Msaada: Kadi ya gari BMW X5 inahitajika

Msaada: Kadi ya gari BMW X5 inahitajika

Natafuta kadi ya gari BMW X5 kwa mtu ambaye gari ilipata ajali (haitengenezeki). Katika pitapita yangu nimekuta yard flani kuna gari BMW X5 inauzwa bei ya kutupwa ila haina kadi wala document yoyote. Muuzaji katoa sharti kuwa ili aiuze lazima uende na kadi ya Gari husika.
Msaada tafafhali.
Ni gari nzuri sana hata ukiona hutapenda kuiacha.
Napokea na ushauri pia.
Utafungwa...hivi unajua Kama ulichokiandika hapa Ni ushahidi Tosha wa kukupeleka Mahakamani?
 
Natafuta kadi ya gari BMW X5 kwa mtu ambaye gari ilipata ajali (haitengenezeki). Katika pitapita yangu nimekuta yard flani kuna gari BMW X5 inauzwa bei ya kutupwa ila haina kadi wala document yoyote. Muuzaji katoa sharti kuwa ili aiuze lazima uende na kadi ya Gari husika.
Msaada tafafhali.
Ni gari nzuri sana hata ukiona hutapenda kuiacha.
Napokea na ushauri pia.
Acha upuuzi.
Unatafuta kadi ya gari ili ukaghushi umiliki?
Usithubutu kununua gari lisilo na nyaraka kamili za umiliki..kesi za wizi, ujambazi na mauaji huanza hivi hivi.
 
Kama haina kadi usihangaike nayo hata kama inauza being chee mno. Ni bomu hilo, linasubiri mtu alishike wa-detonate.
 
Natafuta kadi ya gari BMW X5 kwa mtu ambaye gari ilipata ajali (haitengenezeki). Katika pitapita yangu nimekuta yard flani kuna gari BMW X5 inauzwa bei ya kutupwa ila haina kadi wala document yoyote. Muuzaji katoa sharti kuwa ili aiuze lazima uende na kadi ya Gari husika.
Msaada tafafhali.
Ni gari nzuri sana hata ukiona hutapenda kuiacha.
Napokea na ushauri pia.
Wewe unajihatarishia sana maisha yako,
Sitaeleza kwa undani lakini ujue tu hata hao wanaokujia PM kukwambia wanazo kadi za X5 ni mtego huo,
 
Wewe unajihatarishia sana maisha yako,
Sitaeleza kwa undani lakini ujue tu hata hao wanaokujia PM kukwambia wanazo kadi za X5 ni mtego huo,
Umenena vema sana Shark; huyu anayetafuta kadi ya gari JF hajui matokeo ya anachokifanya. Mpaka sasa ameshahatarisha usalama wake na wa muuzaji wa hiyo BMW X5 inayotafutiwa kadi kinyemela. Kadi ya gari inatolewa na mamlaka husika (TRA) baada ya kuwasilisha kwao kumbukumbu zote za gari husika zikiwemo na taarifa (particulars) za gari husika kama namba ya model, engine, chassis, rangi, aina ya bodi na mengine mengi. Taarifa za gari moja haziwezi katu kufanana na za gari nyingine, hususan namba ya engine na chassis. Hayo yote hufanyika endapo tu gari hilo limeingia kihalali kwa kuonyesha nyaraka zote husika zikiwa sahihi. Kama huyo muuzaji aliingiza hiyo gari kihalali na iko show room na amepata mnunuzi, kwa nini asishughulikie usajili wa gari hilo TRA, badala yake anakutuma wewe utafute kadi? Utaipata wapi kadi yenye taarifa za hiyo gari ambayo haijasajiliwa? Achana na huo ujinga, utapotezwa! Nauita ujinga kwa sababu labda ulikuwa hujui, sasa umejua; ukiendelea na huu ujinga, utageuka na kuwa upumbavu na utaingia kwenye mdomo wa mamba wala hutatoka humo. Kama unataka mambo ya konakona usiyalete humu; utaumia.
 
What if nikienda kuikagua na fundi wangu na tukapeana guarantees wakati wa kufanya biashara?

And what if ukipata kadi na ukanunuga gari hilo alafu baada ya wiki ukakamatwa kwamba gari nilawizi [emoji84]
 
Back
Top Bottom