Msaada: Kadi ya gari BMW X5 inahitajika

Msaada: Kadi ya gari BMW X5 inahitajika

Huyo jamaa anatafuta kadi ya gari yake iliyoibiwa, nyie hamjamgundua tu, anamtafuta mwizi wake kwa staili hii
 
Yaaaan yeye anauza gari lakini wewe mnunuz ndo uende na kadi? Au sjaekewa. Kuna ktu unatafuta....
 
Of course not. Ninachotaka ni kadi tu
Wewe hujui hata kadi ya gari inaandikwa nini. Maana hiyo gari yako haifanani chassis number na kadi unayotafuta, Rangi, mwaka ilotengenezwa na kadhalika. Kama unataka mradi kadi inayofanana na kadi ya gari nenda Stationary yoyote na kadi ya gari ya shemeji yako watakutengezea inayofanana ambayo Road licence utalipia kwa dada yako maana Ukienda kulipa TRA utaishia Segerea
 
Dili ya wizi imetokea wapi? Au unafkr kila mtu ni mpiga dili humu? Kama huna msaada kwa nn usikae kimya tu?
Hapo huo ni wizi mkuu, unajua kwani ni hiyo gari haina card. Sababu ni mbili tuu either imeingia nchini bila kulipiwa ushuru na sababu ya Pili ni kuwa imeibiwa.
Kama sababu ni hizo hauoni unataka kushiriki wizi moja kwa moja?
Hizi deal watu wa mkoa Fulani walifanya sana miaka ya nyuma ila sasa hivi hakuna anaethubutu ogopa sana kuingia mikononi mwa askari wa Interpol Kijana au TRA ya Magu
 
Natafuta kadi ya gari BMW X5 kwa mtu ambaye gari ilipata ajali (haitengenezeki). Katika pitapita yangu nimekuta yard flani kuna gari BMW X5 inauzwa bei ya kutupwa ila haina kadi wala document yoyote. Muuzaji katoa sharti kuwa ili aiuze lazima uende na kadi ya Gari husika.
Msaada tafafhali.
Ni gari nzuri sana hata ukiona hutapenda kuiacha.
Napokea na ushauri pia.
Ngoja jamaa wa TRA wakuchomekee hapa ndipo utakapojua gongo si chai. Ajabu sana unaweka ombi hili open kwenye mtandao.
 
>> utapata matatizo ww Hiyo GARI sio nunua tu vits Utanue MJINI >>>
 
Ni kadi ipi mkuu ? kama ni hizi zinazotelewa na TRA mmh usifanye hiyo mambo... lakini nakushauri mwambie huyo jamaaa mmliki wa gari akachukue loss report police then aende TRA kwa ajili ya kuprocess kadi mpya... lakin kama gari ya magumashi hapoo mmmh bora kudeclare alipe kodi ya serikali mchezo uisheee...
 
Bwashe Kadi ya gari sio Kama ya ccm... Kuna taarifa muhimu sana zipo kwenye Kadi haziwezi kubadilishwa kirahisi. Halaf, hata ukipata hiyo ya mbovu unajua kuwa utatakiwa uilipie tra kwa Muda ilolala afu ndo ununue hiyo ya Dili??? Futa namba ya huyo anaetaka kukuuzia, atakuingiza pabaya. Gari sio ice cream. Na haswa kipindi hiki.
 
Insurance utakata vipi mkuu? au unakurupuka tu. Kama uwezo wako ni dagaa kula dagaaa usitamani nyama. Ukitamani nyama ukafanya magumashi upate nyama utapata nyama mbovu mwisho wa siku utahara
 
Bwashe Kadi ya gari sio Kama ya ccm... Kuna taarifa muhimu sana zipo kwenye Kadi haziwezi kubadilishwa kirahisi. Halaf, hata ukipata hiyo ya mbovu unajua kuwa utatakiwa uilipie tra kwa Muda ilolala afu ndo ununue hiyo ya Dili??? Futa namba ya huyo anaetaka kukuuzia, atakuingiza pabaya. Gari sio ice cream. Na haswa kipindi hiki.
Hawezi kukuelewa.
 
Ninachokiona hapa ni watu ambao hawaijui wanachokiongea.. Wenye uelewa mdogo
 
Back
Top Bottom