Uandishi wako mkuu una changamoto. Ila kuweka hayo kando, Computing & Communication Technology ni fani ambazo zina upana mkubwa kupita kiasi. Hardware, Software, Databases, Data transmission, Telecommunications, Data Encryption, Programming... Kila kitu kinaingia chini ya hizo fani na kila kitu ni kipana zaidi. Unabidi uende moja kwa moja kwenye maada ni nini unahitaji kukijua. Unahitaji kujua kuhusu hiyo kozi, ningeshauri kuwasiliana na aidha watu waliomaliza au wanaosoma katika chuo husika au uongozi wa chuo moja kwa moja. Au kama unahitaji kujua kitu fulani katika hizo fani basi ukiseme moja kwa moja kwani ni fani pana sana hizo