Msaada kuhusu kupima DNA

Kapime jaman usiuziwe mbuzi kwenye gunia
 
Kapime DNA hospitali kubwa za serikali wanatoa hiyo Huduma ila hakikisha unawaelezea ukweli wote usifiche kitu,

Maana ukionekana kama unapima DNA kwasababu umejisikia tu kufanya hivyo basi kwa Kuzuia ongezeko la watoto wa mitaani huwa wanakupa majibu kwamba mtoto ni wako hata kama sio wako,

Hivyo waambie kila kitu alichokuelezea mkeo hapo watakupa majibu sahihi maana uzuri ni kwamba Baba wa mtoto yupo.
 
Hata hizi hospital za mkoa naweza kupata kipimo hicho
 
Gharama ya DNA ni Wastani wa 150,000.....!

All in all kila kinachotokea Kwa Binadamu kina sababu.
Ipo sababu Kwa Nini umeachana na huyo Mwanamke.....!
Pia ipo sababu Kwa Nini umeletewa huyo Mtoto na Mungu ili Umtunze...!
Kwa ninavyofahamu gharama za DNA ni laki tatu kwa wote. Baba mama na mtoto. NA NI LAZIMA vipimo vifanyike kwa wote. Na vinafanyika kwa mkemia mkuu wa serikali, ofisi zake zipo kule nyuma ya ocean Road hospital barabara ya kuelekea Ikulu ya magogoni geti hili la nyuma.

Kuhusu utaratibu;
Unaweza fanya kwa mwanasheria au kwa amri ya Mahakama.

Asante.
 
Basi gharama zimepanda.
 
Kwanza pole San ndugu yangu,lakini mm nakushauri hyo pesa ya kulipa DNA achana nayo ipeleke kwa mtoto apate huduma zote,Amin mtoto ni wako2 maana mwanaume kulea mtoto asiye damu yake ni tangu enzi na enzi,hata yesu alilelewa na yusuph kama skosei wakat yusuph haya mfanya chochote huyo bikira Maria,lakini pia kama kuna uhitaji mkubwa San wakulima DNA achana na hizo za kizungu ni gharama San tumia za kikwetu niza uhakika sana na rahisi hazina hata gharama yaani bure kabsa
 
Nifahamishe kuhusu hiyo ya bure mkuu
 
Fafanua mstari wa mwisho
 
Mmekuwa wapumbavu sana wala hamna heshima na maisha ya watoto...Mnazaa mtoto baadae mnagoombana ni kumtafutia maisha magumu huyo mtoto.
 
Hii mada nimeenda nayo mpaka page three nikisoma soma maoni mawili matatu kutoka kwa wadau naona kuna wengine walishakuwa kwenye situation kama hii.

So mimi nadhani mpaka tulipofikia tuhitimishe tu kwa kusema kwa wale wanaojisikia wito wa kuoa watafute wanawake “BIKRA” hii peke yake ndiyo salama yao,mitaa imejaa malaya sana usipoenda kwa akili kupigwa toto la ex's wa kimada wako sijui mkeo ni kugusa tu chap unakuta hili hapa.
 
Umenena vyema na kwa hekima sana, yeye aendelee kumlea mtoto aachaane na hasira za huyo mama. Inaonekana mama mwenyewe kapinda.
 
Itakuaje ikiwa sio wangu na ntakuwa nimepoteza gharama zangu zaid, na itakuwaje kama baba yake yupo kwel kama mama yake anavosema siku akija kumdai mtoto kila mtu atanigeuka kwakuwa nimeshaambiwa sio wangu nikakaza fuvu
Wewe lea mtoto hadi pale itakapothibishwa vinginevyo. Kwani unatumia milioni ngapi? mtoto kazaliwa ndani ya malango yako unataka akalelewe na nani? Hata DNA huna haja ya kupima, fanya kadri ya uwezavyo na hutokuwa na cha kupoteza.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…