MSAADA: Kubadili jina na namba ya NIDA

MSAADA: Kubadili jina na namba ya NIDA

Pelly

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2013
Posts
286
Reaction score
363
Habari zenu wana jf,

Samahani naombeni ushauri kwa mwenye kufahamu.

Nina rafiki yangu alirudia darasa la sita miaka ya 80+ sasa akaendelea na sekondari na chuo na akaenda kupata degree yake Malaysia sasa amerudi nchini akaajiriwa sector binafsi na sasa ameacha anafanya mambo yake binafsi,

Changamoto aliyonayo ni kwamba aliporudia alibadilisha majina mawili yaani alitumia jina la kwanza lingine, la pili akaweka la baba yake ambalo anatumia kwa cheti cha kuzaliwa na la mwisho akatumia la babu yake, ambalo baadaye akaenda kuforge cheti chakuzaliwa kwa jina hilo jipya na kupatia passport mbaya zaidi alipunguza hadi umri wake

Kwa sasa ameenda kulikana jina jipya alilosomea na anataka kutumia cheti chake cha kuzaliwa cha zamani chenye majina ya baba yake mzazi na lake la utotoni, issue ipo NIDA je watakubali kumbadilishia namba maana kadi ya NIDA inaanza na mwaka wako wa kuzaliwa.

Asanteni na poleni kwa kuwachosha ila kama hujaelewa usisite kuniuliza

Sent from my SM-J700F using JamiiForums mobile app
 
It possible

Tafuta kiapo Cha mwanasheria /mahakama

Nakala ya jina lako jipya katika gazeti la Serikali

Cheti cha kuzaliwa

Pia nakala ya majina kutoka ardhi

Mkuu hizo process andaa 50k pia nenda kwa mwanasheria au nida wakupe information sahihi .
 
Tukusaidie umsaidie mdanganyifu.
Mwambie amuulize shetani aliyemrubuni kudanganya.
Wahenga walisema njia ya mwongo Ni fupi.

Kama hujapenda njoo unipige Niko Kimara.
 
Mbaya zaidi mwaka wa kuzaliwa umebadilika sababu jina la sasa hivi hadi kitambulisho na cheti kinaonesha kazaliwa mwaka 1990 wakati anataka kurudisha jina na cheti halali kazaliwa 1985 na majina anabadilisha mawili yaani mfano aliitwa Joseph James Maduu anarudisha Jimmy James Ndalo

Sent from my SM-J700F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom