Wana JF Nimenunua king'amuzi cha Star Times. Wauzaji waliniuliza hali ya ninapoishi na kunishauri nitumie antena ya kawaida ili mradi tu inashika TBC kwani ile ya kwao ndogo haitashika mawimbi (signals). Nimefanya hivyo lakini inashika Channel 20 tu. TBC, Chanel 10 hazishiki. Nilipowauliza wakaniambia nitafute antena nyingine yenye nguvu ziaidi. Natumia antena aina ya Airstar (inayozunguka) naishi Mtoni Kijichi, bondeni kidogo kabla ya kufika Maghorofa ya Polisi (Zamani Nasaco)Ombi langu ni kutaka kujua ni antena ya aina gani na vipimo gani ambayo naweza kufunga na kupata channel zote za Star Times?Nawasilisha