Msaada kisheria: Kucheleweshewa mishahara

Mlachake

JF-Expert Member
Oct 13, 2009
4,412
4,559
Wandugu,
Vyuma vimekaza kweli kweli, Mhindi wangu mpaka leo hajanilipa mshahara wangu wa mwezi uliopita nahisi wa December ndio nitalipwa January mwishoni.

Hivi hakuna sheria yoyote inambana muajiri kwenye suala la kuchelewesha mishahara?

Nimeipitia labour law act karibu yote lakini naona maruweruwe
 
Wandugu,
Vyuma vimekaza kweli kweli, Mhindi wangu mpaka leo hajanilipa mshahara wangu wa mwezi uliopita nahisi wa December ndio nitalipwa January mwishoni.

Hivi hakuna sheria yoyote inambana muajiri kwenye suala la kuchelewesha mishahara?

Nimeipitia labour law act karibu yote lakini naona maruweruwe
Pole mkuu na hii kweli inaboa sana
 
Ishu hapa ungeelez Hyo mhindi anatoa sababu gan kuhusu kuchelewa kwa mishahara?ndo tujue tunakusaidiaj?
 
Sheria ya wafanyakazi na mahusiano kazini ktk kifungu cha 27 ambacho ni mahususi kwa ajili ya malipo ya mishaara, hakija sema chochote na sheria kiujumla ipo kimya tu, ila isipokua sheria hio sura namba 366 inasisitiza muajiri alipe kama mkataba unavyosema, sasa kuchelewesha kwa muda mrefu kulipa ni moja ya sababu ya kuuvunja mkataba.
 
Back
Top Bottom