Msaada juu ya Antena ya King'amuzi cha Star Times

Sambwisi

Senior Member
Nov 12, 2010
175
67
Wana JF Nimenunua king'amuzi cha Star Times. Wauzaji waliniuliza hali ya ninapoishi na kunishauri nitumie antena ya kawaida ili mradi tu inashika TBC kwani ile ya kwao ndogo haitashika mawimbi (signals). Nimefanya hivyo lakini inashika Channel 20 tu. TBC, Chanel 10 hazishiki. Nilipowauliza wakaniambia nitafute antena nyingine yenye nguvu ziaidi. Natumia antena aina ya Airstar (inayozunguka) naishi Mtoni Kijichi, bondeni kidogo kabla ya kufika Maghorofa ya Polisi (Zamani Nasaco)Ombi langu ni kutaka kujua ni antena ya aina gani na vipimo gani ambayo naweza kufunga na kupata channel zote za Star Times?Nawasilisha
 
Wanadai antena zote zielekee kisarawe kaka harafu kwenye deck yao hapo kuna taa mbili zinawaka moja red na ya pili ni njano hivi kwa ajili ya signal kama haijawaka mkuu rekebisha antena yako fresh tu!jipe moyo!
 
Kama uko bondeni pandisha sana juu hiyo antenna na ni vizuri kama ungetumia antenna za kwao na antenna haitakiwi icheze cheze utakapofunga antenna ndio hapo hapo coz hizo antenna zinafuata mawimbi kama ya dish za satellite ikisigea nyuzi moja tu inaanza kusumbua.
 
Back
Top Bottom