VIFURUSHI VYA BEI KUBWA KULIKO HIVYO VISIMBUZI VINGINE, DSTV KIFURUSHI KIDOGO ZAIDI NI CHA SHILINGI 19000/= KWA AZAM HATA 10000/= UNAPATA SINEMA ZETU MWEZI MZIMA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Vip hapo kwa Azam, hiyo ten unapata channel kama ngapi? Naomba unitajie unazokumbuka. Samahani lakini.
 
TAMTHILIA ZOTE ULIZOZITAJA HAPO, ZINAPATIKANA KISIMBUZI CHA DSTV AMBACHO NDIO KINA VIFURUSHI VYA BEI KUBWA KULIKO HIVYO VISIMBUZI VINGINE, DSTV KIFURUSHI KIDOGO ZAIDI NI CHA SHILINGI 19000/= KWA AZAM HATA 10000/= UNAPATA SINEMA ZETU MWEZI MZIMA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nashukuru sana mkuu umenifumbua macho,ngoja nifuatilie hicho
 
Back
Top Bottom