Msaada juu ya Kusafiri na Gari za IT

Msaada juu ya Kusafiri na Gari za IT

Mamaya

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2011
Posts
5,238
Reaction score
4,740
Heshima mbele wanabodi.
Niko Dar kwenye pilikapilika ambazo nategemea kuzimaliza kesho Alhamis mchana saa nane. Nataka nigeuze kwenda makambako ila nataka nipande gari za IT ili nifike Ijumaa asbh, naombeni msaada wapi naweza kuzipata hapa Dar na naweza kwenda kupandia wapi,au kama kuna mwenye no za suka yoyote anaaendesha gari za IT anisaidie.Lakini pia ushauri kama upo nipeni maana ni first time nataka nipande hizi gari za IT
.
Natanguliza shukrani.
 
mkuu huwa zinasimama pale mbezi mwisho karibu na kanisa romani,ni ushauri tu hizo gari
huwa zintembea vibaya sana kama una moyo mwepesi panda bus....
 
Jamaa kasema vema ila hata pale Misugusugu customs zinasimama kwa taratibu za forodha, angalizo lingine ni kuwa unatakiwa kuwa risk taker ( kitu ambacho mtu wa Makambako nadhani ni kawaida) hawana bima wale jamaa na usiku ndio traffic police wanaweza kuwa nafuu maana haziruhusiwi kupakia abiria, otherwise saa kumi na mbili asubuhi upo MKB.
 
kupanda IT inawezekana umejichoka ila plz zingatia ushauri uliopewa, wengi wa madereva wa IT hawajawa na uzoefu wa kuendesha gari na pia hawana uzoefu wa kuendesha gari umbali mrefu mfano wanataka kukesha kuendesha gari barabarani hadi usingizi unawasababishia ajari na kumbuka wapo kwenye 'highway', fanya uamuzi mzuri!
 
Heshima mbele wanabodi.
niko dar kwenye pilikapilika ambazo nategemea kuzimaliza kesho alhamis mchana saa nane. nataka nigeuze kwenda makambako ila nataka nipande gari za IT ili nifike ijumaa asbh, naombeni msaada wapi naweza kuzipata hapa dar na naweza kwenda kupandia wapi,au kama kuna mwenye no za suka yoyote anaaendesha gari za it anisaidie.lakini pia ushauri kama upo nipeni maana ni first time nataka nipande hizi gari za it.
natanguliza shukrani

Pale kidongo chekundu unapoanzia mtaa wa livingstone, kuna coster za mbeya na huondoka nida ya saa 8 hadi tisa kuelekea mbeya, wahi hizo IT ni nomaaaaaaaa
 
Pale kidongo chekundu unapoanzia mtaa wa livingstone, kuna coster za mbeya na huondoka nida ya saa 8 hadi tisa kuelekea mbeya, wahi hizo IT ni nomaaaaaaaa

mkuu hizo coster nauli bei gani?
 
Mkuu,
Kupanda IT si uamuzi mbaya kwani huwa napanda sana. Tatizo huwa ni uzoefu wa madereva na spidi zao. Ila mara nyingi wale wanaopakia abiria huwa ni madereva ambao washakuwa na uzoefu kiasi wa kuendesha kwenye highway. Kuzipata nenda Kimara Rombo, lakini pia waweza kupanda Coster pale Kidongo chekundu.
 
Jamaa kasema vema ila hata pale Misugusugu customs zinasimama kwa taratibu za forodha, angalizo lingine ni kuwa unatakiwa kuwa risk taker ( kitu ambacho mtu wa Makambako nadhani ni kawaida) hawana bima wale jamaa na usiku ndio traffic police wanaweza kuwa nafuu maana haziruhusiwi kupakia abiria, otherwise saa kumi na mbili asubuhi upo MKB.

misugusugu ni wapi mkuu
 
Sifahamu, ila kama ishu ni nauli? panda fuso ndio the cheapest buku 2 umefika makambako, wapandia pale kimara kibo mida ya jioni jioni

hiyo fuso si ndo bitafika hata usiku ijumaaa? maana target yangu ni kufika asbh
 
dah, mbona mwantisha kuhusu hizi gari za It, mi huwa naona zinakatiza tu asbh nikafikiri ziko poa, kumbe ni hataaaaare kiasi hiki?
 
Karibu ulanzi wa kichanga.Nenda Ubungo stand ya mkoa unaweza kupata private car,au lazima iwe IT!
 
Karibu ulanzi wa kichanga.Nenda Ubungo stand ya mkoa unaweza kupata private car,au lazima iwe IT!

nikipata hizo private mbona itakuwa poa. nimesema it kwa sababu daily zipo excepr jmos na jpili. sasa ubungo stend ya mkoa wapo? na nitajuaje hili linaenda mbeya,songea au njombe?
 
we mbufi sana!!umeambiwa nenda pale UBT!!!CI UKAULIZIE PALE TERMINAL!!!MBONA HUJIAMINI HIV??????WE MBENA WA WAPI UCIYEJIAMINI
 
Wakuu nimerudi jana tu kutoka Ruvuma, kwa kweli idadi ya gariza IT zilizomalizikia njiani kwa hesabu za haraka haraka zilifika sita. Hii ilinilazimu kumuuliza dereva wangu hii inasababishwa na nini, dereva wangu kumbe naye kabla ya kupata ajira rasmi alishawahi kufanya kazi kama hizo tena kwamalipo mazuri (si chini ya laki mbili).

Anasema tatizo mmiliki wa gari la IT anajikuta anatafuta dereva wa bei chee vijiweni na kukwepa wale wazoefu, matokeo yake wanajikuta furaha yote ya kupeleka gari nyumbani inaishia porini, na kibaya zaidi hata na maisha yao yanaishia hapo hapo.

Barabarabi kuna changamoto nyingi zinataka dereva uwe na uzoefu wa kutosha kwanza ukianzia na barabara husika pamoja na ozoefu wa kutosha wa tabia ya gari lako (Zijue breki zako kwa ufasaha, tairi zako na life span yake, upepo wake uko sahihi kw asafari ndefu kama hizo nk).

Ndugu mtoa mada nafikiri utakuwa umepata pakuanzia utafiti pia, sio tu kila gari upande je na uzoefu wa dereva kwa safari kama hizo upo?
 
nikipata hizo private mbona itakuwa poa. nimesema it kwa sababu daily zipo excepr jmos na jpili. sasa ubungo stend ya mkoa wapo? na nitajuaje hili linaenda mbeya,songea au njombe?

Madereva wengi wa IT ni wa vijiweni. Pia gari nyingi tunazonunua toka Japan (used) tunabadirisha tairi ili tuwe salama hasa kwa safari ndefu (kwa IT hilo sina hakika). Wiki iliyopita nimetoka Mbeya/Iringa, nimeona IT 2 zilizopata ajali kiasi cha kutelekezwa (beyond repair) nafikiri watakua walifungua vitu vya muhimu tu. Moja ipo kabla ya Ruaha mbuyuni na nyingine ni baada ya kupita Ruaha mbuyuni. Think twice.
 
Inategemea dereva utakaye mpata kama anauzoefu kiasi gani,ila kwa ufupi zile gari zinatembea balaa! Mimi nlishasafiri nazo kwenda Iringa muda ambao nlifika ckuamini.
 
IT kifo nje nje nilipoteza hawara aliyekuwa akinipa yote, nilimkataza kupanda IT akawa mbishi nikamwambia bora adake Fuso alikataa kona za lyofi zilichukua uhai wa kiburudisho changu.
 
  • Thanks
Reactions: ram
Jamani, on a serious note gari za it ni gari gani? Mimi nafikiri ni ninapoziona zimeandikwa it maana yake imetoka bandarini na inaenda kuwekwa namba. Kwa maelezomyenu wajuvi ni kama vile yaaani na zenyewe zinapigaga route kwenda na kurudi.
 
Sifahamu, ila kama ishu ni nauli? panda fuso ndio the cheapest buku 2 umefika makambako, wapandia pale kimara kibo mida ya jioni jioni

Huyu jamaa hayuko serious, waswahili wanasema msafiri pwani. Kila kitu anataka atafuniwe.
 
Back
Top Bottom