Utafiti wako uliishia wapi?Naomba wajuzi mnipe mnipe mwongozo wake ukoje. Nataka kufungua hiyo biashara ila sikupata muda wa kumalizia utafiti wake kwa namna ya kujiunga kwa waingizaji wakuu na mie niwe msambazaji wao. Kuna madogo nataka wajikwamue na mie niingize za mboga, sasa nahitaji wazoefu mnipe mawazo yenu, madogo sio wa kuwamini sana maana bongo kama muijuavyo vishawishi sasa nikijua vingine toka kwa wadau naweza nikajiongeza mwenyewe.
Asanteni na poleni kwa uandishi wangu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa nimekuelewa , shida yangu kubwa ni process za uwakala mkuu.mbuzi ukimchunguza sana hutamla......
hakuna biashara inayolipa haraka labda uuze madawa tu. Mitungi hawawezi kukuibia hao madogo zaidi watakukimbia maana watakuwa hawaoni pa kukuibia. Labda akuambie mtungi umepotea, nimedondosha pesa nilizouza mtungi
Sawa kabisa , delivery unaweza fanya mpaka 15 km bado faida ipo.kwanza uzuri wa hii biashara bidhaa zako zote zinahesabika vizuri pasipo na shaka, changamoto ni mzunguko wake inahitaji utafiti wa kutosha kuweza kupata eneo sahihi,au lenye afadhali yaan mzunguko wa iyo mitungi uwepo, pia ubunifu wa hali ya juu sana, mfano unaweza kufanya transportation free around 1.5km au chini ya apo au zaidi ya apo kulingana na usafiri ambao unao na kijana/vijana, unaweza wanunulia baskeli ya kawaida au ya kucharge ili wawe wanawapelekea wateja wanaacha na businss card hii mbinu ingesaidia kwa kiasi fulani, pamoja na mbinu nyingi za kunasa wateja,,,,,,,, mara nyingi maduka ya gas unawekamo na m-pesa, tigo pesa na related busnss kama izo.
wafuate mawakala wakuu ofisini ukawaulize watakupa utaratibu. Nadhani unatakiwa uwe na mtaji kiasi alafu wao wanakuja kukuletea mzigo unaotaka malipo unalipa kadri unavyouza taratibu. Nenda kila kampuni ya gesi unahitaji kuiuza mawakala wao watakupa utaratibu mzuri tu na rafiki kwa biashara yako. Huhitaji kuwa na mtaji mkubwa bali uaminifu wako
Asante sana kwa ushauri, mimi sipo hapo kwenye hilo zoezi ila nilitaka kupata maelezo toka kwa wadau ili vijana watakapo nipa mrejesho nilinganishe nione. Si unajuwa vijana wanaweza kukuletea na maelezo ya nyongeza ahaha.wafuate mawakala wakuu ofisini ukawaulize watakupa utaratibu. Nadhani unatakiwa uwe na mtaji kiasi alafu wao wanakuja kukuletea mzigo unaotaka malipo unalipa kadri unavyouza taratibu. Nenda kila kampuni ya gesi unahitaji kuiuza mawakala wao watakupa utaratibu mzuri tu na rafiki kwa biashara yako. Huhitaji kuwa na mtaji mkubwa bali uaminifu wako
Huo mtaji umechangamka na kwenye mchanganuo Kuna makosa kidogo ukiufuatisha Kama ulivyo mbeleni unakwama.Huo mtaji. Mhh lkn ahsante kwa mchanganuo, umenifungua akili
Habari wakuu, baada ya kuhangaika na cv sana maofisini...... Sasa naomba nijuzwe nataka kufanya hii biashara nipo Mbeya ambaye amewai kufanya hii biashara Msaada kuhusu mtaji na faida kwa kila mtungi na mchanganuo wake kwa undani faida na hasara.. Nawasilisha
Nitafute nikupe fursa ya tamu km u jasiri utapiga pesa mpk ulete ushuhuda hapa.
Pitia pm.