Msaada Kuhusu pete ya uchumba.

rikiboy

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
22,170
Reaction score
43,974
Napenda kuuliza jamani eti Utaratibu wa kumvalisha pete ya Uchumba mwanamke kama umezaa nae bila ndoa upoje??? Je lazima ndugu wawepo unapomvalisha au unawapa tu taarifa hasa wazazi kuwa nimepata mchumba na pete nishamvalisha bila wao kumuona physically na vip kuhusu kwenda kanisani maana me ni mkristo???

Pia vipi kuna uwezekano wa kufunga harusi kanisani wakati tuna mtoto tayari?? Nahitaji mwanga kidogo hasa wenye experience na hili suala zima.
 
Kama hujui vitu vidogo kama hivyo basi nikushauri usioe kwanza kausha walau mwaka mmoja zaidi.
Ni kuamua tu mwenyewe utaratibu unaoona ni mrahisi kwako ambao utaendana na bajeti yako. Ya nini kualikwa watu weeengi uingie gharama, aubya nini hadi ukafanyie ukumbini hata nyumbani panatosha.
 
Kwao wananifahamu na nilienda kujitambulisha baada ya kujifungua kuhusu mahari ndo bado mkuu...!! Duuh kumbe pete mpaka mahari nilipe[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Utambulisho kwanza Ila kuvishana Pete Ni mpk uwe umelipia mahari n kanisani ndoa unafunga Ila lazma urudi kundini wewe na mchumba wako
Hii ya kurudi kundini kweli maana me Ni mlutheri..!! Vip Kubariki ndo na harusi tofauti yake ni nini?? Au tofauti ni kiimani zaidi lakini mavazi hata ya kuvaa siku ya sherehe kama shela yanafanana???
 
Una experience. .hongera itanibidi nije kuongeza ujuzi kwako
Utambulisho kwanza Ila kuvishana Pete Ni mpk uwe umelipia mahari n kanisani ndoa unafunga Ila lazma urudi kundini wewe na mchumba wako
 
Ahaa nimeshaelewa mkuu ila Sherehe zote sendofd na harusi zinafanyika??
 
Kwao wananifahamu na nilienda kujitambulisha baada ya kujifungua kuhusu mahari ndo bado mkuu...!! Duuh kumbe pete mpaka mahari nilipe[emoji23][emoji23][emoji23]

Pete bila mahari ni sawa na kula ndio unawe mikono .... Mahari ni muhimu mara milioni kuliko hata hiyo pete, pete ni zawadi tu kwa mpenzi wako, I mean zawadi kama zawadi nyingine yoyote ile lakini mahari ni heshima kwa mke na familia yake pamoja na unyenyekevu wa ombi la kukubaliwa mke na wazazi.

Kwa kifupi, kama mahari ni gari then pete ni kale ka taa ka juu ndani ya gari ambako, ukifungua mlango huwa kanawaka
 
inaelekea ww hauendagi kanisani wala jumuiya
 
huyu jamaa ni mweupe kwa kweli asubiri kidogo
 
Vipi akiwa ni mpentekoste ndio haruhusiwi kabisa kufunga ndoa na huyo mwanamke ama?
 
Hairuhusiwi kabisa. Ndio imetoka hivyo
Doh!! Imekula kwangu hii... na mimi nimemzalisha binti ila nahitaji kumuoa baadae na wote tumeokoka kwa maana hiyo sie ndoa ndio tusahau kabisa (lakini mchungaji wangu aliniambia haina shida)
 
Ni TAG mkuu, sikutengwa aisee
 
lengo la harusi ni nini wakati nyie ni wanandoa na mna mtoto tayari
 
Swali lako linatuwakilisha wanaume wengi wahumu JF hatuna ndoa ila tunawatoto
 
kama ulivyoshauriwa na mchangiaji mmoja kuwa kama hayo mambo ambayo yapo ya msingi kabisa (too basic need) na hata kijana mdogo tu wa form two anaweza kukuelezea kutokana na taratibu za koo zake wewe unaanzisha jukwaa ni bora ukasubiria hata mwaka mmoja kwanza kabla ya kufanya maamuzi ya kubariki au kufunga ndoa.
Pia kuhusu mtoto pia umeshajiridhisha kuwa ni wako??? Jiridhishe kwanza ili usije kuleta mada nyingine siku za usoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…