Habari! Naomba kwa anaye fahamu shule ya machame girls anieleze kuhusu mazingira yake ya kusoma ipo maeneo yapi na pia contacts zake ikiwezekana , naomba ushauri wenu juu ya kuenda shule hii asante
Machame Girls ipo Wilaya ya Hai, zamani enzi zetu ilikua inavuma sana na wasichana waliokua wanatoka huko walikua wapo juu sana kimasomo lkn kwa sasa hivi sina uhakika sana kama bado inavuma kama zamani miaka yetu!
machame ipo hai kama alivokupa details huyo jamaa unapita moshi kama unaenda arusha then unaingia ndani ndani makoa kwa mbele,
BOX 3043 Moshi
Mazingira ya shule mazuri na ya kusoma pia mazuri wewe tu, ila itaendelea kua shule ya gvt tegemea ugali na maharage kwenda mbele. Huduma za kiafya pia nzuri
Dah, nimetoka maeneo hayo miaka 17 iliyopita ila shule ni nzuri na mazingira pia (natumaini hadi sasa) nilikuwa shule moja ya boarding jirani na mara nyingi tulikuwa tukisali machame girls.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.